BVR Yamkataa Goodluck Jonathan Nigeria

BVR Yamkataa Goodluck Jonathan Nigeria

JAYJAY

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2008
Posts
8,795
Reaction score
9,153
Naomba kuchukua nafasi hii kuitaarifu Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi kuwa makini na ubora wa mashine maalumu za BVR zitakazotumika kwenye zoezi zima la uandikishaji na uchaguzi.

Katika uchaguzi mkuu wa leo nchini Nigeria, Rais anayewania muhula wa pili Bwana Goodluck Jonathan mashine ilikataa kumtambua mara tatu kabla ya kufanikiwa.

Hali hii inaweza kupelekea upotezaji wa muda na hofu kwa mhusika, Kwa hiyo Wajipange Kweli Kweli!
 
Duh inamkataa rais, hiyo ni dalili hata wananchi watamktaa!
 
Tume yetu si ilienda kuomba vifaa hivyo, kumbe navyo ni feki!
 
Mmh inamaana taarifa zake hazikuwa sahihi au ndo digitali kwenye nchi zetu
 
Pia shida ni kwa makarani wa tume,sijui wamechukuliwa ki ujomba ujomba,maana ni kama laptop ndio wanaiona leo pia speed ya kwenye keyboard ni shida,wanadonyoa herufi moja moja na huku vidole vikiwa vimekakamaa utadhani wanarusha rosho kwenye taarabu,kazi anayo Mzee Lubuva na analogue yake.
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuitaarifu Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi kuwa makini na ubora wa mashine maalumu za BVR zitakazotumika kwenye zoezi zima la uandikishaji na uchaguzi.

Katika uchaguzi mkuu wa leo nchini Nigeria, Rais anayewania muhula wa pili Bwana Goodluck Jonathan mashine ilikataa kumtambua mara tatu kabla ya kufanikiwa.

Hali hii inaweza kupelekea upotezaji wa muda na hofu kwa mhusika, Kwa hiyo Wajipange Kweli Kweli!

Ni kawaida kwa hizo mashine inategemea orientation ya vidole kama unaweka kama vile ulivyoweka wakati wa kuchukuliwa your finger print.
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuitaarifu Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi kuwa makini na ubora wa mashine maalumu za BVR zitakazotumika kwenye zoezi zima la uandikishaji na uchaguzi.

Katika uchaguzi mkuu wa leo nchini Nigeria, Rais anayewania muhula wa pili Bwana Goodluck Jonathan mashine ilikataa kumtambua mara tatu kabla ya kufanikiwa.

Hali hii inaweza kupelekea upotezaji wa muda na hofu kwa mhusika, Kwa hiyo Wajipange Kweli Kweli!
Inasemekana kakaa kituoni dakika 50! Kisha mchakato wenyewe ni mrefu, unatambuliwa na baadaye unarudi kuja kupiga kura. Yeye alitakiwa kurudi saa saba kupiga kura! Wametayarisha maji na sabuni kuwanawisha wapiga kura! Hapa kwetu itakuwa kazi kweli kweli.
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuitaarifu Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi kuwa makini na ubora wa mashine maalumu za BVR zitakazotumika kwenye zoezi zima la uandikishaji na uchaguzi.

Katika uchaguzi mkuu wa leo nchini Nigeria, Rais anayewania muhula wa pili Bwana Goodluck Jonathan mashine ilikataa kumtambua mara tatu kabla ya kufanikiwa.

Hali hii inaweza kupelekea upotezaji wa muda na hofu kwa mhusika, Kwa hiyo Wajipange Kweli Kweli!

Haikufanikiwa ..wamemuandikisha manually ndio kaweza kupiga kura
 
Wanigeria na tecnolojia yao yote bado wanahangaishwa na Bvr, je kwa sie wa kuunga unga Si itakua majanga.!!
 
Mkuu kweli kabisa tume imelazimika kutoa maelekezo baadhi ya taratibu zifanyike manually!
 
Black Continent umeme wa visado mnahangaika na Technolojia ya juu kiasi hicho kwanini ?... NIDA wangekuwa makini kuwaandisha Watanzania zoezi la kupiga kura lingekuwa jepesi sana ...
 
io ni kwa nigeria taifa ambalo wapo mbele yetu .hapa kwetu sijui itakuaje.ni bora tume ikachukua tahadhari mapema
 
Wanigeria na tecnolojia yao yote bado wanahangaishwa na Bvr, je kwa sie wa kuunga unga Si itakua majanga.!!

Geoge w bush alizigomea sasa kwetu Afrika unadhani itakuaje.Hata hivyo Data za tume ya uchaguzi ya Nigeria ziliingiliwa.inasadikika mambo c shwari kwa Chama tawala.
 
Nje ya BVR hakuna tech nyingine ya kuandikisha watu?
 
Waafrica tu a vidole vigumu sana ..tunatakiwa kutengenezewa bvr machine zetu zenye uwezo wa ku detect ngozi ngumu kama turubai
 
Back
Top Bottom