CCM hawajiheshimu

CCM hawajiheshimu

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,226
Reaction score
48,672
Kitendo cha kuwa na wanasiasa wanaoiongoza Serikali lakini kiongozi wa chama cha siasa kinachoiongoza hiyo serikali kuanza kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali, ni dalili kwamba chama kilichoko madarakani hakijiheshimu.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapotoa fursa kwa chama Kilichoko madarakani kuisimamia serikali nje ya mfumo rasmi. Mambo ya Viongozi wa CCM kujifanya wanaikagua serikali kama inatekeleza mambo yao, ni uvunjivu wa Katiba na ishara kwamba CCM haijiheshimu.

Ziara za Kinana ni kama zinaonesha kwamba Msimamizi Mkuu wa Serikali kashindwa kuisimamia serikali hivyo Kinana sasa anafanya kazi hiyo. Kinana anatoa maagizo kwa serikali kwa mamlaka gani aliyo nayo?

Kama CCM ingekuwa inajiheshimu ingemzuia Kinana kufanya anachofanya kwani kinaidhalilisha serikali wanayoiongoza na kitendo hicho pia kinaonesha Msimamizi wake Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania anayetokana na chama chao, hatimizi majukumu yake ipasavyo.
 
Bora huyo Kinana aendelee hivyohivyo ana faida kuliko viongozi wa serikali, na siku akitamka tozo zinaumiza wananchi utaona zitafuta haraka.

Nchi hii anayemzidi cheo Kinana ni Rais tu.
Kwani wanaotekeleza maagizo ya Kinana si wako chini ya Rais? Ni kama Kinana anapoka madaraka ya Rais.
 
Kitendo cha kuwa na wanasiasa wanayoiongoza Serikali lakini kiongozi wa chama cha siasa kinachoiongoza hiyo serikali kuanza kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali, ni dalili kwamba chama kilichoko madarakani hakijiheshimu...
Hata hapo kwenu mkuu,kuna kipindi madiwani walijianzishia ziara kutembelea miradi bila mawasiliano na Mkurugenzi wa manispaa.

Mkurugenzi aliwapiga spana za kwenye makomwe yao wakatulia.Hii inaonesha ni kwa kiwango kipi bado miongozo na taratibu za uongozi na utendaji ambavyo hauleweki kwa baadhi yao.

Wanahitaji kupewa elimu.Ukikutana na mtekelezaji/mtendaji jeuri anakuaibisha jua la saa sita.
 
Serikali inatekeleza Ilani ya CCM so ni lazima Komredi Kinana awakague.

Angeenda Tundu Lisu ndio tungemuona ana kiherehere.
 
Kitendo cha kuwa na wanasiasa wanayoiongoza Serikali lakini kiongozi wa chama cha siasa kinachoiongoza hiyo serikali kuanza kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali, ni dalili kwamba chama kilichoko madarakani hakijiheshimu.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapotoa fursa kwa chama Kilichoko madarakani kuisimamia serikali nje ya mfumo rasmi. Mambo ya Viongozi wa CCM kujifanya wanaikagua serikali kama inatekeleza mambo yao, ni uvunjivu wa Katiba na ishara kwamba CCM haijiheshimu.

Ziara za Kinana ni kama zinaonesha kwamba Msimamizi Mkuu wa Serikali kashindwa kuisimamia serikali hivyo Kinana sasa anafanya kazi hiyo. Kinana anatoa maagizo kwa serikali kwa mamlaka gani aliyo nayo?

Kama CCM ingekuwa inajiheshimu ingemzuia Kinana kufanya anachofanya kwani kinaidhalilisha serikali wanayoiongoza na kitendo hicho pia kinaonesha Msimamizi wake Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania anayetokana na chama chao, hatimizi majukumu yake ipasavyo.
Ili ujue chama kimechokwa hapa Bukoba ziara yake ilipokelewa na vijana wa skauti,hakuna mtu mzima aliyesumbuka na ziara hiyo mbali na chawa wao wa CCM.
 
Kitendo cha kuwa na wanasiasa wanayoiongoza Serikali lakini kiongozi wa chama cha siasa kinachoiongoza hiyo serikali kuanza kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali, ni dalili kwamba chama kilichoko madarakani hakijiheshimu.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapotoa fursa kwa chama Kilichoko madarakani kuisimamia serikali nje ya mfumo rasmi. Mambo ya Viongozi wa CCM kujifanya wanaikagua serikali kama inatekeleza mambo yao, ni uvunjivu wa Katiba na ishara kwamba CCM haijiheshimu.

Ziara za Kinana ni kama zinaonesha kwamba Msimamizi Mkuu wa Serikali kashindwa kuisimamia serikali hivyo Kinana sasa anafanya kazi hiyo. Kinana anatoa maagizo kwa serikali kwa mamlaka gani aliyo nayo?

Kama CCM ingekuwa inajiheshimu ingemzuia Kinana kufanya anachofanya kwani kinaidhalilisha serikali wanayoiongoza na kitendo hicho pia kinaonesha Msimamizi wake Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania anayetokana na chama chao, hatimizi majukumu yake ipasavyo.
Kwa Tanzania, chama ni msimamizi wa serikali- maana ndio kilichowaweka hao madarakani. Lakioni bora hata Chama kinasema, hao tuliowchagua kama wawakilishi wetu (Bunge) ambao ndio wanaotakiwa kuisimamia serikali, pumba hovyo kabisa.
 
Ngoja chadema na wananchi tuanze mikutano ya hadhara hakuna wa kuzuia Sasa maana ni KWa mjibu wa katiba, itafanyika , tumekua wapumbavu Yani ccm ifanye mikutano kana kwamba nchi ya kwao wengine hakuna, panueni Magereza ,shame on you
Kiufupi Ziara ya kinana inaonesha jinsi CCM isivyowaamini na kuwaheshimu waliowapa kazi ya kuongoza serikali yetu.
 
Kwa Tanzania, chama ni msimamizi wa serikali- maana ndio kilichowaweka hao madarakani. Lakioni bora hata Chama kinasema, hao tuliowchagua kama wawakilishi wetu (Bunge) ambao ndio wanaotakiwa kuisimamia serikali, pumba hovyo kabisa,
Kimfumo kuna huo utaratibu wa chama kuisimamia serikali. Hapa ni kwamba CCM inafanyakazi za serikali.
 
Kimfumo kuna huo utaratibu wa chama kuisimamia serikali. Hapa ni kwamba CCM inafanyakazi za serikali.
Mkuu Allen,

Kinana amaesema viongozi wa Chama wawe qwakali kwa watendaji - hilo ni chagizo kwamba hebu msikae kimya tuu kwa mambo yanavyofanywa na watendaji serikalini. Again mkuu, kwa hali ilivyo Tz hapa acha wamsaidie Bi Mkubwa.
 
Back
Top Bottom