CAG fanya ukaguzi maalum kwa waliotumbuliwa ili kuona hasara Taifa iliyopata na ushauri mbinu kukabiliana na utumbuaji usio na tija

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Hakuna Jambo linalodhorotesha Utumishi wa umma nchini Kama hii style yakutumbuana kila siku. Viongozi wa nchi wameacha kutafuta suluhu ya matatizo ya wananchi badala yake wamejikita kutumbua kila siku na bila hoja ya msingi. Clip ikirushwa mtandaoni tayari mtu amefukuzwa kazi bila kujali uhusika wake.

Lakini pia utaratibu huu umeligharimu taifa fedha nyingi sana ambazo zingeweza kusaidia kufanyika kwa shughuli nyingine zakulisaidia taifa.

Kumtumbua mtu kunaambatana na kumlipa maslahi yake na kama alikuwa mwajiriwa wa kudumu serikalini anarejea kazi yake ya awali bila kushuka kwa mshahara wake Jambo linalopelekea mtu kulipwa fedha nyingi kwa majukumu yasiyolingana na mshaara.

Wananchi wamekuwa wakishangilia lakini wakumbuke anayetumbuliwa analitia taifa hasara kwa kulipwa benefits za cheo alichokuwa nacho pamoja na gharama nyingine ikiwemo kusafirisha familia na mizigo kurejea eneo lake la makazi au kituo Cha kazi kwa wale wanaorejea ofisi zao za awali.

Wanaharakati nao pia wamekuwa wakipiga kelele kushangilia na kufurahia, wanasiasa vilevile na wasomi kwa jumla.

Kiwango Cha uteuzi na utumbuaji Tanzania ni kikubwa kwa miaka mitano iliyopita nadhani kuliko Taifa lolote Duniani. Je watu wanaoteuliwa Wana sifa? Kama Wana sifa je, anayetengua ana sababu zakutengua au nikufurahisha adhara?

Kwa mfumo huu unaoendelea, ni mteule gani wa Rais atakayekuwa na courage ya kusimama na kuongoza wakati anajua akitumbuliwa jamii inamzomea? Kwanini viongozi wasiwe unpopular kulinda cv zao? Leo hii kwa style inayoendelea kama tungepewa nafasi yakuwatumbu Marais kwa mapungufu yao tungekuwa na Marais wangapi?

Nadhani ni wakati wakusema kutumbua No la sivyo wanaotumbuliwa watiwe hatiani ili wakose stahiki zao na kuliepusha Taifa na gharama za mishahara mikubwa ya watendaji wanaorudi kukaa benchi huku wakinufaika na marupurupu ya vyeo vyao.
 
Ndugu usiandike kitu kwa miemko ujui changamoto wanazopitia wananchi kwa viongozi mizigo kama hao unao watetea wanajiona mungu watu wanapokua kwenye utendaji wao wanashindwa kutatua changamoto za wananchi ndugu yangu morogoro kuna uozo mwingi sana kuhusu watendaji wa halmashauri
 
Hivi ni tatizo ni utumbuaji usokuwa na tiba au uteuzi wa kimazoea??
Ifike kipindi Rais apunguziwe kazi... Na kuwepo inclusive national vetting committee!
 
Hakuna Jambo linalodhorotesha Utumishi wa umma nchini Kama hii style yakutumbuana kila siku. Viongozi wa nchi wameacha kutafuta suluhu ya matatizo ya wananchi badala yake wamejikita kutumbua kila siku na bila hoja ya msingi. Clip ikirushwa mtandaoni tayari mtu amefukuzwa kazi bila kujali uhusika wake.

Lakini pia utaratibu huu umeligharimu taifa fedha nyingi sana ambazo zingeweza kusaidia kufanyika kwa shughuli nyingine zakulisaidia taifa.

Kumtumbua mtu kunaambatana na kumlipa maslahi yake na kama alikuwa mwajiriwa wa kudumu serikalini anarejea kazi yake ya awali bila kushuka kwa mshahara wake Jambo linalopelekea mtu kulipwa fedha nyingi kwa majukumu yasiyolingana na mshaara.

Wananchi wamekuwa wakishangilia lakini wakumbuke anayetumbuliwa analitia taifa hasara kwa kulipwa benefits za cheo alichokuwa nacho pamoja na gharama nyingine ikiwemo kusafirisha familia na mizigo kurejea eneo lake la makazi au kituo Cha kazi kwa wale wanaorejea ofisi zao za awali.

Wanaharakati nao pia wamekuwa wakipiga kelele kushangilia na kufurahia, wanasiasa vilevile na wasomi kwa jumla.

Kiwango Cha uteuzi na utumbuaji Tanzania ni kikubwa kwa miaka mitano iliyopita nadhani kuliko Taifa lolote Duniani. Je watu wanaoteuliwa Wana sifa? Kama Wana sifa je, anayetengua ana sababu zakutengua au nikufurahisha adhara?

Kwa mfumo huu unaoendelea ,ni mteule gani wa Rais atakayekuwa na courage yakusimama na kuongoza wakati anajua akitumbuliwa jamii inamzomea? Kwanini viongozi wasiwe unpopular kulinda cv zao? Leo hii kwa style inayoendelea kama tungepewa nafasi yakuwatumbu Marais kwa mapungufu yao tungekuwa na Marais wangapi?

Nadhani ni wakati wakusema kutumbua No la sivyo wanaotumbbuliwa watiwe hatiani ili wakose stahiki zao na kuliepusha Taifa na gharama za mishahara mikubwa ya watendaji wanaorudi kukaa benchi huku wakinufaika na marupurupu ya vyeo vyao
Naunga mkono hoja, na hili hata mimi niliwahi kulisema hapa
P.
 
Hakuna Jambo linalodhorotesha Utumishi wa umma nchini Kama hii style yakutumbuana kila siku. Viongozi wa nchi wameacha kutafuta suluhu ya matatizo ya wananchi badala yake wamejikita kutumbua kila siku na bila hoja ya msingi. Clip ikirushwa mtandaoni tayari mtu amefukuzwa kazi bila kujali uhusika wake.

Lakini pia utaratibu huu umeligharimu taifa fedha nyingi sana ambazo zingeweza kusaidia kufanyika kwa shughuli nyingine zakulisaidia taifa.

Kumtumbua mtu kunaambatana na kumlipa maslahi yake na kama alikuwa mwajiriwa wa kudumu serikalini anarejea kazi yake ya awali bila kushuka kwa mshahara wake Jambo linalopelekea mtu kulipwa fedha nyingi kwa majukumu yasiyolingana na mshaara.

Wananchi wamekuwa wakishangilia lakini wakumbuke anayetumbuliwa analitia taifa hasara kwa kulipwa benefits za cheo alichokuwa nacho pamoja na gharama nyingine ikiwemo kusafirisha familia na mizigo kurejea eneo lake la makazi au kituo Cha kazi kwa wale wanaorejea ofisi zao za awali.

Wanaharakati nao pia wamekuwa wakipiga kelele kushangilia na kufurahia, wanasiasa vilevile na wasomi kwa jumla.

Kiwango Cha uteuzi na utumbuaji Tanzania ni kikubwa kwa miaka mitano iliyopita nadhani kuliko Taifa lolote Duniani. Je watu wanaoteuliwa Wana sifa? Kama Wana sifa je, anayetengua ana sababu zakutengua au nikufurahisha adhara?

Kwa mfumo huu unaoendelea, ni mteule gani wa Rais atakayekuwa na courage ya kusimama na kuongoza wakati anajua akitumbuliwa jamii inamzomea? Kwanini viongozi wasiwe unpopular kulinda cv zao? Leo hii kwa style inayoendelea kama tungepewa nafasi yakuwatumbu Marais kwa mapungufu yao tungekuwa na Marais wangapi?

Nadhani ni wakati wakusema kutumbua No la sivyo wanaotumbuliwa watiwe hatiani ili wakose stahiki zao na kuliepusha Taifa na gharama za mishahara mikubwa ya watendaji wanaorudi kukaa benchi huku wakinufaika na marupurupu ya vyeo vyao.
Bite, hili uliwahi lisema, jana limetajwa Bungeni Kwenye hotuba ya bajeti kuu ya serikali
Kati ya vitu ambavyo Magufuli alikuwa akiimbwa navyo ni kubana matumizi ya Serikali

Ila leo baada ya kumsikiliza Mwigulu akiweka mikakati mipya ya kubana matumizi, nimeona kumbe Serikali ina matumizi ya hovyo ambayo hata huyo Magufuli aliendelea nayo hadi sasa Samia ndio anakuja kuyapunguza

Mojawapo ya lililonishtua ni kuwa Mkurugenzi au Katibu Mkuu akitumbuliwa bado anaendelea kulipwa mshahara uleule aliokuwa nao, akasema kuwa inawezekana hata ukakuta kuna wizara 15 tu lakini ukakuta kuna watu 50 wanalipwa mshahara wa katibu mkuu, ama kuna halmashauri 100 lakini wanaolipwa kama wakurugenzi ni 500.

Aisee
Mkuu Johnny Sack , kumbe hili wewe ndio umelijua jana!, karibu angalia tarehe ya bandiko hili uone watu tulisema nini na lini
Nilisema
Wanabodi,
  1. Maofisa Kuwekwa Pembeni Kusubiri Kupangiwa Kazi Nyingine. Mfano wanaposikia maofisa wakuu fulani wa umma, wamesimamishwa kazi, na kuteuliwa wengine kukaimu nafasi zao!. Hatua hii kisiasa ni nzuri, maana ina mpa kick Magufuli kwa ku boost political mileage yake, na hivi ndivyo wafanyavyo ma populist leaders dunia nzima, boosting their political mileage tuu ila kiuchumi inatuumiza na kuliumiza taifa!. Magufuli analibebesha taifa hili mzigo mkubwa wa gharama kuliko hata serikali ya JK!. Kwa mujibu wa sheria za kazi, kila mtumishi aliyesimamishwa kazi kwa tuhuma zozote zile, anaendelea kulipwa mshahara wake wote ule ule kamili, bali marupurupu ndio yanaondolewa!. Mtumishi atalipwa nusu ya mshahara iwapo tuu atasimamishwa kazi na kushitakiwa, na mtumishi hatalipwa kabisa mshahara iwapo atafukuzwa kazi!. Tangu rais Magufuli aanze hii timua tumua, hakuna ofisa mkuu yoyote aliyefukuzwa kazi, wala aliyeshitakiwa, wote wamesimamishwa tuu kazi na kusubiri kupangiwa kazi nyingine!, au wengine teuzi zao zimetenguliwa huku wote wakiendelea kulipwa mishahara yao ile ile!.
  2. Makatibu Wakuu Wanaolipwa Bila Kazi!. Hata upande wa uteuzi wa Makatibu Wakuu, wale Makatibu Wakuu wote ambao Ukatibu wao Mkuu haukutenguliwa, au wameachwa tuu bila kupangiwa kazi nyingine yoyote, wote wanaendelea kulipwa mishahara yao ya makatibu wakuu kusubiria ama kupangiwa kazi nyingine, ama kustaafu kwa umri, au kustaafishwa kwa manufaa ya umma, lakini wakati huu wote wanaosubiria, walalipwa na kupatiwa haki na stahiki zote za level ya Katibu Mkuu!.
Hitimisho
Hivyo baadhi ya hatua zinazochukuliwa na rais wetu Dr. John Pombe Magufuli, japo ni hatua nzuri, na zimefanywa kwa nia njema kabisa, zikiachwa tuu hivi hivi jinsi hii hii inavyo fanyika, zitaligharimu sana taifa hili!, ni bora rais Magufuli angefuata ule mtindo wa Nyerere, ilikuwa hakuna kusimamisha kazi, ilikuwa ni kufukuza tuu au kustaafisha kwa manufaa ya umma!. Anapounda baraza jipya na kuteua makatibu wakuu wapya, wale wote walioachwa, walipaswa kustaafishwa there and then na mishahara yao inasimamishwa kuanzia pale pale walipostaafishwa!.

Hili ninalolisema leo, wengine mtakuja kuliona mwezi Juni /July wakati wa kusomwa kwa bajeti kuu ya serikali, mtashuhudia kuongezeka kwa bajeti ya uendeshaji wa serikali ikiwemo wage bill badala ya kupungua na mbele ya safari mtashuhudia mabadiliko mengi ya baraza za mawaziri au kwa kuwaongeza, au kuzipunguza vizara alizoziunganisha kwa kuziachanisha!. Na kila siku mawaziri watateuliwa na kutumbuliwa kama kubadili nguo, kwa sababu Magufuli huyu ambaye sasa ndie rais wetu, ni Magufuli huyu huyu niliyemzungumza hapa

Happy New Year
Paskali.
Rejea
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!.

Jee Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?- Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?.

Maendeleo ya kweli TZ Yataletwa na Elimu na Ukweli. Tusidanganye, Tusidanganywe, Tusidanganyike!

P
P.
 
Dhana ya kutumbua ni kielelezo cha kutofuata misingi ya utawala wa sheria na utawala bora. Aliyekua mtumbuaji mkuu wa serikali alikua kilaza kwenye sheria za kazi na hakuwa na abc za implications za kiuchumi wakati anatekeleza hiyo kazi kikatili.
 
Back
Top Bottom