Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Chama kipya chenye usajili wa muda cha CCJ ambacho ni mbadala wakiitikadi, mwelekeo, mfumo na uongozi wa CCM kitafanya mkutano na waandishi wa habari Alhamisi Mei 13, 2010 majira ya saa saba mchana kwenye ukumbi wa MAELEZO kutoa utafafanuzi wa mambo mbalimbali kikiwa njiani kuelekea kupata usajili wa kudumu.
CCJ hadi hivi sasa kimekamilisha uhakiki wake wa ndani wa wanachama wake katika mikoa mbalimbali na mkoa wa Mwanza tu ndio uhakiki wa ndani utakamilika mapema Alhamisi na hivyo kuwa tayari kwa uhakika wa Msajili.
Sehemu mbalimbali ambako viongozi wa CCJ wamepita wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kutaka kujiunga na kujua undani wake wakiamini kuwa hatimaye kile Chama ambacho Nyerere alikuwa anakiotea kije ili kiwe mbadala (siyo tishio tu) la CCM hatimaye kimewadia.
Hata hivyo "vi-nzi" vinadokeza kuwa kutokana na utofauti wa CCJ na vyama vingine viliyvyopo kuna uwezekano mkubwa wa wakuu kuhakikisha kinacheleweshewa usajilii wa kudumu ili kisiweze kushiriki uchaguzi mkuu. Hata hivyo, support ambayo imepatikana hadi hivi inahakikisha kuwa msajili hatakuwa na kisirani cha kukinyima usajili na jambo hili litafanyika mapema zaidi ili kuwatendea haki wanachama maelfu ambao wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu chama kama hiki.
Tutawaletea taarifa mbalimbali kesho kwa kadiri nitakavyozipata.
CCJ - Tumaini Jipya la Watanzania, kuelekea mabadiliko ya kweli!'
Kwa maelezo zaidi:
Constantine Akitanda
CCJ, Katibu Mwenezi Taifa
Tel:
Dar es Salaam+255 717 116 386
KUTOKA KWA MICHUZI
CCJ yakabidhi majina ya wanachama wake leo
Mwenyekiti wa CCJ Mh. Richard Kiyabo akionesha risiti ya stakabadhi ya malipo ya kuwakilisha majina ya wanachama leo ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa jijini Dar
CCJ hadi hivi sasa kimekamilisha uhakiki wake wa ndani wa wanachama wake katika mikoa mbalimbali na mkoa wa Mwanza tu ndio uhakiki wa ndani utakamilika mapema Alhamisi na hivyo kuwa tayari kwa uhakika wa Msajili.
Sehemu mbalimbali ambako viongozi wa CCJ wamepita wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kutaka kujiunga na kujua undani wake wakiamini kuwa hatimaye kile Chama ambacho Nyerere alikuwa anakiotea kije ili kiwe mbadala (siyo tishio tu) la CCM hatimaye kimewadia.
Hata hivyo "vi-nzi" vinadokeza kuwa kutokana na utofauti wa CCJ na vyama vingine viliyvyopo kuna uwezekano mkubwa wa wakuu kuhakikisha kinacheleweshewa usajilii wa kudumu ili kisiweze kushiriki uchaguzi mkuu. Hata hivyo, support ambayo imepatikana hadi hivi inahakikisha kuwa msajili hatakuwa na kisirani cha kukinyima usajili na jambo hili litafanyika mapema zaidi ili kuwatendea haki wanachama maelfu ambao wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu chama kama hiki.
Tutawaletea taarifa mbalimbali kesho kwa kadiri nitakavyozipata.
CCJ - Tumaini Jipya la Watanzania, kuelekea mabadiliko ya kweli!'
Kwa maelezo zaidi:
Constantine Akitanda
CCJ, Katibu Mwenezi Taifa
Tel:
Dar es Salaam+255 717 116 386
KUTOKA KWA MICHUZI
CCJ yakabidhi majina ya wanachama wake leo
Mwenyekiti wa CCJ Mh. Richard Kiyabo akionesha risiti ya stakabadhi ya malipo ya kuwakilisha majina ya wanachama leo ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa jijini Dar
Viongozi wa Chama Cha Jamii (CCJ) wakimkabidhi majina ya wanachama wa bara na visiwani Mkuu wa Masijala katika ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, Bi. Mwajuma Amir. Kutoka kulia ni Naibu Katibu wa chama hicho kwa upande wa Zanzibar, Mh. Ali Hatibu Ali, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Mh. Renatus Muabhi, Mwenyekiti wa Chama hicho, Mh. Richard Kiyabo na Katibu Mwenezi Taifa, MNh. Costantine Akitanda. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika ofisi za msajili wa vyama vya siasaMtaa wa Shaaban Robert jijini Dar.
Viongozi wa kitaifa wa CCJ wakiondoka ofisi za Msajili wa Vyama baada ya kukabidhi majina ya wanachama wao wa bara na visiwani