CCM damu yangu! Ikifa na mimi Nakufa..

CCM damu yangu! Ikifa na mimi Nakufa..

Habari!
Binafsi hili vuguvugu la kuiponda ccm na kuiona haifai linaniumiza sana,
Nimezoea kula bure (kula kwa kupitia deals).
Nasafiri bure (nadhani hapa ni kwa kodi za walala hoi).

Chochote nitakacho napata kwa sababu CCM ipo madarakani, rafiki zangu kibao wamepata ajira kubwa kubwa regardles ujuzi wao mdogo na elimu yakuunga unga walionayo,(wawili wapo bandari, wanne wapo maliasili) just because ccm ndiyo wameshikilia dola.
Nina magari zaidi ya mawili, i got them kwa sababu tu ccm iko madarakani.

Ninavyosikia juu ya kufa kwa CCM naweweseka sana jamani.
Ila ninaamini CCM wakishindwa 2015.

Tupo wengi sana tutakao kuwa maskini, si mimi peke yangu.
Machale yananicheza sana.

Akina riz washajiwekewa njia m'badala yakujinasua endapo chama hakitaingia madarakani 2015.
Tunapambana kwa kila njia kwa maslai yetu, umaskini si mzuri jamani!

Maisha yakupanda bodaboda na kugombania daladala ni magumu jamani.

Nitafurahi ccm isipokufa niendelee kuishi kwa ubwerere.
Hata wenzangu nao watafurahi..

Kura yako unaipiga wapi 2015 au we ni banyamulenge haupigi kura?
 
Kura yako unaipiga wapi 2015 au we ni banyamulenge haupigi kura?

i suppose to defend my interest aisee
kwa nguvu zote..

unaniulizaje kuhusu kura yangu?
read my heading above
 
CCM haina watu kama wewe, upo peke yako
 
Kwani chama kikishindwa uchaguzi ndio kinakufa?

Chama cha Mapinduzi hakipo kingekuwepo madarakani hata CDM isingekubalika...kilichopo ni Dola iliyojivika nguo za Kijani na kujiita CCM na kuachukua yale yote ya CCM na kuyaita yakwake, ndio maana leo polisi wanaishi km miungu watu, uhamiaji wanaweza wakakuita wewe ni raia wa Chile na ikakubalika, Mahakama inaweza ikakuhukumu hata km jina la mtuhumiwa si lako, Waziri mkuu anaweza akaamrisha wananchi wake wauawe bila woga eti amechoka (sijui kwanini asijiuzulu wenye nguvu waendelee), rais anaweza akajenga hoja kuwa safari ndio msingi wa maendeleo ya nchi na ikakubalika, Mawaziri wana gawana wapi pa kuchukulia hela na kushindana na kajenga nini au kanunua gari gani, wanachama wa CCM ndio wananchi halali wa taifa hili wengine woote risasi ni halali yao....!
 
je umekubali kuwa msukule wa CCM hadi kifo kiwatenganishe?
 
lakini umeongea uhalisia wako,
Kifo cha CCM ni kifo cha wengi,msiba mkubwa sana
 
lakini umeongea uhalisia wako,
Kifo cha CCM ni kifo cha wengi,msiba mkubwa sana

Ila kina Nape wanatumia power sana kujikweza na kujiandaa kwa maisha baada ya kifo cha CCM
Tutalia wengi
 
Chama cha Mapinduzi hakipo kingekuwepo madarakani hata CDM isingekubalika...kilichopo ni Dola iliyojivika nguo za Kijani na kujiita CCM na kuachukua yale yote ya CCM na kuyaita yakwake, ndio maana leo polisi wanaishi km miungu watu, uhamiaji wanaweza wakakuita wewe ni raia wa Chile na ikakubalika, Mahakama inaweza ikakuhukumu hata km jina la mtuhumiwa si lako, Waziri mkuu anaweza akaamrisha wananchi wake wauawe bila woga eti amechoka (sijui kwanini asijiuzulu wenye nguvu waendelee), rais anaweza akajenga hoja kuwa safari ndio msingi wa maendeleo ya nchi na ikakubalika, Mawaziri wana gawana wapi pa kuchukulia hela na kushindana na kajenga nini au kanunua gari gani, wanachama wa CCM ndio wananchi halali wa taifa hili wengine woote risasi ni halali yao....!

hapo kwenye red siyo ukweli
 
Back
Top Bottom