CCM imechanganyikiwa?

CCM imechanganyikiwa?

Vyasaka msituletee upuuzi wenu.

Fanyeni mfanyavyo, ila msituchokoze na siasa zenu za kipuuzi.

Sisi ni wachapa kazi.

Majungu pelekeni kwenu, pumbavu kabisa
Washamba wakisukuma munakaxi gani munafanya washamba nyie
 
Unaheshimika sana humu kiasi siamini kuwa ungesema hivyo kwamba Wakati ni hakimu mzuri. Vipi jicho lako la tatu!
Ndio maoni yangu hayo sina zaidi... Kuhusu jicho la tatu sijajua una maanisha nini
 
Bora umekiri wewe ni mshamba na zumbukuku ila siyo mimi.
Hata magu ukimuuliza atakuambia sio mshamba na zumbukuku.
Hapa tunazungumzia nchi na sio individuals. Use muelewa basi!
 
Naweza kusema NDIO. Kama kaenda kuomba mkwe aonewe huruma na kuachiwa, naye akapewa sharti LA kusema Yale hadharani ili msamaha upatikane huko sio kununuliwa?
nani wa kuaminiwa CDM?
 
Huu ni zaidi ya utoto na ulemavu wa kukosa tafakuri... Haya yanayoendelea nchini nikiri wazi kuwa pamoja na kwamba kuna matukio ya kutisha ya kuwashambulia wapinzani kwa silaha za moto na silaha nyingine zenye kujeruhi na kusababisha ulemavu....

Lakini hili la kutumia ushawishi wa ahadi za mali pesa vyeo na ulinzi kwenye bishana ili watu warejee ccm ni uhuni na michezo ya kitoto kabisa

Tusijaribu kuwaiga Rwanda.... Ukubwa wa ile nchi ni sawa na mkoa mmoja wa Tanzania... Tusiige zile siasa kuna kuna mvutano wa makabila mawili... Siasa za pale zinahusika sana na ukabila
Tumeshashuhudia yaliyotokea kwenye uchaguzi wa madiwani hivi karibuni, watu wameumizwa sana.. Watu wamejeruhiwa sana, watu wamebambikiwa kesi sana... Hii ni ishara gani kwenye uchaguzi 2020?(kama utakuwepo lakini) tofauti ya hoja ndio tuumizane kiasi hiki? Vyombo vyetu vya usalama na tume ya uchaguzi vimevaa miwani ya mbao

Kama hii haitoshi pamoja na kufanya yale yote kwenye uchaguzi ule sasa ni mwendo wa kununua wapinzani... Naamini kuna kundi kubwa sana ndani ya ccm wanashangazwa na haya lakini hawana pa kusemea.. Hawa wanaonunuliwa wanaenda kutupwa huko... Ni uchoyo na ulafi wa aina yake... Ni sawa na kuwa na makabati ya nguo lakini bado unataka na za jirani....

Hawa wanaonunuliwa hawaendi kuonyesha vipawa vyao huko, wanaenda kuminywa na kufichwa ili mradi tu kukomoa kaliba fulani ya watu...

Hivi kipaumbele ni kuua upinzani? Ingekuwa mashindano yako hivyo kusingekuwa na kushindana basi... Tunapoteza muda mwingi kwenye siasa za kipuuzi kabisa.. Mwisho wa siku morali wa kujenga taifa unashuka kabisa.... ccm halisi wanabaki na kinyongo, ccm makinikia wanakuwa na hofu na kutojiamini.... Mwendo mpya wa kuwindana kusimangana na kuchomeana unaaza.... Ni aina gani hii ya siasa mnafanya?

Mtanunua wangapi? Mtawabana wangapi ili waombe Po na kujiunga nanyi? Kumbukeni kuna kura million 6 +, tena hizi mmezitamka nyie... Uhalisia ni kwamba zipo zaidi ya hapo tena kwa mbali sana....

Tunawakemea kwa sauti ya uzalendo hamjengi bali mnabomoa, hamtengenezi bali mnaharibu.. Hamuunganishi bali mnatenaganisha.... Huu ni uwendawazimu na kukosa tafakuri... Hivi mmesahau kuwa WAKATI SI MILELE?!?!??

Kwa tahmini ya kisayansi pia ungejiuliza hao wanaonunuliwa ni wanachama wa aina gana na kwanini wanunuliwe kama kweli wameshiba itikadi ya vyama vyao? Kweli mtu anayeamini misingi ya chama chake anaweza kweli kununulika? Huwezi kuona tatizo upande mmoja tu na kuacha mwengine, otherwise, tathmini yako inakuwa haina maana sana zaidi ya kujaza server. Jaribu sana kwenye uandishi kubalance na sio lazima uonekane mnazi tu wa cham flani.
 
Kwa tahmini ya kisayansi pia ungejiuliza hao wanaonunuliwa ni wanachama wa aina gana na kwanini wanunuliwe kama kweli wameshiba itikadi ya vyama vyao? Kweli mtu anayeamini misingi ya chama chake anaweza kweli kununulika? Huwezi kuona tatizo upande mmoja tu na kuacha mwengine, otherwise, tathmini yako inakuwa haina maana sana zaidi ya kujaza server. Jaribu sana kwenye uandishi kubalance na sio lazima uonekane mnazi tu wa cham flani.
kwahiyo Mugisher unataka kunipangia cha kuandika? Mbona heading iko wazi kabisa? Kama una wazo mbadala au unapingana na nilichoandika.. Jenga hoja yenye mashiko sio kuanza kuniambia ningeandika hivi ama vile
 
Ni wajinga pekee ambao wangeweza kununulika kwa thamani ya kuikana imani yake na itikadi wanazoziamini na kuzisimamia, wajinga kama hao siamini kama wangeweza kupatikana kwenye chama kinachojinathibisha kuwa ni "chama makini". Msihangaike kumtafuta mchawi bali mjitathimini wenyewe kwanza.

Sote tunaishi mitaani na tunayaona yanayoendelea kwa sasa, tunaingia kwenye vikao, tunasikiliza maoni ya wana mitaa wenzetu, Kuhusu kununulika kwa mazingira ya huku sijasikia, ila kuna uwezekano madiwani wengi wa Cdm 2020 eidha wakaacha kugombea ama wakagombea kupitia Ccm ingawa nalo ni gumu. Ukiondoa vita dhidi ya ufisadi, umeiondoa Cdm kwenye ramani, kosa lilianzia hapo tu.
 
Mkuu mshana tusione kimya huko ccm nako hakufai, wanalalama wapinzani wanavyopokelewa kwa shangwe na kupewa vyeo na thamani kubwa wakati wao wafia chama wameachwa solemba.
Hilo liko wazi ndio maana hakuna shangwe kabisa
 
Inasikitisha kuona kuwa kwa kiasi fulani JK alitusogeza mbele kiustarabu lakini ghafla tumerudi nyuma sana na kuwa washamba na mazumbukuku.

Angalau sasa umewajua washamba ni akina nani. Uliokuwa unawadhania washamba wamekuonesha wao sio washamba, sasa mshamba ni nani? Jibu unalo
 
Kama kuna ushahidi wa ccm kuhusika ni kweli inapaswa kukemewa kwa nguvu zote, lkn wasi wasi wangu makamanda jahazi linatoboka baada ya kujadili nini tatizo mnakuja na visingizio lukuki. Wanachama wanakimbia eti oohh wanahongwa sababu nyepesi kweli kweli.

Kwa sasa mmekosa mtu kama slaa mnabaki kulia lia tu mitandaoni. Ukweli ni kuwa mmewaangusha wananchí hata kabla ya kupewa dola, mlichobakisha kwa sasa kila anaekuambieni ukweli eti ccm. Edo na wengine kadhaa wapo njiani nyie katafteni flash mseme wanahongwa.
Kichaa ulishawahi kuona ccm ikipitisha mgombea ubunge bila kikao chochote wala kura ya maoni toka enzi za mwalimu?
Nikuhakikishie wakiimaliza chadema wanahamia wao kwa wao yaa ccm asili(wanaoijua ccm miiko yake taratibu zake na asili yake dhidi ya ccm washamba wa siasa(waliokurupukia siasa wasiojua ccm ilitoka wapi miiko yake na misingi)
Na mwisho wa siku mshindi anajulikana
 
Lakini hili la kutumia ushawishi wa ahadi za mali pesa vyeo na ulinzi kwenye bishana ili watu warejee ccm ni uhuni na michezo ya kitoto kabisa

Siyo kweli - Jibu hoja hizi:-
(i) Siku Lowassa amehamia kwenu mlipa fedha kiasi gani?
(ii) Siku Masha amehamia kwenu mlimlipa fedha kiasi kipi?
(iii) Siku Nyarandu amehamia kwenu mlimlipa nini?
(iv) Siku Kingunge amehamia kwenu mlimuahidi nini?
(v) Siku Sumaye amehamia kwenu aliahidiwa nini?
(vi) walihamia watu wengi wakitoka ccm - Je, hawa mnawalipa kitu au vitu gani? VILE MSIVYOWALIPA WATU WANAOHAMIA KWENU NDIVYO CCM KISIVYOWALIPA CHOCHOTE WAHAMAJI

Kivutio CCM:
(i) Uwezo wa CCM kusimamia utekelezaji wa miradi yenye tija kwa wananchi,
(ii) Uwezo wa CCM kuchukia na kuchukuwa hatua dhidi ya matukio ya kifisadi,
(iii) uwezo wa CCM kurudisha heshima ya uwajibikaji wa taasisi zake,
(iv) Uwezo wa CCM kuwa na mkakati wa kukuza ajira kupitia viwanda na kilimo,
(v) Uwezo wa CCM kutoa elimu bure (chekechea - sekondari) nknk
 
Back
Top Bottom