Elimu bure Tanzania ya sasa HAIWEZEKANI na wala HAIPO, wanasiasa wanadanganya tu kwa ajili ya kuwa ghilibu Watanzania.
Ni ujinga na undezi wa hali ya juu kuita ní elimu bure eti kwa kuwa ule mchango wa Tsh 20,000 umeondolewa.
Wakati wa JK Nyerere ndiyo kulikuwa na elimu bure ambapo ilihusisha ada za Shule, madaftari na peni, vitabu, nauli. Kwa vyu vikuu ilihusisha pia posho ya mwezi na chakula cha canteen.
Wazazi wetu walikuwa wanawajibika kutupeleka shule na kutupatia mavazi tu. Mengine yote ilikuwa ni jukumu la serikali.
HII ya Magufuli ni maumigizo tu
Nakumbuka shule za msingi kulikuwa na maktaba, kulikuwa na vitabu vya masomo yote na kwa idadi ya wanafunzi mliopo darasani.
Monitors wanikuwa wanaangalia ratiba kujua SoMo linaanza au linafuata.
Anaenda chukua vitabu vya SoMo husika anagawa kwa Kila mwanagunzi.
Daftari likiisha unapelekwa kwa mwalimu was Somo hilo,anasaini unapeleka kwa mwalimu anayehusika na store anakupatia jipya.
Kila mwaka wanafunzi mnapelekwa bohari kubeba vifaa vya kufundishia na maftari
Saa nne mnapata bluga la nguvu.
Ukiingia sekondari unasafiri kwa warrant ya serikali. SHAAABASH HUYO NDIYE JULIAS
Mwalimu Julius alifanikiwa kupambana na adui
Ikumbukwe wakati kulikuwa na magonjwa ya mlipuko, surua, ndui na ukoma.
Surua na ndui ziliua sana has a watoto.
Mwalimu alileta chanjo mashuleni, wakati huo vituo vya afya havikuwepo hivyo hats siyo wanafunzi walienda kupatia chanjo hapo.
Ikumbukwe pia wakati huo raslimali za taifa hazikutumika Kama ilivyo Sasa.
Madini tulikuwa na mgodi was Almad tu Mwadui,
Utalii ulikuwa mdogo Sana, hatukuwa na wawekezaji Kama sasa
Hatukuwa na uvuvi wa kimataifa au mkubwa Kama Leo hii
Uvuvi ulifanywa na serikali TACOSHIRI.
Tulitegemea Kodi za kichwa na kilimo Cha mazao ya biashara.
1. Mikoa ya pamba(usipokuwa na shamba la pamba mahakamani) mnunuzi serikali
2. Mkonge,( mkulima serikali)
3.chai(mnunuzi serikali)
4. Kahawa( mnunuzi serikali)nk
NATIONAL MILLING,
Lilikuwa shirika la serikali lilisaidia kununua mahindi ya wakulima
GAPEX,
Shirika la serikali la kuuza mazao nje ya nchi.
1. Ufuta
2. Mtama
3. Korosho
4 . Mazao yote yatokanayo na misitu ikiwemo asali
Serikali ilikuwa na pesa za kuendesha Mambo yake.
Nyakati hizi zinapesa kuliko wakati ule,CCM MNAKWAMA WAPI,?