CCM imechanganyikiwa?

CCM imechanganyikiwa?

Mimi binafsi naamini udhalimu huu Mungu hataufumbia macho milele, iko siku wenyewe kwa wenyewe wataanza kunyosheana vidole baada ya mambo kwenda tofauti na matarajio yao, wana wanunua watano au kumi, wenye akili zao timamu 100 au 200 wanaondoka kimyakimya, mmefanya nini! haya yana mwisho tu za watu kama mengine yaliyofikia mwisho. tununueni wote 6m hapo mtakuwa mmeweza.
 
Huu ni zaidi ya utoto na ulemavu wa kukosa tafakuri... Haya yanayoendelea nchini nikiri wazi kuwa pamoja na kwamba kuna matukio ya kutisha ya kuwashambulia wapinzani kwa silaha za moto na silaha nyingine zenye kujeruhi na kusababisha ulemavu....

Lakini hili la kutumia ushawishi wa ahadi za mali pesa vyeo na ulinzi kwenye bishana ili watu warejee ccm ni uhuni na michezo ya kitoto kabisa

Tusijaribu kuwaiga Rwanda.... Ukubwa wa ile nchi ni sawa na mkoa mmoja wa Tanzania... Tusiige zile siasa kuna kuna mvutano wa makabila mawili... Siasa za pale zinahusika sana na ukabila
Tumeshashuhudia yaliyotokea kwenye uchaguzi wa madiwani hivi karibuni, watu wameumizwa sana.. Watu wamejeruhiwa sana, watu wamebambikiwa kesi sana... Hii ni ishara gani kwenye uchaguzi 2020?(kama utakuwepo lakini) tofauti ya hoja ndio tuumizane kiasi hiki? Vyombo vyetu vya usalama na tume ya uchaguzi vimevaa miwani ya mbao

Kama hii haitoshi pamoja na kufanya yale yote kwenye uchaguzi ule sasa ni mwendo wa kununua wapinzani... Naamini kuna kundi kubwa sana ndani ya ccm wanashangazwa na haya lakini hawana pa kusemea.. Hawa wanaonunuliwa wanaenda kutupwa huko... Ni uchoyo na ulafi wa aina yake... Ni sawa na kuwa na makabati ya nguo lakini bado unataka na za jirani....

Hawa wanaonunuliwa hawaendi kuonyesha vipawa vyao huko, wanaenda kuminywa na kufichwa ili mradi tu kukomoa kaliba fulani ya watu...

Hivi kipaumbele ni kuua upinzani? Ingekuwa mashindano yako hivyo kusingekuwa na kushindana basi... Tunapoteza muda mwingi kwenye siasa za kipuuzi kabisa.. Mwisho wa siku morali wa kujenga taifa unashuka kabisa.... ccm halisi wanabaki na kinyongo, ccm makinikia wanakuwa na hofu na kutojiamini.... Mwendo mpya wa kuwindana kusimangana na kuchomeana unaaza.... Ni aina gani hii ya siasa mnafanya?

Mtanunua wangapi? Mtawabana wangapi ili waombe Po na kujiunga nanyi? Kumbukeni kuna kura million 6 +, tena hizi mmezitamka nyie... Uhalisia ni kwamba zipo zaidi ya hapo tena kwa mbali sana....

Tunawakemea kwa sauti ya uzalendo hamjengi bali mnabomoa, hamtengenezi bali mnaharibu.. Hamuunganishi bali mnatenaganisha.... Huu ni uwendawazimu na kukosa tafakuri... Hivi mmesahau kuwa WAKATI SI MILELE?!?!??
Hivi, hii dhana ya wapinzani kununuliwa (viongozi na wanachama wa upinzani na sio wa CCM) inatokana na ile video ya akina Lema na Nasari?
Na ni kwa nini mnataka watu waamini katika sinema (Kufikirika)? Manataka kutuaminisha kwamba kitendo cha watu kuhama kutoka chama kimoja cha siasa na kwenda kwenye chama kingine (tawala au pinzani) huwa wamenunuliwa? Je, mmeisha jua bei iliyoko mnadani (CCM na CHADEMA)?
Endeleeni kuweweseka na siku mkizinduka mtakuta mmeendelea kubaki wapinzani dhaifu!
Acheni kulalamika! Tafuteni dawa!
 
Tuache vyote ila tukiua vyama vya upinzani ni kuua uchumi ...maana watu watakua wanapiga tu bila hata woga maana hakuna wa kuwasema.
 
Kama kuna ushahidi wa ccm kuhusika ni kweli inapaswa kukemewa kwa nguvu zote, lkn wasi wasi wangu makamanda jahazi linatoboka baada ya kujadili nini tatizo mnakuja na visingizio lukuki. Wanachama wanakimbia eti oohh wanahongwa sababu nyepesi kweli kweli.

Kwa sasa mmekosa mtu kama slaa mnabaki kulia lia tu mitandaoni. Ukweli ni kuwa mmewaangusha wananchí hata kabla ya kupewa dola, mlichobakisha kwa sasa kila anaekuambieni ukweli eti ccm. Edo na wengine kadhaa wapo njiani nyie katafteni flash mseme wanahongwa.

Akina Zitto, Kitila, Mwigamba, Kafulila, Msando nk wote walihama enzi za Slaa. Sasa sijui unamaanisha nini kwamba watu wanahama kwakuwa Slaa hayupo. Ni hivi, sasa hivi ccm imeamua kununua wapinzani ili ijenge taswira inakubalika kitu ambacho sio kweli.
 
mshana jr

Tungepata waonyaji na wakemeaji wa huu uhuni ingependeza haiwezekani mtu mmoja apeleke nchi jinsi anavyotaka Hata Kama kakosea asikosolewe hii sio fair. Ila akumbuke atawadanganya Watu Wote ila sio Siku zote. Ajifunze Kwa Mugabe Ipo Siku udhalimu utafika mwisho. Kila mtu anaogopa yy ni Nani???

Tz haijawa kilaza Namna hii au ni kizazi cha zilipendwa haki yanane I wish I could be meja General.
Mungu tusaidie!!!
Huna rafiki ambaye ni Major General? Unamlinganisha Mugabe na Magufuli au ZANU PF na CCM? Vipi, kitumbua kimetiwa mchanga?
 
Kabla ya kufa na kuoza KANU ya Kenya ilinunua kila iliyemhofia akiwemo Raila Odinga huyu unayemfahamu , na akapewa UKATIBU MKUU wa KANU .

Kwahiyo haya yanayotendeka , ni njia ya ccm kufa kibudu .
 
Hivi ukiwa CCM ujinga unahusika? Upofu na uziwi je?!! Huoni kinacho endelea wala husikii...?!! Hata kuwaza kweli huwezi?! ....mkuu wa wilaya wakati ananunua watu Arumeru wewe ulikuwa wapi? uko dunia gn?!! .Naamini wapo CCM welevu hasa na IPO siku watapata pa kusemea.@Mshana
Hakuna ushahidi wa arumeru ni fununu tu na flash.
 
Akina Zitto, Kitila, Mwigamba, Kafulila, Msando nk wote walihama enzi za Slaa. Sasa sijui unamaanisha nini kwamba watu wanahama kwakuwa Slaa hayupo. Ni hivi, sasa hivi ccm imeamua kununua wapinzani ili ijenge taswira inakubalika kitu ambacho sio kweli.
Inawezekana wananunuliwa je hatua gani zinachukuliwa ili wasikubali kununuliwa? Je aina hii ya viongozi wanaonunulika kirahisi kuliko machangudoa wa kona bar inafaa kuongoza nchi yenye rasilimali nyingi kama hii?
 
Hata hapa kwetu kuna ma kabila makubwa mawili yaani ccm na chadema ukipenda mwangaluka na shimboni shafo. CCM hoyeeeee



Vyasaka msituletee upuuzi wenu.

Fanyeni mfanyavyo, ila msituchokoze na siasa zenu za kipuuzi.

Sisi ni wachapa kazi.

Majungu pelekeni kwenu, pumbavu kabisa
 
Huu ni zaidi ya utoto na ulemavu wa kukosa tafakuri... Haya yanayoendelea nchini nikiri wazi kuwa pamoja na kwamba kuna matukio ya kutisha ya kuwashambulia wapinzani kwa silaha za moto na silaha nyingine zenye kujeruhi na kusababisha ulemavu....

Lakini hili la kutumia ushawishi wa ahadi za mali pesa vyeo na ulinzi kwenye bishana ili watu warejee ccm ni uhuni na michezo ya kitoto kabisa

Tusijaribu kuwaiga Rwanda.... Ukubwa wa ile nchi ni sawa na mkoa mmoja wa Tanzania... Tusiige zile siasa kuna kuna mvutano wa makabila mawili... Siasa za pale zinahusika sana na ukabila
Tumeshashuhudia yaliyotokea kwenye uchaguzi wa madiwani hivi karibuni, watu wameumizwa sana.. Watu wamejeruhiwa sana, watu wamebambikiwa kesi sana... Hii ni ishara gani kwenye uchaguzi 2020?(kama utakuwepo lakini) tofauti ya hoja ndio tuumizane kiasi hiki? Vyombo vyetu vya usalama na tume ya uchaguzi vimevaa miwani ya mbao

Kama hii haitoshi pamoja na kufanya yale yote kwenye uchaguzi ule sasa ni mwendo wa kununua wapinzani... Naamini kuna kundi kubwa sana ndani ya ccm wanashangazwa na haya lakini hawana pa kusemea.. Hawa wanaonunuliwa wanaenda kutupwa huko... Ni uchoyo na ulafi wa aina yake... Ni sawa na kuwa na makabati ya nguo lakini bado unataka na za jirani....

Hawa wanaonunuliwa hawaendi kuonyesha vipawa vyao huko, wanaenda kuminywa na kufichwa ili mradi tu kukomoa kaliba fulani ya watu...

Hivi kipaumbele ni kuua upinzani? Ingekuwa mashindano yako hivyo kusingekuwa na kushindana basi... Tunapoteza muda mwingi kwenye siasa za kipuuzi kabisa.. Mwisho wa siku morali wa kujenga taifa unashuka kabisa.... ccm halisi wanabaki na kinyongo, ccm makinikia wanakuwa na hofu na kutojiamini.... Mwendo mpya wa kuwindana kusimangana na kuchomeana unaaza.... Ni aina gani hii ya siasa mnafanya?

Mtanunua wangapi? Mtawabana wangapi ili waombe Po na kujiunga nanyi? Kumbukeni kuna kura million 6 +, tena hizi mmezitamka nyie... Uhalisia ni kwamba zipo zaidi ya hapo tena kwa mbali sana....

Tunawakemea kwa sauti ya uzalendo hamjengi bali mnabomoa, hamtengenezi bali mnaharibu.. Hamuunganishi bali mnatenaganisha.... Huu ni uwendawazimu na kukosa tafakuri... Hivi mmesahau kuwa WAKATI SI MILELE?!?!??
Hii ni kadi ya mwaka mpya kwa magufail.
 
Ukiona unanunulika ujue upo biasharani hutufai!!
Ukiona unatishika ujue hujakomaa hutufai!!
Ukiona unalaghaika kwa namna yoyote ile ili kuidhohofisha kesho ya taifa hakika bora usingeingia kwenye siasa maana u msaliti ambae adhabu itakukumba tu uwe utawalani au mbadalani!!
 
Inawezekana wananunuliwa je hatua gani zinachukuliwa ili wasikubali kununuliwa? Je aina hii ya viongozi wanaonunulika kirahisi kuliko machangudoa wa kona bar inafaa kuongoza nchi yenye rasilimali nyingi kama hii?
Yaani mpaka leo hujui?
Huwezi kumlinda mtu.

Au hukuona jinsi ilivyotakiwa kuwa na minyororo mikubwa ili kuwadhibiti watu?
 
Ukiona unanunulika ujue upo biasharani hutufai!!
Ukiona unatishika ujue hujakomaa hutufai!!
Ukiona unalaghaika kwa namna yoyote ile ili kuidhohofisha kesho ya taifa hakika bora usingeingia kwenye siasa maana u msaliti ambae adhabu itakukumba tu uwe utawalani au mbadalani!!
Very well said
 
Mwenendo wetu kijamii, kisiasa kwa kweli unaacha maswali mengi kuliko majibu. Wale wahenga wenzangu watanielewa pale Mwalimu alivyotuambia kuwa ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, kati ya hayo uongozi bora ni mojawapo. Jinsi tunavyo endelea na maisha ya sasa naona viongozi wetu wamekuwa so impulsive na hawana vision kabisa. Tunachoona sasa hivi ni siasa za maji taka, maigizo na viongozi waliokuwa na unmanageable egos.
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la political prostitution ambapo viongozi waliochaguliwa na wananchi kwa kodi za wananchi wanadiriki kuwaambia wananchi hao hao waliowachagua kuwa wanamuunga mkono kiongozi fulani hivyo kujivua ubunge/udiwani. Dr. Martin Luther King Jr, aliwahi kusema hivi " We need leaders not in love with money but in love with Justice. Not in love with publicity but in love with humanity." Yardstick hii hapa kwetu hakuna wa kuitimiza na hivyo basi future ya taifa letu ni tete.
 
Inawezekana wananunuliwa je hatua gani zinachukuliwa ili wasikubali kununuliwa? Je aina hii ya viongozi wanaonunulika kirahisi kuliko machangudoa wa kona bar inafaa kuongoza nchi yenye rasilimali nyingi kama hii?

Inapokuja kwenye suala la pesa sioni mtu anayemudu kugomea kwenye jamii inayogubikwa na umasikini. Kwa maneno ya mtaani hakuna mkate mgumu mbele ya chai. Na bahati ccm ambayo ndio mnunuzi wanafahamu vyema kwamba penye udhia ni kupenyeza rupia.
 
Back
Top Bottom