Bye bye tigo

Bye bye tigo

Sasa kwenye menu yangu 15000 kimewekwa wiki badala mwezi...wanacheza sana hawa tigo...yaani kuanzia leo line yangu ya tigo itakuwa napokea simu tu...bassss ...wamevikosa visenti vyangu vya kuchangachanga...
 
hee! wana mambo. haya na mie najiunga sana cha wiki, wakikiondoa......

Hiko cha wiki watakiondoa na kitakuwa cha siku...jitayarishe kuhama na wewe....hiyo ndio bongo ...
 
Yaani aliyebadilisha jina la tigo na kulipa ile maana mbaya ningemjua ningempa zawadi ...maana kawapatia sana...they deserve that meaning..
 
Mimi niliwawekea mgomo voda tangu mwaka jana sijaweka vocha, napokea tu kwa sababu ya upuuzi mdogo hivi hivi (tangu kipindi kile walipoweka dakika za mgao) . Na nilikuwa naweka 15000 kwa mwezi kwa hiyo za miezi yote hii wameshazikosa na hawanipati ng'o nipo baba lao.
 
Mimi niliwawekea mgomo voda tangu mwaka jana sijaweka vocha, napokea tu kwa sababu ya upuuzi mdogo hivi hivi (tangu kipindi kile walipoweka dakika za mgao) . Na nilikuwa naweka 15000 kwa mwezi kwa hiyo za miezi yote hii wameshazikosa na hawanipati ng'o nipo baba lao.

Nakuja huko...tigo imekula kwao...
 
Nimekuwa nikijiunga kifurushi cha 15000 kila mwezi . Sasa tigo wamekiondoa kwenye menu yangu sasa kuna cha 50.000 na cha 100.000 . Nimewapigia kuwauliza mbona sioni kifurushi cha 15000 ,nikaambiwa kimeondolewa kwangu kwa kuwa nimeonekana najiunga nacho sana .. kwa iyo nimeonekana tajiri sana ...Airtel nakuja kwenu nipokeeni..bye bye tigo

Mimi na TTCL tu hadi nife...
 
Yani kama ulikuwepo nilimfokea huyo jamaa wa tigo ..hasira zote nikammalizia yeye...yeye akanijibu kimeondolewa kwako kwa kuwa unajiunga nacho sana...

mie walinijibu kijeuri kabsa system imeonyesha unaeka sana vocha nyingi hivyo ndo imekuondolea nkamwambia hyo system itawaamuliaje watu aina ya bundle akasema ndo hivyo kisha akamalizia una jngne tukusaidie
 
mie walinijibu kijeuri kabsa system imeonyesha unaeka sana vocha nyingi hivyo ndo imekuondolea nkamwambia hyo system itawaamuliaje watu aina ya bundle akasema ndo hivyo kisha akamalizia una jngne tukusaidie

Ungemwambia jengine lipo ni kwamba mi nawaageni tigo mi bye bye...
 
Yaani tigo kampuni ya ajabu sana...wakikuona unajiunga sana na vifurushi wanaondoa baadhi yake..badala wanipe zawadi kwa kuwa mteja wao mzuri eti wao ndo wananikimbiza..yaani usaniii + wizi = tigo
 
Yani jama tu nimewakimbia voda nikaja tigo nikijua Paramus okay kumbe nl majangs tu. Ngoja nirudi zangu voda
 
Afu nimejiunga cha mwezi yani speed hakuna. Vodacom kudawnload movie nilikuwa nachukuwa 1hr ti tayari ila tigo cku nzima
 
Afu nimejiunga cha mwezi yani speed hakuna. Vodacom kudawnload movie nilikuwa nachukuwa 1hr ti tayari ila tigo cku nzima

TCRA sijui wanaona matatizo haya ....au wapo wapo tuuu...wanazungusha viti ofisini..
 
Hivi ule mkongo sijui mkonga uliishia wapi? Maana ulikuja na mbwembwe kweli.

Ule mkonga umesambaa sana mkuu, ila matunda hatuyaoni, sijui wanashindwa nini kufunga wireless dar nzima wakati mkonga upo pale bure kabisa
 
Tigo Mtandao wao kama maeneo ya Kunduchi Juu, Mivumoni na Wazo hauna nguvu kabisa. Nalipia Kaban za wiki lakini ni WIZI mtupu. Bora kuhama
 
Ule mkonga umesambaa sana mkuu, ila matunda hatuyaoni, sijui wanashindwa nini kufunga wireless dar nzima wakati mkonga upo pale bure kabisa

Mkuu kwani dar ndo kuna watanzania tuu ? huduma zao mbovu plus majanga..
 
Kumbe kushusha gharama ile mwanzo walipoanza na maofa tele ilikuwa kuwavutia watu ili wajazane kisha wamalize kama ule mtego wa tenga unaweka na chupa ya soda shingoni unaifunga kamba ndani unamwagia mtama njiwa wakishaingia unavuta kamba tenga linashuka, mateka kibao.

Kweli biashara mbinu
 
Back
Top Bottom