CCM inajiandaa kukabiliana na mbwa waliyemfuga kwa kumnyima uhuru kwa kumweka bandani kiasi cha hata kwenda haja, wamemkadiria masaa

CCM inajiandaa kukabiliana na mbwa waliyemfuga kwa kumnyima uhuru kwa kumweka bandani kiasi cha hata kwenda haja, wamemkadiria masaa

mkulimamiwa

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2025
Posts
2,254
Reaction score
4,466
Mbwa aliye huru ni rafiki wa kila mtu, labda umchokoze

Mbwa aliyefungwa na kutiwa minyororo bandani, hana rafiki, hata anayempa chakula, siku atakapojua haki zake, atamtia majeraha, atamchapa meno mpaka boss wake

Ndicho sisiem walichowafanya Watanzania, waliwafungia bandani miaka mingi huku wakiwatishia eti mkiwapa wapinzani kutakuwa na vita, 🤣🤣, ila ccm nyie...!!

Watanzania kujua haki zao imekuwa ni kosa, wao wanachokifanya, ni kuwateka, kuwauwa na kuwapeleka magereza bila hata sababu

Haki ya kuchagua ipo, haki ya kuwa na tume huru, hii haipo, na hii ndiyo vita kali iliyopo na ndilo dai kubwa kwa vyama vyote hata ccm wenyewe

Haiwezekani, tume iundwe na Rais ambaye pia anaingia kwenye kinyang'anyilo cha kupigiwa kura! Huu ni wizi wa wazi wazi

Hiki ndicho kilio cha Watanzania

Sasa Mbwa kajua haki zake, ni mkali hataki kusogelewa hata na boss wake, maana kesha kata mnyororo na kupenda vya kujitafutia!

Kwa hali hii, CCM mnadhani mtalazimisha hivi mpaka lini?
 
Back
Top Bottom