CCM hawajiheshimu

CCM hawajiheshimu

Kitendo cha kuwa na wanasiasa wanaoiongoza Serikali lakini kiongozi wa chama cha siasa kinachoiongoza hiyo serikali kuanza kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali, ni dalili kwamba chama kilichoko madarakani hakijiheshimu.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapotoa fursa kwa chama Kilichoko madarakani kuisimamia serikali nje ya mfumo rasmi. Mambo ya Viongozi wa CCM kujifanya wanaikagua serikali kama inatekeleza mambo yao, ni uvunjivu wa Katiba na ishara kwamba CCM haijiheshimu.

Ziara za Kinana ni kama zinaonesha kwamba Msimamizi Mkuu wa Serikali kashindwa kuisimamia serikali hivyo Kinana sasa anafanya kazi hiyo. Kinana anatoa maagizo kwa serikali kwa mamlaka gani aliyo nayo?

Kama CCM ingekuwa inajiheshimu ingemzuia Kinana kufanya anachofanya kwani kinaidhalilisha serikali wanayoiongoza na kitendo hicho pia kinaonesha Msimamizi wake Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania anayetokana na chama chao, hatimizi majukumu yake ipasavyo.
Hivi nchi hii ina Rais au tumetundika picha ya mtu ambaye anapaswa kufanya kazi za Urais wakati nchi inateketea!
 
Umesahau jambo moja, johnthebaptist sio kuwa anasubiri muda wa kula tuu bali na wa kujisaidia pia.
Huyo ni ile mizigo kwa taifai

Umesahau jambo moja, johnthebaptist sio kuwa anasubiri muda wa kula tuu bali na wa kujisaidia pia.
Huyo ni ile mizigo kwa taifa
Mzigo wa Taifa ni Mbowe anayelambishwa asali kwenye Maridhiano

Kazi ya Maridhiano ni ya Kikosi Kazi cha Prof Mkandala na Zitto Kabwe wa ACT wazalendo
 
Mzigo wa Taifa ni Mbowe anayelambishwa asali kwenye Maridhiano

Kazi ya Maridhiano ni ya Kikosi Kazi cha Prof Mkandala na Zitto Kabwe wa ACT wazalendo
Ila kwa miaka 73 uliyo nayo na bado unatumia "Smartphone" wewe mkali. Wenzako "Whiskies" zilishawamaliza.
 
Ngoja chadema na wananchi tuanze mikutano ya hadhara hakuna wa kuzuia Sasa maana ni KWa mjibu wa katiba, itafanyika , tumekua wapumbavu Yani ccm ifanye mikutano kana kwamba nchi ya kwao wengine hakuna, panueni Magereza ,shame on you
CHADEMA ioneshe Kwa vitendo ujasiri wa kufanya mikutano iliyoruhusiwa kikatiba.
 
Ili nini kitokee? Wewe unaona sawa mikutano kuzuiwa kinyume cha Katiba?
Namaanisha wasiogope KIVULI. Mikutano ni halali, wafanye, maana hata KIBALI hakipo kikatiba.

Ni kuwaarifu tu POLISI basi na Si kuomba KIBALI.
 
Namaanisha wasiogope KIVULI. Mikutano ni halali, wafanye, maana hata KIBALI hakipo kikatiba.

Ni kuwaarifu tu POLISI basi na Si kuomba KIBALI.
Kama kungekuwa na Jeshi la Polisi linaloheshimu sheria na mahakama inayolinda haki za watanzania, hilo lingewezekana.
 
Ili ujue chama kimechokwa hapa Bukoba ziara yake ilipokelewa na vijana wa skauti,hakuna mtu mzima aliyesumbuka na ziara hiyo mbali na chawa wao wa CCM

Na wanatumia nguvu kubwa kutaka kuonyesha wanakubalika, ila wanajua ukweli ni kuwa CCM haikubaliki. Hii ndio sababu mkakati wao namba moja ni kuhakikisha CDM inakufa, kwani wanaamini ndio imewapoteza kwenye siasa za ushindani.
 
Umecheka kwa sababu hujaelewa. Pole!
Hapana... kaelewa SANA ila kawakumbuka wenzie waliotangulia mbele ya haki. Hawa "Wastaafu" wanaokula hela zetu za kodi mpaka wafe, huwa wanakunywa sana "Whisky". Huyu pamoja na "kumwagilia moyo" huwa anatumia "Smartphone" yake kupotosha mawazo ya vijana.
 
Ukishangaa ya Kinana Basi hujasikia ya kiongozi wa mbio za mwenge anavyotoa amrii. kila mkoa
 
Bora huyo Kinana aendelee hivyohivyo ana faida kuliko viongozi wa serikali, na siku akitamka tozo zinaumiza wananchi utaona zitafuta haraka.

Nchi hii anayemzidi cheo Kinana ni Rais tu.
Katiba inamruhusu au unaongea tu? Shida tumezoea kufanya mambo yetu kiholela holela,hata kufikiri kwetu ni kwa kiholela.
 
Back
Top Bottom