CAF Champions League

CAF Champions League

mpaka sasa haukuna kituo cha hapa nchini kilichojinasibu kuonyesha,kuna vituo nane vya misri vitaonyesha japo haviwekwa wazi na uongozi wa yanga umetuahidi kutuwekea link ili tufuatilie kwa internet,' KIDUMU CHAMA CHA YANGA'.

anha okay..Kidumu daima........
 
JF TV tutakua live hapa.
We mwambie shemeji leo asikubugudhi kabisaaaaa!
Fundi mitambo wangu Makoye Matale na ACCOUNT FULL natumai tutakua pamoja hapa huku wachambuzi wetu studio Masuke Ndetchia watakua wakichambua mechi hii bila kuegemea upande wowote.

hahaa shemeji yako leo hayupo so hakuna wa kunibugudhi
hiyo team imekaa poa sana
tutafatilia mwanzo mwisho,niko humu ndani............
 
mpaka sasa haukuna kituo cha hapa nchini kilichojinasibu kuonyesha,kuna vituo nane vya misri vitaonyesha japo haviwekwa wazi na uongozi wa yanga umetuahidi kutuwekea link ili tufuatilie kwa internet,' KIDUMU CHAMA CHA YANGA'.

Mechi saa ngapi kwa EAT?
 
JF TV tutakua live hapa. We mwambie shemeji leo asikubugudhi kabisaaaaa! Fundi mitambo wangu Makoye Matale na ACCOUNT FULL natumai tutakua pamoja hapa huku wachambuzi wetu studio Masuke Ndetchia watakua wakichambua mechi hii bila kuegemea upande wowote.
.
pamoja mkuu..leo vijana hawatatuangusha, japo tutapoteza wadau humu kwa muda.
 
Last edited by a moderator:
.
pamoja mkuu..leo vijana hawatatuangusha, japo tutapoteza wadau humu kwa muda.
Na yanga ikishinda tu na kumtoa muarabu tutegemee machafuko makubwa pale kwenye msongamano lile vuguvugu la rage na simba lazima liibuke.teee.......teeeee.,...teeeee.
 
Kama kawa kama dawa,leo lazima waarabu wakae,na hiki hapa ndicho kikosi kitakachoanza kuwaua waarabu leo,Niyonzima ni mgonjwa nadhani ata kwenye bench hatakuwepo.
Line up:Yanga.
1.Deo Munishi
2.Twite Mbuyu
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub
5.Kelvin Yondani
6.Frank Domayo
7.Saimon Msuva
8.Mrisho Ngasa
9.Didier Kavumbagu
10.Emmanuel Okwi
11.Hamisi Kiiza

ivi Kaseja mlimchukua ''wa kupigia picha''?acheni kuua vipaji vya watu
 
JF TV tutakua live hapa.
We mwambie shemeji leo asikubugudhi kabisaaaaa!
Fundi mitambo wangu Makoye Matale na ACCOUNT FULL natumai tutakua pamoja hapa huku wachambuzi wetu studio Masuke Ndetchia watakua wakichambua mechi hii bila kuegemea upande wowote.

Mkuu tatizo nikiweka uchambuzi wangu hapa watu kama kina Makoye Matale, WABHEJASANA, watu8 , Anselm, ram, Heaven on Earth, ACCOUNT FULL, Bantu lady, BASIASI wataniona niko biased.

Kikosi chenu kimepangwa vizuri sana ila kumkosa Haruna Niyonzima ni pengo kubwa sana kwa Yanga nilitajia awepo kikosini na pengine Kiiza angeanzia benchi lakini ndo shida kama alivyoimba Mbaraka Mwaruka Mwinshehe haina hodi, yenyewe siku yoyote tu inaingia.

Tukiweka ushabiki pembeni, hii mechi ni ngumu kwa timu zote mbili na kama Yanga wanautaka ushindi kweli hawatakiwi kufanya uzembe kama walivyofanya kwenye mechi ya awali, walicheza vizuri na kupata nafasi nyingi za kufunga lakini walishindwa kuzibadili na kuwa magoli, uzembe ambao mwaka juzi uligharimu kwa Zamalek, walicheza vizuri sana mechi ya hapa nyumbani wakapata nafasi nyingi lakini wakashindwa kufunga magoli kilichofuata wote tunajua. Mechi hii ya leo hawatakiwi kupoteza nafasi za kufunga.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom