Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Hakuna Jambo linalodhorotesha Utumishi wa umma nchini Kama hii style yakutumbuana kila siku. Viongozi wa nchi wameacha kutafuta suluhu ya matatizo ya wananchi badala yake wamejikita kutumbua kila siku na bila hoja ya msingi. Clip ikirushwa mtandaoni tayari mtu amefukuzwa kazi bila kujali uhusika wake.
Lakini pia utaratibu huu umeligharimu taifa fedha nyingi sana ambazo zingeweza kusaidia kufanyika kwa shughuli nyingine zakulisaidia taifa.
Kumtumbua mtu kunaambatana na kumlipa maslahi yake na kama alikuwa mwajiriwa wa kudumu serikalini anarejea kazi yake ya awali bila kushuka kwa mshahara wake Jambo linalopelekea mtu kulipwa fedha nyingi kwa majukumu yasiyolingana na mshaara.
Wananchi wamekuwa wakishangilia lakini wakumbuke anayetumbuliwa analitia taifa hasara kwa kulipwa benefits za cheo alichokuwa nacho pamoja na gharama nyingine ikiwemo kusafirisha familia na mizigo kurejea eneo lake la makazi au kituo Cha kazi kwa wale wanaorejea ofisi zao za awali.
Wanaharakati nao pia wamekuwa wakipiga kelele kushangilia na kufurahia, wanasiasa vilevile na wasomi kwa jumla.
Kiwango Cha uteuzi na utumbuaji Tanzania ni kikubwa kwa miaka mitano iliyopita nadhani kuliko Taifa lolote Duniani. Je watu wanaoteuliwa Wana sifa? Kama Wana sifa je, anayetengua ana sababu zakutengua au nikufurahisha adhara?
Kwa mfumo huu unaoendelea, ni mteule gani wa Rais atakayekuwa na courage ya kusimama na kuongoza wakati anajua akitumbuliwa jamii inamzomea? Kwanini viongozi wasiwe unpopular kulinda cv zao? Leo hii kwa style inayoendelea kama tungepewa nafasi yakuwatumbu Marais kwa mapungufu yao tungekuwa na Marais wangapi?
Nadhani ni wakati wakusema kutumbua No la sivyo wanaotumbuliwa watiwe hatiani ili wakose stahiki zao na kuliepusha Taifa na gharama za mishahara mikubwa ya watendaji wanaorudi kukaa benchi huku wakinufaika na marupurupu ya vyeo vyao.
Lakini pia utaratibu huu umeligharimu taifa fedha nyingi sana ambazo zingeweza kusaidia kufanyika kwa shughuli nyingine zakulisaidia taifa.
Kumtumbua mtu kunaambatana na kumlipa maslahi yake na kama alikuwa mwajiriwa wa kudumu serikalini anarejea kazi yake ya awali bila kushuka kwa mshahara wake Jambo linalopelekea mtu kulipwa fedha nyingi kwa majukumu yasiyolingana na mshaara.
Wananchi wamekuwa wakishangilia lakini wakumbuke anayetumbuliwa analitia taifa hasara kwa kulipwa benefits za cheo alichokuwa nacho pamoja na gharama nyingine ikiwemo kusafirisha familia na mizigo kurejea eneo lake la makazi au kituo Cha kazi kwa wale wanaorejea ofisi zao za awali.
Wanaharakati nao pia wamekuwa wakipiga kelele kushangilia na kufurahia, wanasiasa vilevile na wasomi kwa jumla.
Kiwango Cha uteuzi na utumbuaji Tanzania ni kikubwa kwa miaka mitano iliyopita nadhani kuliko Taifa lolote Duniani. Je watu wanaoteuliwa Wana sifa? Kama Wana sifa je, anayetengua ana sababu zakutengua au nikufurahisha adhara?
Kwa mfumo huu unaoendelea, ni mteule gani wa Rais atakayekuwa na courage ya kusimama na kuongoza wakati anajua akitumbuliwa jamii inamzomea? Kwanini viongozi wasiwe unpopular kulinda cv zao? Leo hii kwa style inayoendelea kama tungepewa nafasi yakuwatumbu Marais kwa mapungufu yao tungekuwa na Marais wangapi?
Nadhani ni wakati wakusema kutumbua No la sivyo wanaotumbuliwa watiwe hatiani ili wakose stahiki zao na kuliepusha Taifa na gharama za mishahara mikubwa ya watendaji wanaorudi kukaa benchi huku wakinufaika na marupurupu ya vyeo vyao.