Captain Tesha awaacha watanzania kwenye mataa

Captain Tesha awaacha watanzania kwenye mataa

Jamaa mbwe mbwe zote zile na kuahidi atarudi kabla ya uchaguzi kutoa tamko lakini mpaka sasa ameufyata kimya.

Sasa tumueleweje? Je naye amelambishwa asali?

Kapewa onyo na wakubwa wake wa kazi?

Kabadili maamuzi kwa mapenzi yake?

Au alikuwa anatafuta umaarufu (attention seeker)?
Labda tayari ni R.I.P
 
Siasa kama mapenzi usiwekeze sana roho na nafsi yako itakuumiza vibaya.
 
Capt. Tesha amefanya ya kwake kwa nafasi yake na wakati wake, tujiulize wewe na mimi tumefanya nini?

Tunataka tulishwe kwa kijiko hadi mdomoni?

Kwa vyovyote itakavyokuwa Capt. Tesha ameingia katika historia ya juhudi za ukombozi na kutetea haki, atakumbukwa na kusomwa vizazi na vizazi. Je, wewe na Mimi tutakumbukwa kwa nini?

Yote kwa yote Capt. Tesha, Humphrey polepole, Gwajima, Warioba, Heche, Lissu, na wengineo wote waliosimana katika ukweli tuwape heshima zao inavyostahili. Wao wamemwaga mafuta sisi kazi yetu ni kuwasha moto.
 
Yule kafanya alichoweza, walau ni jasiri na shujaa, ni askari hasa. Sio sisi tunajificha kwenye ID fake na tunalalamika kwa chinichini, wengine ndo unafiki mwingi...ambao ni sifa ya Mtanzania. Kaweka historia yule...katimiza alichotaka kufanya, kaongea
 
Jamaa mbwe mbwe zote zile na kuahidi atarudi kabla ya uchaguzi kutoa tamko lakini mpaka sasa ameufyata kimya.

Sasa tumueleweje? Je naye amelambishwa asali?

Kapewa onyo na wakubwa wake wa kazi?

Kabadili maamuzi kwa mapenzi yake?

Au alikuwa anatafuta umaarufu (attention seeker)?
Chai
 
Tesha hana deni na sisi ila JWTZ imesaliti watanzania..imepoteza heshima yake kubwa sana.

Zamani nilikua najua vyombo vyote vya ulinzi vinaliogopa JWTZ na sehemu ambapo jeshi lipo lazima viufyate ila jambo la kusikitika mauaji haya yaliyotokea yalifanyika mbele yao wakiwa kazi yao kusaidia kubeba majeruhi🚮...wanaangalia tu wananchi ambao ndo mabosi zao ambao ndo wanawalinda wakiuwawa kinyama.
 
Tesha hana deni na sisi ila JWTZ imesaliti watanzania..imepoteza heshima yake kubwa sana.

Zamani nilikua najua vyombo vyote vya ulinzi vinaliogopa JWTZ na sehemu ambapo jeshi lipo lazima viufyate ila jambo la kusikitika mauaji haya yaliyotokea yalifanyika mbele yao wakiwa kazi yao kusaidia kubeba majeruhi🚮...wanaangalia tu wananchi ambao ndo mabosi zao ambao ndo wanawalinda wakiuwawa kinyama.
Ulitaka Jeshi lisaidie magaidi yaliyokuwa yanachoma Petrol Stations na Maduka ya Watz? Utakuwa na matatizo ya akili wewe!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom