CCM imechanganyikiwa?

CCM imechanganyikiwa?

Naomba wale wote wananchi ambao itikadi yetu ya upinzani ni IMANI au tunaopenda demokrasia tusife moyo na tusiwaamini hawa wanasiasa vigeugeu,yaan mtu anaongea mpaka unaemsikiliza unaona aibu
Upinzani unatakiwa kuwa na msimamo..sio kubadili gia na kula matapishi kila baada ya dk 5 vinginevyo hakuna kitu. Hii ya Lema, Mbowe na Lowassa iwe funzo tosha.
tapatalk_1516363879382.jpeg
tapatalk_1516023263813.jpeg
 
Huu ni zaidi ya utoto na ulemavu wa kukosa tafakuri... Haya yanayoendelea nchini nikiri wazi kuwa pamoja na kwamba kuna matukio ya kutisha ya kuwashambulia wapinzani kwa silaha za moto na silaha nyingine zenye kujeruhi na kusababisha ulemavu....

Lakini hili la kutumia ushawishi wa ahadi za mali pesa vyeo na ulinzi kwenye bishana ili watu warejee ccm ni uhuni na michezo ya kitoto kabisa

Tusijaribu kuwaiga Rwanda.... Ukubwa wa ile nchi ni sawa na mkoa mmoja wa Tanzania... Tusiige zile siasa kuna kuna mvutano wa makabila mawili... Siasa za pale zinahusika sana na ukabila
Tumeshashuhudia yaliyotokea kwenye uchaguzi wa madiwani hivi karibuni, watu wameumizwa sana.. Watu wamejeruhiwa sana, watu wamebambikiwa kesi sana... Hii ni ishara gani kwenye uchaguzi 2020?(kama utakuwepo lakini) tofauti ya hoja ndio tuumizane kiasi hiki? Vyombo vyetu vya usalama na tume ya uchaguzi vimevaa miwani ya mbao

Kama hii haitoshi pamoja na kufanya yale yote kwenye uchaguzi ule sasa ni mwendo wa kununua wapinzani... Naamini kuna kundi kubwa sana ndani ya ccm wanashangazwa na haya lakini hawana pa kusemea.. Hawa wanaonunuliwa wanaenda kutupwa huko... Ni uchoyo na ulafi wa aina yake... Ni sawa na kuwa na makabati ya nguo lakini bado unataka na za jirani....

Hawa wanaonunuliwa hawaendi kuonyesha vipawa vyao huko, wanaenda kuminywa na kufichwa ili mradi tu kukomoa kaliba fulani ya watu...

Hivi kipaumbele ni kuua upinzani? Ingekuwa mashindano yako hivyo kusingekuwa na kushindana basi... Tunapoteza muda mwingi kwenye siasa za kipuuzi kabisa.. Mwisho wa siku morali wa kujenga taifa unashuka kabisa.... ccm halisi wanabaki na kinyongo, ccm makinikia wanakuwa na hofu na kutojiamini.... Mwendo mpya wa kuwindana kusimangana na kuchomeana unaaza.... Ni aina gani hii ya siasa mnafanya?

Mtanunua wangapi? Mtawabana wangapi ili waombe Po na kujiunga nanyi? Kumbukeni kuna kura million 6 +, tena hizi mmezitamka nyie... Uhalisia ni kwamba zipo zaidi ya hapo tena kwa mbali sana....

Tunawakemea kwa sauti ya uzalendo hamjengi bali mnabomoa, hamtengenezi bali mnaharibu.. Hamuunganishi bali mnatenaganisha.... Huu ni uwendawazimu na kukosa tafakuri... Hivi mmesahau kuwa WAKATI SI MILELE?!?!??


CCM si chama , hilo ni genge la Mafia , haya uliyoyaandika ni kumpigia mbuzi gitaa
 
Kwa tahmini ya kisayansi pia ungejiuliza hao wanaonunuliwa ni wanachama wa aina gana na kwanini wanunuliwe kama kweli wameshiba itikadi ya vyama vyao? Kweli mtu anayeamini misingi ya chama chake anaweza kweli kununulika? Huwezi kuona tatizo upande mmoja tu na kuacha mwengine, otherwise, tathmini yako inakuwa haina maana sana zaidi ya kujaza server. Jaribu sana kwenye uandishi kubalance na sio lazima uonekane mnazi tu wa cham flani.

Ni wajinga pekee ambao wangeweza kununulika kwa thamani ya kuikana imani yake na itikadi wanazoziamini na kuzisimamia, wajinga kama hao siamini kama wangeweza kupatikana kwenye chama kinachojinathibisha kuwa ni "chama makini". Msihangaike kumtafuta mchawi bali mjitathimini wenyewe kwanza.

Sote tunaishi mitaani na tunayaona yanayoendelea kwa sasa, tunaingia kwenye vikao, tunasikiliza maoni ya wana mitaa wenzetu, Kuhusu kununulika kwa mazingira ya huku sijasikia, ila kuna uwezekano madiwani wengi wa Cdm 2020 eidha wakaacha kugombea ama wakagombea kupitia Ccm ingawa nalo ni gumu. Ukiondoa vita dhidi ya ufisadi, umeiondoa Cdm kwenye ramani, kosa lilianzia hapo tu.
 
Time will tell brother!... Let's just wait an see!

Ila kwa sasa mnaweweseka kutafuta mchawi wakati DJ anawasokota taratibu.
The one you classify him as DJ is far better a hundred thousand times than you and your whole clan... And I stand to be correct
 
Back
Top Bottom