By Any-means, usimuambie ChatGPT “Roast Me”!

By Any-means, usimuambie ChatGPT “Roast Me”!

Pumbavu 😂

Screenshot_20260430-224915.png


Ai n vile unavyomlisha taarifa zako na sio kwamba anajua siri zako, hapa kwangu amekosea Vitu kibao tuu
 
Hizi AI ziko ki surveillance sana, na epuka kuzi feed vitu kama Personally Identifiable Information. Kama wewe ni mfuatilia utagundua hawa jamaa wewe ndio unawafundisha katika kufikiri, na wataalamu waki intelijensia kama watataka taarifa muhimu kwako, kama wakipitia simu huenda wakapata taarifa zako nyingi kama huwa una share kwa namna moja au nyingine taarifa binafsi

Kuna jamaa wanaitwa Antropic, nilikuwa naitumia hii nikaja kuachana nayo baada yakuona wana mvutano na serikali ya marekani katika suala muhimu inayohusu taarifa za siri za mtu binafsi. Chakushangaza wakati natumia AI hii ilinipa jina la kampuni nayofanya kazi bila mimi kui feed mahala napofanya kazi

Hapa nikawa aware kuwa Hizi AI usi point direct kila unachotaka kikusaidi wewe kama muhitaji jaribu kutengeneza script au prompt ambayo haiku point direct wewe kama wewe
 
Kuna kipindi nilikuwa napenda sana kusoma habari za nyota ila mwisho wa siku nikaja kugundua jamaa walizipanga sifa za nyota ambazo kila mtu anazo, kwa mfano utaambiwa wewe unanyota ya punda pia wewe unakiu sana ya mafanikio, sasa swali la kujiuliza ni nani ambaye hana kiu ya mafanikio?

Nimemjaribu huyo AI naona ametembea na sifa zile zile za ujumla ambazo kila mtu anazo.....ni ngumu sana mtu kuweka tabia yake kwa AI mara nying watu huweka vijitabia vya muda mfupi ambavyo huwa havikai sana
 
Back
Top Bottom