CAF Champions League

CAF Champions League

Walisha anza kukuangusha dar huko usitegemee jipya mkuu.we lala mapema hauna haja ya kupoteza usingizi ukiiombea mabaya yanga.

mkuu kule ni ARABUNI,huo mfupa ulimshinda TUPISO MAZEMBE
kwa ukanda huu wa kusini mwa jangwa la sahara
mwenye uwezo wa kumfunga mwarabu ni SIMBA SC
 
mkuu kule ni ARABUNI,huo mfupa ulimshinda TUPISO MAZEMBE
kwa ukanda huu wa kusini mwa jangwa la sahara
mwenye uwezo wa kumfunga mwarabu ni SIMBA SC
Kwan hao simba wako wapi si waende basi wakamfunge...mnafikir hili kombe kama la mtani jembe sio? Nye subirin mabonanza huku hamuwez hata kidogo.
 
Mkuu Masuke kwanini unafikili kwamba kutokuwepo Niyonzima ni hatari kwa Yanga?maana ata ili mechi waliyocheza na Ruvu Shooting Niyonzima hakuwepo na Yanga ilipanga kikosi hikihiki na kikashinda mabao 7-0....je huoni kama leo ni kiama kwa Ahly?
cc watu8 ndetichia Kitoabu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Masuke mimi nakubaliana nawewe kuhusu Yanga kama watarudia makosa walioyafanya hapa home.
Kukosa nafasi nyingi kila wanapofika langoni, tulipata nafasi nyingi sana.
Pia wawe wajanja wa kulinda lango siyo waachie wee tufungwe magoli yasiyohesabika.

Kama wao waliruhusu goli moja nasi tuwe wajanja hata pale mambo yatakapokuwa magumu kiasi kwamba tumeshindwa basi goli liwe moja tu ndio tufungwe.
All in all Mungu ibariki Yanga, naamini juhudi na kujituma, umoja na Kuomba dua yote yanawezekana.
 
Mkuu Masuke kwanini unafikili kwamba kutokuwepo Niyonzima ni hatari kwa Yanga?maana ata ili mechi waliyocheza na Ruvu Shooting Niyonzima hakuwepo na Yanga ilipanga kikosi hikihiki na kikashinda mabao 7-0....je huoni kama leo ni kiama kwa Ahly?
cc watu8 ndetichia Kitoabu

Mkuu usilinganishe uwezo wa Ruvu shooting na hao waarabu, Kiukweli Niyonzima ni kiungo mzuri sana kwa sababu zifuatazo. Kwanza anao uwezo wa kumiliki mpira na kupiga chenga watu kadhaa, mchezaji wa namna hii anakuwa na faida sana kama timu yake imezidiwa kwa sababu akichukua mpira anao uwezo wa kujua mpira niupeleke wapi na kama haoni sehemu nzuri ya kuupeleka atakao nao ili wenzake wajipange hicho kitu Ngasa hana.

Pili kutokana na uwezo alio nao Niyonzima kwenye mechi ngumu ndo huwa anang'ara sana ama kutoa pasi ya goli au kufunga yeye mwenyewe sasa unapomkosa mtu kama huyo ni tatizo, ana umbo dogo lakini ana stamina ya hali ya juu na pasi zake zina macho na ni mhamasishaji mkubwa anapokuwa uwanjani.
 
Mkimtumia vzuri emmanuel mna goli moja na likiingia hilo goli na likakubaliwa pakini ndege juu ya treni....
 
Piga hao yanga 8 bila warudi kucheza ligi ya bata huku
 
Mkuu Masuke mimi nakubaliana nawewe kuhusu Yanga kama watarudia makosa walioyafanya hapa home.
Kukosa nafasi nyingi kila wanapofika langoni, tulipata nafasi nyingi sana.
Pia wawe wajanja wa kulinda lango siyo waachie wee tufungwe magoli yasiyohesabika.

Kama wao waliruhusu goli moja nasi tuwe wajanja hata pale mambo yatakapokuwa magumu kiasi kwamba tumeshindwa basi goli liwe moja tu ndio tufungwe.
All in all Mungu ibariki Yanga, naamini juhudi na kujituma, umoja na Kuomba dua yote yanawezekana.


Nadir Haroub na Kelvin Yondani wanatakiwa wafanye kazi kubwa sana ya kumlinda Deogratius Munishi, Domayo afanye kazi kubwa sana ya kuziba penetration passes zote, kungekuwa nauwezekano akapata japo nusu ya uwezo wa Gilberto Silva wakati yuko Arsenal itakuwa nzuri sana, kama wataruhusu mashambulizi ya mara kwa mara mabeki wa Yanga huwa wanashindwa kuelewana hasa wale wa kati.

Sina wasi wasi sana na mabeki wa pembeni ingawa pia hata mashambulizi ya Ah Ahly mara nyingi huwa wanapenda kutokea pembeni na kumimina krosi kwa hiyo Msuva na Okwi nao inabidi wawe wanafanya jitihada za kurudi kusaidia wakati timu inashambuliwa. Kiiza na Kavumbagu hawatakiwi kufanya makosa ya kosa kosa, nafasi moja goal moja, nafasi ya pili goal la pili.
 
Back
Top Bottom