CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

Wanabodi,

Nikiwa hapa Dom, nimebahatika kukutana baadhi ya wabunge wapya wa CCM na wa kambi ya upinzani, kujaribu kufahamiana, sio siri, baadhi yao hawana hata substance ya ni nini kilichowafanya washinde, na kwa viti maalum ndio usiseme kabisa!, wengi wao kama si makapi tuu, basi ni vidumu, basi ni kwa ajili ya kutoa huduma na kibinaadamu!, na hili litathibitishwa na michango yao kikao cha Januari.

Nilipoongea na baadhi ya wale makamanda waliokata magogo kanda ya ziwa, nimewaona ni wa kawaida tuu, hivyo nimefikia jibu moja la uhakika, kuwa CCM katika baadhi ya maeneo, imechokwa mpaka basi!, upinzani hata ungesimamisha jiwe, lingechaguliwa!, nadhani ni moja ya sababu kuu iliyopelekea wengi hawakujitokeza waliona kujitokeza kupiga kura ni kujisumbua tuu!.

Nasisitiza CCM imechokwa, na ule ushindi wa kishindo wa toka Asilimia 80% niliyohakikishiwa na mwana CCM mwandamizi mpaka asilimia 60% ni uthibitisho tosha, Watanzania wameichoka CCM ila pia hawakuwachagua wapinzania kwa wingi zaidi, kwa sababu wapinzani hawajaonyesha wako tayari kukamata dola.

Najua kwa dhati, japo JK anafurahia ushindi kwa furaha ya machoni, lazima atakuwa na huzuni moyoni kwa kukataliwa na hiyo asilimia 20% kukataliwa ni kukataliwa tuu, kunauma. Hivyo CCM lazima watakaa na kujiuliza kulikoni, huenda wakajipanga upya na kuja kwa mbinu mpya, ila kwa vile CCM imechokwa, hata ijipange upya vipi, safari ya kwaheri ndio imeanza, there is nothing to stop it from failing down!.

Dawa pekee ya kuitibu CCM, ni kuirevamp CCM completely, task nambari moja ni Makamba should go first with his old guards team. Msisubiri mpaka uchaguzi mkuu wa chama chenu, miaka miwili ijayo (2012), itakuwa too late. If you are to du anything, doi it now and fast!. Leteni fresh blood kina January type, Kippi, Nape type and the like ambao wanaweza siasa za kisasa za dot com type.

Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.

Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa kwenye Usukani, Katibu Mkuu mpeni Zitto, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, ili Walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kuwapigia kura 2015.

Kitendo cha kuihodhi kambi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani, Chadema peke yenu hamuwezi!.

Kama CCM iko ICU na Chadema haijajipanga, spika ndio huyo mama ma over confidence na over reaction, 2015 tutegemee nini?.

Angalizo: Pasco wa Jamii Forums ni political commentator ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!

Ccm imechokwa na mafisadi
Wasiopenda kufanya kazi kwa bidii

Vibaka

Walevi
Na malofa

Ambao wanaogopa kasi ya magufuli
 
"Dr.W.Slaa

Dr. Slaa, asante sana kwa kunijibu, kitendo tuu cha kuonyesha umenisoma, hiyo ni faraja tosha kwangu kuwa hata kama hamtayarekebisha mapungufu, my only defence ni kuwa tuliwaambia, mesej sent.

Kwa kuanzia, nakupongeza sana wewe binafsi kugombea, umeleta changamoto ambayo haijawahi kutokea.Ushindi wa hayo majimbo mliyoyatwaa ni uthibitisho wa the powers within you. For the first time in my life, nimehamasika na naweza kutupa karata yangu mahali 2015.

Pole kwa kutopata ushindi uliotarajiwa, ila amini usiamini, wewe bado ni mshindi kwenye roho za watu, na JK ni mshindi kwenye makatasi ya kura. Tunatakiwa kuwa wa shukrani kwa kidogo chochote tunachopata, wewe mwenye majimbo 5 hadi 22 na la 23 ni kesho, ulitakiwa kuonyesha appreciation kwa Watanzania waliokuamini, kitendo cha kususia kutangazwa matokeo for whataver reasons, ni political immaturity, na binafsi nilifadhaishwa sana, umepoteza the golden opportunity ya kuspeak out you mind, hata kama hatimaye utakuja kuita waandishi na kuyasema ya moyoni, never will they have the impact kama ungejitokeza pale na kusema nimekuja siyakubali matokeo kwa sababu yamechakachuliwa.

Nakubaliana na wewe kuhusu weakneses kwenye analysis yangu, infact kitu nilichokisema hapa, its only my observation. True analysis inapatikana baada ya kufanya research, nakiri sijafanya research yoyote serious zaidi ya observation tuu, ila hili jicho langu ndilo la mwananchi wa kawaida kule kijijini na sio jicho la reseacher as a member of academia.

La kambi ya upinzani, nimelisemea, if you go by the books, it is ok kwa vile nyinyi peke yenu mnaconstitute ile quoram kwa mujibu wa kanuni, don't play by the book, just play by reality, logic and moderation. Umimi wenu Chadema, haujaanza leo, msipokubali weaknesses zenu, you can not turn them ito streghths. Naomba nisiende tena kwenye personalities zaidi, tunakuomba kaa siti ya mbele, shika usukani, pangeni safu yenu vizuri, futeni dhana zote zilizojengeka dhidi yenu ziwe za kweli au za kizushi, 2015 ikulu ni yenu, maana wale milioni 12 waliojiandikisha halafu hawakupiga kura, ndio mtaji wenu wa 2015 haswa ukizingatia vijana wa shule za kata ndio watakuwa vyuoni!.

Asante tena.

This time chadema wamepaniki kutokana na kosa walilofanya la kuuza chama kwa mafisadi papa.
 
Wadau nimejaribu kutafakari kuona kama kura yangu niwape CCM lakini nimefanya uamuzi wa kuwapa UKAWA.
Sababu ni hizi;
(1) Kwa muda wa miaka 53 maisha ya tulio wengi ni magumu. Si mijini au vijijini maisha yanakuwa magumu kila siku.
(2) Ajira kwa vijana tulio wengi hakuna. Kazi ni shida kupata ndani ya CCM. Hata ukisikia kazi kama NSSF au Bank. Ukienda kwenye interview utasikia mko watu 500 mnaogombania kazi 20.
(3) Kwa miaka 53 umeme umekuwa shida kote mijini na vijijini.
(4)Kwa miaka 53 maji ni shida.
(5)Kwa miaka 53 huduma za afya mbovu. Hakuna dawa na upungufu wa vitanda wodini.
(6) Kwa miaka53 sekta ya utalii imeshuka kwa viongozi kuuza Wanyama wetu na kusafirishwa nje
ya nchi. Sijui wamefikiria nini kuuza. Maana wao wakiwa na wanyama huko kwamfano Dubai.
Unadhani watakuja kuangalia wanyama Tanzania.?Tafakari!!
Kwa sababu hizo hapo juu nashindwa kuwaamini hawa watu ambao kuongoza nchi kwao imekuwa mazoea tuu. Na
hakuna ufatiliji wa utatuzi wa haya matatizo. KIJANA WA LEO TAFAKARI KWA KWELI!!!!! JE UTAISHI HIVI MPAKA LINI ??. USIANGALIE KWAKO BINAFSI HATA KAMA UNAKAZI SASA. ANGALIA MAISHA YA WATANZANIA WOTE WAKATI UNAPIGA KURA.
 
Alafu kuna watanzania wanaishabikia ccm. Watanzania ni wa kupimwa akili.
 
Bahati mbaya hao masikini na mafukara ndo wanaipenda sana CCM!!
 
mtaji wa ccm kwenye kura ni umasikini na ujinga unaosababishwa na rushwa na kujuana...
 
Hii inaonyesha jinsi gani mfumo wa elemu ulivyokuwa mbovu ndani ya CCM na kufanya vijana tunaopata shida, malofa kusahau shida na kuwabeba hawa watu kwa sababu tunaletewa fiesta za kina wema, Ali kiba na diamond kwenye kampeni. Huu ni Ulofa aiseee!!!!
 
Ndio maana TUNAHITAJI MABADILIKO,ili tutoke kwenye haya mateso ndani ya nchi yetu wenyewe.
 
Richmonduli hio baba...eti leo tumpe Ikulu ujinga mtupuu..
 
CCM is not for people's interest and/or benefits, except for enriching itself.
 
Tumechelewa sana kuwaondoa watu hawa kupitia sanduku la kura.
 
Watanzania wenzangu ni miaka 50 na zaidi CCM inatutesa kimwili kiuchumi na kiimani. Maisha yetu yamekuwa magumu ajabu.Watanzania wamechoka Na wameishiwa pumzi.

Ukiumwa bila ya Hela hujatibiwa kila kitu ni hela, ni Hela tu.Ajira kwa watoto wa maskini hakuna zimebaki za watoto wao.Mikopo ya elimu in kwa watoto wao wa maskini ni kuuza mashamba na mifugo.Vijiji imebidi vijana tukimbie tuje tutafute maisha mijini.

Taabu zote hizi ni Utawala mbovu wa CCM .

Nawaomba wote WATANZANIA TUIOGOPE CCM KAMA UKOMA
 
Nini ukoma?Mimi naiogopa CCM kuliko Israeli mtoa roho!
Maana inatesa halafu haiuwi,bora Israeli akija anachukua chake kiroho safi.
 
Saloon yako umefunga kisa umeme alaf unasema kazi tu
Umealikwa mahali umeenda bila kunyoosha nguo af unasema hapa kazi tu
Unaishi kwa dada ako nyama imeharibika kwenye fridge unabwabwaja hapa kazi tu.
Umeme umerudi ghafla kwa dada ako ukaunguza kila kitu af unacheka hapa kazi tu.
Kaka ako shughuli zimekwama huko ofisini anarudi hana raha we umejitanua hapa kazi tu.
Simu yenyewe umepewa imezima charge unashindwa kuwasiliana af unakazana hapa kazi tu.
We huoni maisha ni magumu kadri siku zinavozidi kwenda, umekaa tu hapo na lipensi lako la kijani na nyekundu unawaza hapa kazi tu.
Unatakiwa kuchomwa ile sindando ya kuboost akili
Watu wana hasira
 
Back
Top Bottom