CCM and UDASA, this is shameful

CCM and UDASA, this is shameful

Honey Faith

Wamekodiwa kwa kazi zote mbili, kuzomea na kushangilia kihasara hasara hivi! Inategemea na wakati tu.
Unakumbuka pale ubungo plaza mlileta akina nani? Acheni kuumia iliwatokea, sasa nakutaarifu kuwa kwa mdahalo wa leo Wassira kawafanya kitu mbaya.
 
Last edited by a moderator:
Wekeni hoja muondoke, hayo ya CCM waachieni wenyewe
 
Makene...

Ni kwa nini Tundu Lissu asingekataa mwaliko?...

Ilishaelezwa hapa nini CCM wanafanya kuhusiana na Kongamano hilo...Nimeshangaa sana kuwaona Lissu, Machali , Kafulila na wajumbe wengine wa UKAWA kama sehemu ya Kongamano hilo...
Ni lazima wawepo ili ukweli ujulikane. Kina wasira na chemba wakiachwa wenyewe wataeneza sumu kwa wananchi wanaowatizama na kuwasikiliza.
 
Hii movie ipo chini ya Kijana mmoja anaitwa DANIEL ZENDA,alishamaliza chuo mda mrefu Lkn bado anakazania cheo cha Mwenyekiti wa Mkoa Wa Vyuo Vikuu!!
Yeye ndiye aliyeratibu zoezi la kubeba vijana wa kwenda kuzomea na kushangilia...Vijana wengi wamekutania maeneo ya Buguruni na kupanda basi za UDA kwenda Nkurumah.
Huyu ZENDA ni mfuasi wa Wassira kindakindaki...hata vijana wangu wawili wa mtaani kwangu leo wameenda Nkurumah ili wapate hela ya vocha.Hapa ndipo tulipofikia kama Taifa...
Inaumiza sanaaa
 
Tumaini Makene mbona iko wazi kuwa UDASA inaongozwa na mwenyekiti Dr Francis Michael ambaye ni mjumbe wa bunge la katiba ambaye ni CCM wa kutupa. Katibu ni Faraja Kristomus ambaye ni CCM damu. What do you expect?

Udasa inatumiwa vibaya sana sana na ni aibu ya mwaka. Wanafunzi udsm wako likizo wote lakini hapa wanasingizia waliomo ndani ni wasomi. Nimewashuhudia wakiletwa na mabasi matatu ya uda mbele ya utawala ili kuja kushangilia wanaccm wanaochangia. Shame on Udasa!
 
Comrade Makene.

Yaani pale mkuruma ni maigizo ya hali ya juu.mdahalo umelengwa kwenye maagizo maalum kutoka ccm na meza kuu imeonyesha unazi huo wa wazi wazi. hata watu waliokua wanapewa mic na muhongoza mdahalo. Unaona alikua analenga mrengo flani. Ni tofauti na midahalo inayoendeshwa na [itv] watu upewa mic kutokana na idadi ya watu waliopo katika mdahalo na sio kuwachagua mahususi kwa hili ni haibu kwa [udasa] na [star tv] na tena leo nashangaa hata [tbc] wamehongwa maana ni dhairi kulikua na katu nyuma ya panzia.
 
Makene...

Ni kwa nini Tundu Lissu asingekataa mwaliko?...

Ilishaelezwa hapa nini CCM wanafanya kuhusiana na Kongamano hilo...Nimeshangaa sana kuwaona Lissu, Machali , Kafulila na wajumbe wengine wa UKAWA kama sehemu ya Kongamano hilo...

lisu hakwenda katika malumbano. Ila amekwenda kuwapa watu ufahamu wa kile wananchi wasichokijua
 
Wamefunga tovuti ya tume ,wamewadhalilisha wajumbe wa tume ,kila kukicha wanafanya hila na ghilba rej.kukatwa matangazo ya TBC alipokuwa anaongea prof kabudi,wamebadili kanuni kuwabana walio wachache,wamevunja kanuni kumtanguliza mwenyekiti was tume badala ya rais n.k Hivi bado mnaamini wanna Nia na katiba mpya?
 
Duh! sasa mbona aliyezomewa ni Lukuvi na si Lissu ama wengine. Huu uzi kidogo una ukweli na wakati mwingine uzushi wakati mwingine tuwape heshima zinazostahili wasomi wetu.
 
nashangaa sana kuona akili ndogo kama za lukuvi zinaendelea kutawala nchi
 
Haya maandalizi aliyakataa Kitila Mkumbo jana

Hapo CCM inawashusha watu wake
Mbona nawaona watu wawili tu unataka kuniambia hawa ndiyo wamejaza hilo kongamano halafu kama UKAWA walijua hayo yote kwa nini Tundu Lissu na wenzake wamekwenda kwenye hilo kongamano.
 
Back
Top Bottom