Bibi Ntilie
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 245
- 8
If CCJ people want to participate in the next GE let them join existing parties. There are 18 parties to join or take over. These people are politically naive my brother.
The easiest way was to take a small party like UMD, JAHAZI ASILIA etc, call the national congress and change the name. They decided to take a long route. Reason? They were not real, they just wanted to threaten their old party CCM so that it accommodates them.
I know the essence of CCJ. I spoke to all people they claim to have especially the ethical elders. These are my wazee and i meet them every weekend. None of them is in CCJ. These guys once upon a time visited some elders, and let the Intelligence system know that, and then declared a party. This CCJ thing is hoax. This CCJ confuses us.
Tupige mstari na kujipanga kwenda mbele. Those in CJJ with liberal minds join CUF, those with conservative minds come CHADEMA, those with socialist orientation join NCCR-M or TLP. Tusipoteze muda, we need more MPs in the house.......
Mheshimiwa Zitto,
Maneno yako yanasikitisha sana. Yanasikitisha kwa sababu inaelekea wanaotakiwa na wenye haki na uwezo wa kuanzisha vyama vya upinzani ni watu wenye majina, wananchi wa kawaida kamwe hawapaswi kufanya hivyo. Ama vyama vya siasa shurti viwe na majina ya wanaojulikana ili vipate uhalali wa kuwa vyama vya siasa!
Hivi wakati nyie waheshimiwa wa CHADEMA na vyama vingine vilivyopo mlipokuwa mnaanzisha vyama vyenu nyote mlikuwa na majina yanayovuma nchini? Zitto si ulianzia chini na labda uwezo wako wa kujieleza Bungeni ndio ukakujengea jina? Sasa umekuwa maarufu unaweza kuongea na wazee kila weekend basi Watanzania wenzio wanaojaribu kutaka kujaribu kama ninyi mlivyojaribu na kushindwa kutupeleka peponi, unawakejeli.
Pia nasikitika kusema kwamba sioni mantiki yoyote ya wewe kuja na maneno kwamba unaongea na baadhi ya the so called wazee kila weekend. So what?
Acheni maneno yenu na kejeli kwa wananchi wenzenu ambao wanaona nchi inavyokwenda kombo na wanajaribu kudhihirisha ukereketwa wao kwa njia ambazo zinaruhusiwa na Katiba ya nchi. Nyie tangu muanzishe vyama vyenu hakuna lolote la maana mnalofanya zaidi ya kuangalia nchi inavyosambaratika.
Mimi ni mstaafu. Nimeishuhudia nchi hii ilivyokuwa ikiendeshwa tangu tupate Uhuru hadi sasa. Huko tuendako siko kabisa kulikodhamiriwa. Sasa labda nikutume ukawaambie hao Wazee unaoongea nao, je wao wanaridhika kuona nchi inavyokwenda? Na kama hawaridhiki wanafanya nini kusaidia nchi irudi kwenye mstari au ndio nao wameishakata tamaa kabisa na wako tayari kuiona nchi inatumbukia shimoni?
Wakati nyie mnaridhika na hali halisi, angalieni mamia kwa maelfu kama si mamilioni ya wananchi wanavyoteseka kutokana na hali ngumu ya maisha kwa sababu tu nyie mmeamua kwamba mnayo haki zaidi ya kuanzisha vyama kuliko wao, wakianzisha wenzenu mko tayari kupiga vita na kukejeli; mnayo haki ya kuwa Wabunge, viongozi n.k. kwa hiyo mnayo haki ya kupata share kubwa ya keki ya taifa wakati wananchi wenzenu wanapata mashahara usiokidhi mahitaji hata ya wiki moja, wanakufa na njaa, hawapati tiba zinazostahili na wala watoto wao hawaendi shule kwa sababu nyinyi ndio mna haki na mnastahili kupata kuliko wao. Aliyesema "mwenye shibe hamjui mwenye njaa" kweli hakukosea!
Niko kwenye 'bedrest' lakini baada ya kusoma madudu humu nimeona nitoe mawazo yangu!!