CAF Champions League

CAF Champions League

Nadir Haroub na Kelvin Yondani wanatakiwa wafanye kazi kubwa sana ya kumlinda Deogratius Munishi, Domayo afanye kazi kubwa sana ya kuziba penetration passes zote, kungekuwa nauwezekano akapata japo nusu ya uwezo wa Gilberto Silva wakati yuko Arsenal itakuwa nzuri sana, kama wataruhusu mashambulizi ya mara kwa mara mabeki wa Yanga huwa wanashindwa kuelewana hasa wale wa kati. Sina wasi wasi sana na mabeki wa pembeni ingawa pia hata mashambulizi ya Ah Ahly mara nyingi huwa wanapenda kutokea pembeni na kumimina krosi kwa hiyo Msuva na Okwi nao inabidi wawe wanafanya jitihada za kurudi kusaidia wakati timu inashambuliwa. Kiiza na Kavumbagu hawatakiwi kufanya makosa ya kosa kosa, nafasi moja goal moja, nafasi ya pili goal la pili.
mkuu Masuke, karbia kila post yko unaongea uhalisia mtupu.
ni kuomba MUNGU vijana wetu wafanye kweli ili tuweze kuwatoa hao waarabu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Masuke siku za hivi karibuni kocha mkuu wa Yanga amekua akimlalamikia Niyonzima kwamba anachelewesha mashambulizi ya Yanga kwa kukaa na mpira muda mrefu na kumtaka abadilike ktk mechi ya marudiano na waaarabu,jee huoni kwamba pengine kocha amefurahi kuona Niyonzima ni mgonjwa?maana kwa nionavyo mimi Yanga kwa kikosi hiki watatumia mfumo wa:4-2-3-1 wakiwa na nia ya kushambulia kwa spidi kubwa kupitia pande zote,pembeni na katikati.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Masuke siku za hivi karibuni kocha mkuu wa Yanga amekua akimlalamikia Niyonzima kwamba anachelewesha mashambulizi ya Yanga kwa kukaa na mpira muda mrefu na kumtaka abadilike ktk mechi ya marudiano na waaarabu,jee huoni kwamba pengine kocha amefurahi kuona Niyonzima ni mgonjwa?maana kwa nionavyo mimi Yanga kwa kikosi hiki watatumia mfumo wa:4-2-3-1 wakiwa na nia ya kushambulia kwa spidi kubwa kupitia pande zote,pembeni na katikati.

Hiyo 4-2-3-1, huyo namba moja ni nani, Kiiza au Kavumbagu? Sikatai, ni kweli Niyonzima yuko slow lakini huwa anakuwa slow kwa mahesabu, kwangu mimi mchezaji akiwa slow huku akiangalia mpira aupeleke wapi sioni tatizo, tena huyo anaweza kuwa ni bora zaidi kuliko mwenye haraka na akapoteza mpira, ndo maana nikasema Niyonzima ni msaada sana hasa timu inapokuwa imezidiwa na pengine kocha aliona kwamba Niyonzima yuko slow kwa sababu mechi nyingi ambazo Yanga imecheza chini ya huyu kocha Yanga ndo ilikuwa inadictate tempo ya mchezo na mara nyingi tempo ilikuwa ni ya juu kwa maana kwamba Yanga walikuwa na kasi na muda mwingi walikuwa wanamiliki mpira, kwa hali hiyo huwezi kuona umhimu wake.
 
Mkuu Masuke hapo Kavumbagu ndiye mshambuliaji wa mwisho,Kiiza,Okwi na Msuva ni wapishi watakoukua wanampikia kavumbagu huku nao wakijaribu kufunga na kupiga mashuti,Ila kwa maoni yangu kama kipindi cha kwanza Yanga itaenda sare basi kipindi cha pili kutakua na aja ya kumpumzisha kiiza na kumuingiza Luhende ili kuendelea kuwapa wakati mgumu waarabu.Na hapo kwenye na8 Ngasa atafiti vema maana ni mwepesi wa kuponyoka na kupiga pasi "sumu"Kiukweli leo tukiwatoa waarabu nina uhakika tu
 
Last edited by a moderator:
Utabiri wa watu makini na sio mashabiki kama wewe
Al Ahly 7-Yanga 0
Jumla Al Ahly 7-Yanga 1

Leo sina utabiri, nilipokuwa katika njozi usiku niliona mechi imeisha kwa 1-0, nilitamani sana kujua ni timu gani imeshinda, sikuona muda ukiongezwa wala penati zikipigwa, niliona wachezaji wenye jezi za njano na kijani wakimsifu Mungu.
 
Leo sina utabiri, nilipokuwa katika njozi usiku niliona mechi imeisha kwa 1-0, nilitamani sana kujua ni timu gani imeshinda, sikuona muda ukiongezwa wala penati zikipigwa, niliona wachezaji wenye jezi za njano na kijani wakimsifu Mungu.
na iwe kama ilivyokuwa ndoto yako!
 
Yule mshambuliaji wetu hatari alieshindwa kucheza hapo dar sababu ya majeruh leo yuko fit na anaanza..sisi waarabu lazima tuwanyonye damu hawa yanga
 
Si swala la bahati,nia,sababu na uwezo tunao!mwarabu akijitahidi sana sare.
 
Mm simba lakini kwanza uzalendo...kila la kheri yanga...make Tanzania proud..wishing u all the best..mungu ibariki Tanzania..

Wewe sio mzalendo...isipokuwa wewe hujielewi....Mzalendo wa timu ya taifa sio yanga...Naombea yanga wapigwe kama nne hivi
 
Si swala la bahati,nia,sababu na uwezo tunao!mwarabu akijitahidi sana sare.

Mshindwe kupata ushindi mnono hapa nyumbani eti mkashinde Misri...Wallah...ntatembea uchi kutoka posta hadi kimara
 
Leo sina utabiri, nilipokuwa katika njozi usiku niliona mechi imeisha kwa 1-0, nilitamani sana kujua ni timu gani imeshinda, sikuona muda ukiongezwa wala penati zikipigwa, niliona wachezaji wenye jezi za njano na kijani wakimsifu Mungu.
teh,teh,mkuu nasikia makipa wote ------------,au ndo mnatatafuta sababu mkifungwa
 
Back
Top Bottom