Muwe mnaelewa ndugu zangu vitu vyepesi na Rahisi Kama hivi, CCM ndio iliyounda serikali baada ya kuchaguliwa na watanzania, CCM ndio iliyoomba kura kutoka kwa wananchi, CCM haikuundwa na serikali Bali CCM ndio iliyounda serikali iliyopo madarakani, CCM ndio itakayokwenda kwa wananchi kuwaeleza imefanya Nini na imetekeleza Nini kulingana na ilivyoahidi katika uchaguzi uliopita
CCM ndio itakayopita majukwaani na mitaani Tena kuomba kura na Ridhaa ya wananchi, Sasa kwanini isikague utekelezaji wa ilani yake? Kwanini usiende kusikiliza kero za wananchi? Kwanini isiwasemee wananchi walioichagua na kuiweka madarakani? Unataka Nani afanye kazi hiyo? Unataka ikae tu ofisini? Unataka ikaseme Nini uchaguzi ujao Kama isipojuwa kinachoendelea na kufanywa na serikali yake?
CCM ndio iliyoingia mkataba na wananchi wa kuwatumikia kwa nguvu zake zote, Sasa kwanini isifuatilie utekelezaji wa mkataba wake wa kiutumishi? Unataka ivunje mkataba huo halafu one inyimwe kura Kama adhabu?
Tuiache CCM ifanye kazi yake na nyinyi subilini uchaguzi ujao mtawaeleza hayo wananchi ili muone Kama watawaelewa maana watanzania wa leo siyo wajinga na hawawezi kumpa mtu uongozi anayekaa ofsini muda wote