CCM and UDASA, this is shameful

CCM and UDASA, this is shameful

Ccm inaharibu nchi.Mpango upo pia kwa waandishi wa habari. Sikilizeni kesho headline

Kama hii nchi imefikia mahali chama tawala kinavitumia vyuo vikuu kama toilet pepar basi hakika anguko letu kama taifa kwenye elimu ni kubwa kuliko tafiti zinazotolewa na wanataaluma wenyewe.
 
Binafsi sijaona sababu ya mhitimisha mad(mccm) kuwalaumu wanafunzi kuwa ndio wamemzomea na kuondoka wakati wanafunzi wako likizo chuo kimefungwa.

Pamoja na mapungufu lkn mjadala ulijaa hoja nzito sana.utaona tofauti ya wasomi na wale wazee waliofukuzwa.
 
mimi nilishtuka nilipoona nyuso za watu na akinamama waliokuwa wamevaa kanga nikasema hawa wamekodishwa toka Manzese. Zaidi ya yote Lukuvi akapewa nafasi ya kufunga mdahalo!!!. Hivi kweli UDASA walijipanga?.
Hao kina mama ndiyo waliompa kula John Mnyika unamtafutia matatizo Mnyika siku akiende kuomba kula Manzese.
 
Last edited by a moderator:
Signature yangu;

Kiingereza: Its funny how sometimes the very people you'd take a bullet for, are the ones behind the trigger!
Kiswahili: Inachekesha kwa uchungu unapokuta watu ambao ungeweza kujitolea kula risasi kwa ajili yao, ndio hao hao wako tayari kukufyatulia risasi!
 
Aliye waita Interahamwe hakukosea. Tusubili tu 2015, tutaona zaidi ya haya.
 
Walifikiri watamleta Mh. Lissu ili akishatoa hoja zake basi waje wazicrush lakini Mh. Lukuvi kaishia kwenye hitimisho la kihistoria la kumkubali Lissu na uwezo wake mkuu kiasi hata waliokuwa hawamjui ni nani leo wamepata mwanga.
 
Jamani mbona sometime kilichoongelewa kilikuwa wazi? mie nadhani tujadili contents. Hivi kuandaa UDASA, UKAWA, CCM< au hata CHAMA CHA MADREVA kinahusiana vipi na kujenga hoja. Kwani Ukumbini walikuwa waingia kwa ID, mbona Rwaitama alikuwepo?
 
Hao kina mama ndiyo waliompa kula John Mnyika unamtafutia matatizo Mnyika siku akiende kuomba kula Manzese.

hivi Mnyika alipata kura zote Manzese?wasiopiga kura hawakuwepo?waliopiga kura 2010 ni wale wale tu wanaoishi huko,hakuna waliohamia?
 
Last edited by a moderator:
Mohamedi Mtoi

Ulitaraji nini kamanda? Kwani kiongozi/viongozi wa UDASA ni akina nani?

Anyway, binafsi naona midahalo hii inaibua hisia na kuwashirikisha wananchi wengi zaidi. Maswali ya msingi yanayobakia ni: Je, wasemaji kwenye mijadala hii wanachangia hoja zao kwa uhuru binafsi wa kuchangia ama wanasukumwa na kundi/vikundi fulani? Na msukumo wa hoja zao ni maslahi binafsi ama ya vikundi vyao ama maslahi ya Taifa?

Napenda mijadala hii iendelee, pengine itaamsha sauti zilizochagua kutosikika kwa sasa.
 
nimeshangaa sana LISSU kuzomewa, wale vijana ni wakina nani..?

Mkuu ni matumbo tu ndio yanawasumbua.Utakuta vijana kama hawa wakishamzomea mtu anayesema ukweli wakirudi vyumbani mwao WANAANZA KULIA KWA SABABU NAFSI ZINAANZA KUWASUTA.
 
Signature yangu;

Kiingereza: Its funny how sometimes the very people you'd take a bullet for, are the ones behind the trigger!
Kiswahili: Inachekesha kwa uchungu unapokuta watu ambao ungeweza kujitolea kula risasi kwa ajili yao, ndio hao hao wako tayari kukufyatulia risasi!
Signature yangu;
 
yyan ccm ni kichaka cha wahuni na wazindiki,, alafu yanatoka kama mazuzu vile,, majinga hata kudanganya hayajui pumbuvvuuuuuu ,,,,,,,

Yaan baada ya kuzidiwa matusi ndio mpango mzima kwani Hanna jinsi
 
Hao kina mama ndiyo waliompa kula John Mnyika unamtafutia matatizo Mnyika siku akiende kuomba kula Manzese.
hawa walimnyima kura mnyika na kumpa yule mama yenu kilaza aliyegaragazwa na john.
 
Last edited by a moderator:
Moderator.

Kwa heshima na taadhima naomba tafadhari usifute wala kuunganisha thread hii.

Natambua kwa miaka mingi iliyopita chuo kikuu cha Dar es salaam kilijijengea heshima kwa kuwa tanuru la kuchakata na kuoka fikra na tafakuri tunduizi. Natambua kuwa katika miaka ya nyuma maswala yote magumu ya mkwamo kwenye nchi yalikuwa yakijadiliwa objectively kwenye viunga vya chuo kikuu cha dar es salaam kwa weledi na kwa usawa wa hali ya juu.

Leo kwenye mdahalo wa nini kifanyike bunge la katiba likiendelea wiki ijayo, nimeona kwa dhahiri mdahalo huu umeitishwa tu kwa jina la UDASA lakini ukweli ni kwamba ilikuwa mdahalo wa CCM ukimshirikisha Tundu Lissu kwa minajili ya kufunika kombe ili mwana haramu apite. Na hili limedhihirishwa na kauli ya Lukuvi akimsifu Lissu na kumuona kama ka mzizi ka UKAWA.

Ukiangalia namna wazungumzaji walivyo kuwa wanapewa fursa za kuchangia kwenye mdahalo ule, bila chembe ya shaka utagundua kuwa hakukuwa na fursa sawa ya uchangiaji. Sikuona mantiki ya kumuita Mwigulu Nchemba na kuacha kumuita miongoni mwa washiriki walio tambuliwa awali kama Mheshimiwa Machali na David Kafulila lakini wakati huohuo nafasi ya kuchangia akipewa kada Kunambi wa Ccm.

Haikuwa sahihi kuacha kumpa nafasi ya kuchangia mtu wa kariba ya Prof Sheriff na kumpa nafasi kijana kutoka zanzibar ambaye hata historia ya Zanzibar aliipotosha huku pia akiongea kwa kujiamini lakini kwa kupotosha kuwa tume ya Warioba haikwenda kuchukua maoni Zanzibar.

Kulikuwa na vigezo gani kumpa nafasi ya kuchangia Prof Tabaijuka aliyekiri kuwa hata katiba mpya isipo patika bado ni ushindi kwa ccm na jk huku akiacha Prof Sheriff na Dr Lwaitama tena bila hata kutambuliwa kuwa wako ukumbini?!

Nimebaki najiuliza, wale vijana walio kuwa wanaitwa kuchangia ikiwa ni pamoja na baadhi ya wazee walio ishia kuzomewa, majina yao yalipatikana vipi na ni utaratibu upi ulio tumika?

Umetumika utaratibu upi na vigezo gani vya kuwa na wazungumzaji wengi wa ccm kuliko wazungumzaji wanao unda kundi la ukawa?! Kwa nini hakukuwa na usawa wa wachangiaji?!

Kwa nini mdahalo wa UDASA uhitimishwe na Lukuvi (mccm) nasi mwenyekiti wa UDASA?!

Nabaki najiuliza? Mdahalo ulioandaliwa chuo kikuu ulikuwa wa Udasa au Ccm?! Kama ccm imefanikiwa kuingilia mpaka uhuru wa vyuo vikuu tunaachaje kuamini kuwa elimu pamoja na taasisi zilizo heshimika za elimu ya juu ziko shakani kwa kuendeshwa kwa remote control na kutumika kisiasa?!

Acha.kupanic ww wangeshangiliwa CHADEMA ungesema UDASA ndio wameandaa
 
Back
Top Bottom