Barua ya wazi kwa Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Mkenda na wasaidizi wako

Annie X6

JF-Expert Member
Mar 16, 2023
405
750
Mimi si mtumishi wala kufanyakazi yoyote katika sekta ya elimu. Mimi ni mdau na mzazi.

Mh waziri. Kila mtu atasema anavyotaka kwa kuwa nchi yetu ina uhuru wa kujielezea ili mradi hakuna sheria inayokiukwa.

Mh. Katika sekta hii ya elimu siasa inatumika na haiepukiki. Lakini ni lazima tujiminye tuweke siasa pembeni.

Nipo kwenye magroup kadhaa na nilishuhudia mzazi mwenzangu aliyekuandikia hoja zake ndeeeefu nafikiri hata sikuzisoma nikamaliza maana niligundua mzazi mwenzangu alikerwa sana na tabia iliyojitokeza shuleni hasa shule za Dar es Salaam na mikoa jirani walimu kutoza michango ya mitihani nakadhalika.

Nataka niweke sawa hapa. Mh waziri nakumbuka baada ya fidia ya ada kuanza ilipigwa marufuku michango. Hili lilitekelezwa vizuri tu.

Lakini uhalisia sio kama serikali yetu ilivyokusudia. Ilifikia hatua walimu walikataa kufundisha muda wa ziada ambao uliambatana na kamchango walikojitolea wazaz kummotisha mwalimu anayebaki na watoto muda wa ziada. Nina mifano ingawa sitataja hapa shule zikizokataa michango hiyo kwa kuwa sheria ilishaakataza. Wazaz waliwapigia magoti walimu wawasaidie na wangebeba jukumu la kujibu kama walimu wangeingizwa hatiani. Walim wale wanajua taratibu hawakukubali.

Nirejee kwa wazaz wanaoshirikiana kulinga juhudi za walimu kuwasaidia wanafunzi wakidai walimu wanakula pesa zao.

Hapa Tuweke siasa pembeni. Watoto wetu hawapati msaada wowte serikali mnapopiga msumari wa kukemea wazaz wasishiriki moja kwa moja kuwasupport walimu kusaidia watoto.

Ukweli upo hivi ni Sisi sisi wazaz hata viatu vya watoto wetu hatununui watoto wanakwenda na nguo chakavu. Na sio kwamba hatua pesa...no tunalipa vikoba na sherehe. Nataka nikumbushe jambo ambalo watumishi wa umma ni Royal sana. Wanatii sheria japo hali inakuwa mbaya. Hawataki kukaidi maagizo lakini huku ambako watoto wetu sisi maskini wapo hali ni mbaya sana. Wazaz wenzangu hawajui watoto wa viongozi hawasomi huku. Asilimia 90 walimu watoto wao wanasomeshwa English Medium...tuoneeni huruma

Hawa watoto wetu tunawapa Tsh1000 2000 3000 wengine hata 5000 ili mtoto awe flexible njiani anunue na awe na amani. Jambo ambalo ni kosa kubwa kuzoesha pesa watoto wetu. Watoto wanajaa kwa wauza mihogo wauza barafu nakadhalika hii sio manner

Mh Waziri wa Elimu.
Nashuhudia watoto alfajiri wakijaa kwa wauza mihogo wakinunua na kula njiani. Hizi ni pesa walizosamehewa wazazi ada na hawalipii chakula shuleni. Huu ndio ukweli...mashuhuda ni wengi njiani na barabarani wanaona.

Mh waziri. Ninashuhudia kwenye vikao vya wazazi takwimu za uchangiaji chakula umeshindikana wazazi tumekaidi kulipia chakula tena tulikubaliana wazaz wenyewe lakini wazazi tumegoma. Angalia takwimu. Si unazo mezazi kwako? Jionee mwenyewe wangapi wanachangia japo.mlo mmoja sh 1000 shuleni. Mtoto kupewa pesa ni kosa kubwa kumzoesha mtoto pesa jambo ambalo wazaz wenzangu hawalielewi kuwa tutakuja kuwa na watoto watakaoishia kwenye gambling station.
Kubeti.

Hapa tunaikaanga Tanzania yetu.

Ushauri.

-Fidia ya ada iendelee
  • michango iwekewe limit ila iwekwe kwenye joining instructions na mchango wa chakula uwepo
  • mchango wa dawati uwepo
-Mchango wa kuchangia taaluma uwepo

Mwisho
 
Hapo unakuta halimhusu waziri wa elimu limhusu waziri wa TAMISEMI. Hapana chezea nchi hii nifulu mkanganyiko.
 
Hawa watoto wetu tunawapa Tsh1000 2000 3000 wengine hata 5000 ili mtoto awe flexible njiani anunue na awe na amani. Jambo ambalo ni kosa kubwa kuzoesha pesa watoto wetu. Watoto wanajaa kwa wauza mihogo wauza barafu nakadhalika hii sio manner

Mh Waziri wa Elimu.
Nashuhudia watoto alfajiri wakijaa kwa wauza mihogo wakinunua na kula njiani. Hizi ni pesa walizosamehewa wazazi ada na hawalipii chakula shuleni. Huu ndio ukweli...mashuhuda ni wengi njiani na barabarani wanaona.
Huwa nina mashaka sana na usalama wa chakula hicho cha barabarani, huenda asilimia kubwa ya maradhi mbalimbali husababishwa na ubora hafifu wa chakula vya barabarani
 
Pole mzazi, So hayo mabilioni tunayopewa na World Bank na IMF yanaishia mifukoni mwa wakurugenzi na Kuchimba mashimo mawili matatu ya vyoo?? miaka 60+ ya uhuru tunashindwa hata kuwa na uhakika wa madawati shuleni???!! Hizi ndio habari ambazo zinanifanya nisiamini kama kuna moto huko mbinguni.
 
Mimi si mtumishi wala kufanyakazi yoyote katika sekta ya elimu. Mimi ni mdau na mzazi.

Mh waziri. Kila mtu atasema anavyotaka kwa kuwa nchi yetu ina uhuru wa kujielezea ili mradi hakuna sheria inayokiukwa.

Mh. Katika sekta hii ya elimu siasa inatumika na haiepukiki. Lakini ni lazima tujiminye tuweke siasa pembeni.

Nipo kwenye magroup kadhaa na nilishuhudia mzazi mwenzangu aliyekuandikia hoja zake ndeeeefu nafikiri hata sikuzisoma nikamaliza maana niligundua mzazi mwenzangu alikerwa sana na tabia iliyojitokeza shuleni hasa shule za Dar es Salaam na mikoa jirani walimu kutoza michango ya mitihani nakadhalika.

Nataka niweke sawa hapa. Mh waziri nakumbuka baada ya fidia ya ada kuanza ilipigwa marufuku michango. Hili lilitekelezwa vizuri tu.

Lakini uhalisia sio kama serikali yetu ilivyokusudia. Ilifikia hatua walimu walikataa kufundisha muda wa ziada ambao uliambatana na kamchango walikojitolea wazaz kummotisha mwalimu anayebaki na watoto muda wa ziada. Nina mifano ingawa sitataja hapa shule zikizokataa michango hiyo kwa kuwa sheria ilishaakataza. Wazaz waliwapigia magoti walimu wawasaidie na wangebeba jukumu la kujibu kama walimu wangeingizwa hatiani. Walim wale wanajua taratibu hawakukubali.

Nirejee kwa wazaz wanaoshirikiana kulinga juhudi za walimu kuwasaidia wanafunzi wakidai walimu wanakula pesa zao.

Hapa Tuweke siasa pembeni. Watoto wetu hawapati msaada wowte serikali mnapopiga msumari wa kukemea wazaz wasishiriki moja kwa moja kuwasupport walimu kusaidia watoto.

Ukweli upo hivi ni Sisi sisi wazaz hata viatu vya watoto wetu hatununui watoto wanakwenda na nguo chakavu. Na sio kwamba hatua pesa...no tunalipa vikoba na sherehe. Nataka nikumbushe jambo ambalo watumishi wa umma ni Royal sana. Wanatii sheria japo hali inakuwa mbaya. Hawataki kukaidi maagizo lakini huku ambako watoto wetu sisi maskini wapo hali ni mbaya sana. Wazaz wenzangu hawajui watoto wa viongozi hawasomi huku. Asilimia 90 walimu watoto wao wanasomeshwa English Medium...tuoneeni huruma

Hawa watoto wetu tunawapa Tsh1000 2000 3000 wengine hata 5000 ili mtoto awe flexible njiani anunue na awe na amani. Jambo ambalo ni kosa kubwa kuzoesha pesa watoto wetu. Watoto wanajaa kwa wauza mihogo wauza barafu nakadhalika hii sio manner

Mh Waziri wa Elimu.
Nashuhudia watoto alfajiri wakijaa kwa wauza mihogo wakinunua na kula njiani. Hizi ni pesa walizosamehewa wazazi ada na hawalipii chakula shuleni. Huu ndio ukweli...mashuhuda ni wengi njiani na barabarani wanaona.

Mh waziri. Ninashuhudia kwenye vikao vya wazazi takwimu za uchangiaji chakula umeshindikana wazazi tumekaidi kulipia chakula tena tulikubaliana wazaz wenyewe lakini wazazi tumegoma. Angalia takwimu. Si unazo mezazi kwako? Jionee mwenyewe wangapi wanachangia japo.mlo mmoja sh 1000 shuleni. Mtoto kupewa pesa ni kosa kubwa kumzoesha mtoto pesa jambo ambalo wazaz wenzangu hawalielewi kuwa tutakuja kuwa na watoto watakaoishia kwenye gambling station.
Kubeti.

Hapa tunaikaanga Tanzania yetu.

Ushauri.

-Fidia ya ada iendelee
  • michango iwekewe limit ila iwekwe kwenye joining instructions na mchango wa chakula uwepo
  • mchango wa dawati uwepo
-Mchango wa kuchangia taaluma uwepo

Mwisho
Unampigia ngoma mdundiko kiziwi
 
Back
Top Bottom