Camouflagers na informers

Ufafanuzi ni kwamba nchini Marekani na nchi nyingine zilizoendelea ndiyo wanaofata vizuri kanuni za kuajiri watu wa kitengo,yani ni wale tu wenye IQ kubwa na si vinginevyo.Na ndiyo maana hata ukiwa bar nchini Marekani huwezi kusikia mtu akijisifia kuwa yeye yupo kitengo.Ushahidi ni huu ufuatao;Marekani hao watu wa kitengo wapo wengine wanaoshughulikia ujasusi wa kiuchumi,yani wanaenda nchi nyingine kwa lengo la kuchunguza namna ya kufanya ili nchi yao ipate uchumi mkubwa kwakupitia nchi nyingine.Wakati viinchi maskini vimejikita ktk ujasusi wa kidola tu,huku uchumi ukiachwa pembeni,na ndiyo maana mikataba ya kijinga inasainiwa.Ikumbukwe watu wote wenye IQ kubwa hufikiri kwa kutumia ubongo na siyo tumbo.
Intelligence yetu huwa inafatilia mno siasa aisee, wajikite kwenye uchumi, wenzetu wanaanzisha NGOS kwa malengo flani flani huku kwetu kufatilia wakosoaji tu.
 
Mi ndo mana huwa simwamini mtu hafu wengi huja na mada chokonozi kwenye group kwa malengo yake, nakumbuka nilisoma kisa cha CIA kumpandikiza muislamu mwenye msimamo Mkali kwenye msikiti na yeye ndo aliyekuwa ana plan ugaidi kumbe ni agent wenzake wakaenda kumshitaki nikajua hii dunia nikuwa makini na Ku angalia mambo ya kuongea ukiwa na watu unao wa fahamu na usio waelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
I also read a black ops book recently...it is full of stories about spies who were planted in different places to disguise others and collect the information they needed.
Hapa kwetu hawa wanaokuja kwa makundi kuleta habari njema ya Mwenyezi Mungu au kusaidia vijana au hata kuwekeza....we got to watch them with wide, open eyes
 
Ni ngumu sana
Unaweza hata kumkuta akijifanya chizi maarifa
Muuza urembo
Mwalimu
Fundi nknk kulingana na nature ya kazi...

Jr
Hahaaaa! Mshana kwa ufupi mwambie Carter asimdharau na kumwamini yeyote kwa hili, asimkute teja kituo cha daladala anatokwa udenda akamchukulia huyu si teja tu! daah ni kosa kubwa mno, lakini ajitahidi kuishi kwa nidhamu ili asijenasa kwenye mitego ya hawa wasanii,mimi hupenda kuwaita wasanii kwa kuwa wana uwezo ama weledi wa kuvaa uhalisia utafikiri wao ndo wenyewe kumbe wanaishi kulingana na mazingira kwa lengo maalum.

Cha msingi tuishi kwa kufuata sheria tusije dondokea mikononi mwa watu wa hivi.
 
Ufafanuzi ni kwamba nchini Marekani na nchi nyingine zilizoendelea ndiyo wanaofata vizuri kanuni za kuajiri watu wa kitengo,yani ni wale tu wenye IQ kubwa na si vinginevyo.Na ndiyo maana hata ukiwa bar nchini Marekani huwezi kusikia mtu akijisifia kuwa yeye yupo kitengo.Ushahidi ni huu ufuatao;Marekani hao watu wa kitengo wapo wengine wanaoshughulikia ujasusi wa kiuchumi,yani wanaenda nchi nyingine kwa lengo la kuchunguza namna ya kufanya ili nchi yao ipate uchumi mkubwa kwakupitia nchi nyingine.Wakati viinchi maskini vimejikita ktk ujasusi wa kidola tu,huku uchumi ukiachwa pembeni,na ndiyo maana mikataba ya kijinga inasainiwa.Ikumbukwe watu wote wenye IQ kubwa hufikiri kwa kutumia ubongo na siyo tumbo.
Unatushawishi tusome kitabu cha Yericko boss "Ujasusi Wa Kidola Na Kiuchumi "
Au ndo the Big boss mwenyewe?
 
I also read a black ops book recently...it is full of stories about spies who were planted in different places to disguise others and collect the information they needed.
Hapa kwetu hawa wanaokuja kwa makundi kuleta habari njema ya Mwenyezi Mungu au kusaidia vijana au hata kuwekeza....we got to watch them with wide, open eyes
Bora wanao kuja kwa habari njema sikuhizi hizi NGOs ndo malengo yao mi nilishangaa watu ni wageni wanajua Tanzania in details had makabila, hafu wanajifanya kutoa misaada, ndo nikajua Africa u maskini wetu hautakaa uishe wenzetu wanatumia ujasusi kuendekea kutukandamiza, na kutusoma madhaifu yetu then tunabaki tukishang'aa sharubu
 
I also read a black ops book recently...it is full of stories about spies who were planted in different places to disguise others and collect the information they needed.
Hapa kwetu hawa wanaokuja kwa makundi kuleta habari njema ya Mwenyezi Mungu au kusaidia vijana au hata kuwekeza....we got to watch them with wide, open eyes
Naomba jina la hiki kitabu Tafadhali, nikitafute
 
Kama ni wanaridhaa(amateurs) wataacha alama ila kama ni wajuzi (professionals) kutrace alama zao ni kazi moja kubwa sana

Jr
LOL ila we jamaa una akili sana,inafikiaga mahala huwa nadhani hiyo akaunti yako inatumiwaga na mtu zaidi ya mmoja,ama ni akaunti ya kikundi fulani.kwa kifupi wewe ni kisima cha ujuzi wa mambo.Nahitimisha kwa kusema huwa nafuatilia kwa utulivu sana mada zako,watu wanaokudharau wana upeo mdogo sana.

watu wanadhani kujua mambo mengi ya giza ni uchawi,wala sio kweli ,mapadiri na wachungaji,na maimamu wanajua mengi sana juu ya giza lakini sio wachawi,na kujua si kutenda, hii ni kutokana na kwamba waumini wao ni waathirika wakubwa wa mambo ya giza, na makimbilio yao ni kwa viongozi hao wa dini.
wewe ni jembe.
 
LOL ila we jamaa una akili sana,inafikiaga mahala huwa nadhani hiyo akaunti yako inatumiwaga na mtu zaidi ya mmoja,ama ni akaunti ya kikundi fulani.kwa kifupi wewe ni kisima cha ujuzi wa mambo.Nahitimisha kwa kusema huwa nafuatilia kwa utulivu sana mada zako,watu wanaokudharau wana upeo mdogo sana.
watu wanadhani kujua mambo mengi ya giza ni uchawi,wala sio kweli ,mapadiri na wachungaji,na maimamu wanajua mengi sana juu ya giza lakini sio wachawi,na kujua si kutenda, hii ni kutokana na kwamba waumini wao ni waathirika wakubwa wa mambo ya giza, na makimbilio yao ni kwa viongozi hao wa dini.
wewe ni jembe.
asante sana kwa compliment... Am humbled....
 
KISWAHILI ni wazugaji na wafichua habari
Ni watu maalum lakini wa kila jinsia umri na kaliba... Kati yao wapo mpaka wezi matapeli, wakabaji na wachawi.. Lakini kila walipo wapo kwa lengo maalum.... Kutoa taarifa ambazo zitasaidia kubaini waovu na kuzuia hatari ama kulinda usalama wa nchi raia ama viongozi....
Hawa watu hutumika kwa namna tatu
1. Kutoa taarifa muhimu za kihalifu zinazosaidia kuepusha janga fulani katika jamii... Iwe la kiongozi ama jumuiya
2.Hutumika kuwajenga viongozi na propaganda za kukubalika kwa kiongozi fulani katika jamii
3. Hutumika wakati wa hatari ya usalama wa nchi,mipango ya mauaji ya viongozi, mapinduzi ya kijeshi, maandamano migomo nk
Ni aina ya watu wenye elimu na waliopewa mafunzo maalum juu na namna ya kuvaa uhusika fulani bila kujulikana, namna ya kuongea, kuripoti na kutoweka eneo la tukio bila kuacha alama yoyote na kujulikana uhalisia....

Mfano wa kwanza
Kiongozi mkubwa anapotaka kutembelea eneo fulani, wazugaji na watoa taarifa za siri hufika wiki moja ama zaidi kabla ya ziara rasmi... Hapa hujigawa katika makundi mawili
. kundi la kwanza ni la kusoma hali ya hewa kiusalama na kukubalika kwa kiongozi.. Mambo mabaya yanayotendwa na viongozi wa eneo husika na maoni ya wadau
. kundi la pili ni wazugaji. Hawa ni wana kitengo cha propaganda ili kuonyesha kukubalika, kuaminika na kuungwa mkono kwa kiongozi na imani juu ya wale aliowatembelea.. Hapa si ajabu kumkuta kiongozi anakula chakula mtaani kwenye banda fulani bila hofu, kunywa kinywaji kama dafu ama kula kitu kama karanga tunda nk... Wauzaji wa vitu vyote hivi ni watumishi wake waaminifu

Mfano wa pili
Nchi inapopitia kipindi cha mashaka kama maandamano usaliti na mapinduzi..
Hapa huangaliwa kwanza maeneo yenye ushawishi mkubwa wa jambo husika.... Ndipo hupelekwa timu ya watu maalum!! Mfano anafika mtu wa kawaida kwenye bar ya kawaida mtaani, ambapo pembezoni kuna kijiwe na bodaboda nk.. Huyu aliyeko bar anakuwa busy na simu na kinywaji chake... Hana story na mtu... Kisha anakuja mwingine mzugaji kama machinga, anajifanya anauza keyholders kwa bei poa sana na kama huna hela anakukopesha...
Bila kujua zile keyholders zina mawasiliano ya moja kwa moja na jamaa aliyeko pale bar

Mfano wa tatu
Hatari ya kuvamiwa kijeshi... Hapa ni pakubwa na penye mengi lakini wanawake warembo hutumika sana kipindi hiki... N kundi lingine ni wazugaji wanaojifanya ni wafanyabiashara wakubwa na watafiti wanaotaka kuwekeza ama kutafiti....
Yote kwa yote jihadhari sana na mikusanyiko yenye dhumuni la maandamano hasa ya kisiasa ama kupinga jambo fulani kitaifa... Ukiachana na wale askari wa fanya fujo uone wenye mabomu ya machozi na risasi za mpira, huwa kuna mdunguaji mmoja tu hatari sana kwa ajili ya kumdungua kiongozi ama walio mstari wa mbele... Kimbia jifiche....

Unaposikia kiongozi kafika mahali na watu fulani wamewajibishwa kwa haki, tambua wazi ni kazi iliyotukuka ya wazugaji na wafichua habari
Unaposikia maandamano, mgomo ama mapinduzi fulani yameshindikana jua fika kwamba kuna kazi kubwa imefanywa na hawa jamaa
ILA unapoona mojawapo kati ya hayo niliyotaja yamefanikiwa vizuri, basi hawa jamaa ama wamefeli ama wanekengeuka miiko yao..!
Kamwe usiwaamini hawa watu hata kama ni ndugu yako... HAWATABIRIKI...!



Jr
teh..teh...teh... wewe kama humo vile ila sijajua unatokea kundi gani sijui ndo lile la wachawi au wabahili?....natania tu!
 
Back
Top Bottom