Butiku na wenzake ni 'wahaini'

Siyo aliwekwa ndani. Alishtakiwa huyo yeye na marehemu mdogo wake akiitwa John ambaye alikuwa Trade Unionist. Hao wawili kwa sababu wana ujamaa na Oscar Kambona, Kambona recruited them. Huyu alipokamatwa alikuwa Captain Dan Lifa Chipaka. Kwa hiyo alishtakiwa na kesi ikasikilizwa na akafungwa kama sikosei. Walimtuhumu Nyerere na walikuwa wakimwita "Mchonga meno". Wakati wa kesi he was quite outspoken. Walitaka kumpindua Nyerere kwa sababu nchi wakati huo ilikuwa chini ya utawala wa udikteta wa chama kimoja.Mahakama iliwapata na makosa na akafungwa. Kwa hiyo anamposema Butiku inaeleweka kuwa kapata sababu ya kumcharaza. Kwani Butiku 2005 si alikuwa anamuunga mkono Salim. Sasa na yeye kapata sababu ya kumcharaza JK. Hiyo ndiyo si hasa (Siasa).
 
“Viongozi na wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere isipokuwa Butiku, wote ni mawaziri wakuu wastaafu na mawaziri, wamekosea kuonyesha misimamo yao katika warsha hiyo na kumchafua kwa matusi Rais Kikwete, jambo ambalo si sahihi, tunashangaa kwa nini hawakukamatwa na kushitakiwa kwa makosa ya jinai na uhaini, kesi ambazo huvuta adhabu kali na kubwa,” walisema bila kutaja majina ya viongozi hao.

Sikutegemea Chipaka atumie neno "uhaini" kirahisi rahisi namna hii! Katika watu wote yeye alitakiwa kujua athari zake.

Amandla........
 
Heshima kwako FMEsm

Nimependa andiko lako kwa kweli Muungwana kashikwa pabaya mbaya zaidi bado anafikiria Watanzanda ni mabwege.Kwa mara ya kwanza nadhani Muungwana anamuhitaji Ngoyai amsaidie kuweka mambo sawa,Ngoyai angekuwepo asingekubali hizi cheap propaganda kuwatumia kina Chipaka na maandamano ya waislam jumamosi ni makosa ya kuwa na timu ya watu wa hovyo

Sidhani kwamba Muungwana anajali sana kwa kuwa anao watu wa kumsemea!

Jana nilimsikiliza Agustino Lyatonga Mrema Mwenyekiti wa Chama cha Upinzani cha TLP akihojiwa na Mlimani TV. Akiulizwa kuhusu nia yake ya kutaka kugombe ubunge na akakiri kwamba ameamua kufanya hivyo ili awatumikie wana'nji'. Hilo sikuliona bizzare sana lakini sikuamini masikio yangu nilipomsikia anamfagilia Rais Kikwete na kuwashutumu wale walioongea kwenye Kongamano la Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuelezea mapungufu wanayoyaona katika utendaji wa Rais, serikali na Chama tawala. Hvi hapo atakapokwenda jukwaani kujinadi kwa wananchi bila shaka ataendelea kufagia-fagia tu!

Jamani njaa haina heshima wala utu!

Nilipochoka kusikiliza ya Mrema nikahamia ITV nione kulikoni? Nikakuta mjadala wa jopo la watu wanne - Prof Mushi wa REDET, Mzee Mbawala (sikumbuki wa wapi) Mbunge Beatrice Shelukindo na Mbunge Ole Sendeka. Huko nako hakukuwa na jipya ni kwamba wanaodai/wanaotaka Rais achukue maamuzi magumu tayari alifanya hivyo kwa kukubali kustaafu kwa Lowassa na kuwafikisha watu mahakamani wakiwemo mawaziri - mambo magumu ambayo hayajawahi kufanywa na Rais yeyote. Vijembe vikapigwa kwamba waliokuwa kwenye (controversial) Kongamano wao nao walikuwa kwenye nafasi za uongozi mbona hawakuwahi kufanya hayo?! Prof. Mushi akasema hivi sasa demokrasia imepanuka sana kuliko huko nyuma, hayo ni mafanikio makubwa.... etc etc.

Conclusion ni kwamba Muungwana is just doing fine!
 
- Well, hoja zijibiwe kwa hoja sio viroja kama hawa wakuu, eti mnawaita ni opposition hawa? No wonder CCM itaendelea kushinda daima, I mean hawa kweli ni wenyeviti wa kuchaguliwa? Yaani na wao kama Kikwete, wameshindwa kujibu hoja za Butiku na Quaresi, badala yake wanajibu yale yale ya chuki na wivu kama Bibi Sophia!

- Unajua kwa mara ya kwanza nimeielewa case ya Chadema kukataa kujiunga na vyama vingine, hivi unawezaje kujiunga na vyama mufilisi namna hii? Hawa nao ni mafisadi hawa, hivi wamewahi kugombea nini katika taifa hili mbona hatujwahi kuwasikia? garademiti!

- Ujumbe wangu kwa Rais na washauri wako, acha kutumia hawa wachovu, nilijua huwezi kujibu kama ulivyoahidi sasa umeamua kutumia zile njia zako kama za kamati ya madini, it won't work, sasa do all of us wananchi a big favor, stand up as man kubali mapungufu yako kiuongozi, and then do something about it, au kama huwezi jiuzulu, waachie wengine, wapo wengi sana wanaoweza na usipoangalia very soon wananchi tutaamua bora shetani Lowassa! Kutumia wachovu katika jamii kujaribu kujisafisha kisiasa ina gharama zake kwa taifa, na moja ambayo ni mbaya kuliko zote ni kuigawa jamii katika makundi yanayopingana bila sababu, umeigawa CCM sasa unataka kuligawa taifa, please onea huruma watoto na wajukuu wetu, maana ukiendelea hivi hakitabaki kitu kwa taifa!

- Wakuu sio siri kwamba sasa huu ndio ule Mtandao, tayari umeanza kazi wanayoijua best ya kuchafua yoyote aliyeko kwenye njia yao, sasa ni vyema wananchi tukawa careful na kutokuangukia kwenye mitego yao, tujitahidi kuwa one step ahead huku tukiwaambia ukweli kwamba kama wameshindwa uongozi waondoke lakini hatuwezi kudanganywa kirahisi hivi, shame on you Kikwete na hizi very cheap politics!

Respect.

FMEs!
Maneno yako yamejaa hekima tupu. Haya mambo ya mtandao haya yanaharibu tu Taifa. Yamejaza watu kibao ndani ya nafasi za uongozi wasiojua wanachofanya.
Kweli JK hana mdomo wa kusema mpaka hawa jamaa waliojichokea waanze kumsemea? Sometimes I wonder who is the man/woman behind all these failing strategies? No doubt, these kind of strategies will fail whether its me implementing them or any other person because they don't hold any political truth,maturity or seriousness.
 
Guess what? Yangekwa madheebu mengine hususan Wakatoliki kelele zingekuwa nyingi wakina Makwaia wangeitisha midaalo ari mradi. Poor catholics!
 
Mkuu, viapo vyao vili-expire baada ya kuacha madaraka waliyokuwa nayo. Hivyo wana haki ya kutoa maoni yao kama mtu mwingine yeyote.

Kwa kweli sioni tatizo la mtu kusema mapungufu ya serikali na viongozi wake (kama yapo na anayaona). Haiwezekani kusubiri kusemewa wakati mambo yanaharibika. Vile vile, sidhani kama kilichosemwa na viongozi hao hakijawahi kusemwa na watu wengine katika mijadala ya kawaida. Ni mambo ambayo yamesemwa na wengi sana kabla ya kufika kwenye kongamano hilo. Tofauti iliyopo katika kauli hizo, ni nani aliyesema tu.

Nadhani ni vyema kusubiri kusikia hao wanaoandamana wanataka kutoa ujumbe gani.


Mkuu hapo naona limeeleweka ,waliosema ni wengi,ndio maana kwenye utaratibu wake wa kuongea na wananchi siku moja mh.Rais alisema kwamba wakubwa wajifunze kuongea mbele za wananchi maana kauli zao hazifanani na mtu wa kawaida.wazuie nguvu zao kuongea ikibidi wazielekeze kwenye mambo yenye tija.
 
JK wanataka kumsafisha, na huku Lowassa nae anahitaji kusafishwa....kaazi kweli, kweli. Wanajiachiaje mpaka wanachafuka hivo, kiasi cha kwamba iwe ni kazi ya watu wengine kuwasafisha?
Rais wetu sasa inabidi asuguliwe na JIKI ili awe squeaky clean
 
Inasikitisha kuona kumbe CCM ina nyama mjomba vya upinzani. Pamoja na hayo maandamano, jana on ITV, mama Shelukindo, Ole Sendeka na wengine walikua wanatetea JK. I just turned off the TV baada ya kusikia kwamba tusimulaumu, afanya maamuzi peke yake, ana washauri... Pumba. Kwani tulipigia kura washauri wake? Kwanza tunawajua?
Ninachofurahia ni mwamko tulionao. Leo hatudanganyiki
 
Wana JF, kabla ya kwenda mbali sana ni vyema tukawaangalia hawa watoa hoja. Kwanza ni wenyeviti wa vyama ambavyo havina wanachama.Pili wamechoka. Ingekuwa hoja huu imetolewa na vyama makini (Chadema, NCCR, TLP, n.k) ningeona sababu ya kuijadili.
 
Mpita Njia wa gazeti la Mtanzania la tarehe 4/12/2009 naye akasema yake kwenye kichwa cha habari "Mwalimu Nyerere Foundation!"

Kwa muda sasa Mpita Njia (MN) amekuwa akifuatilia kauli zinazotoka ndani ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere (Mwalimu Nyerere Foundation). Katibu Mtendaji wa MNF, Joseph Butiku amekuwa akishutumu uwapo wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mtu akimwangalia Butiku kwenye luninga wakati anapinga mitandao ndani ya vyama anaweza akasema Mungu weee, mtu si huyu! Kama ana ng'ombe au mwanambuzi anaweza kuuza ampelekee zawadi. Atamwona mzee huyu aliyepata fursa ya kufanyakazi karibu na Mwalimu Nyerere ni mkombozi wa kweli.

HUKU KUPANUKA KWA WIGO WA DEMOKRASIA NAONA KUNALETA MATATIZO KIDOGO. LUGHA ILIYOTUMIWA HAPA NA MPITA NJIA NI LUGHA YA KEJELI. BILA SHAKA MWANDISHI WA MAKALA HII YA MPITA NJIA ANAWEZA AKAWA NA UMRI MDOGO KULIKO HUYU MZEE ANAYEMBEZA KWA KEJELI. HUU NI MFANO DHAHIRI WA MMOMONYOKO WA MAADILI.

Lakini sikia. Kumbe mzee huyu ni chui aliyevaa ngozi ya kondoo. Inawezekana kama si hivyo, basi hajui maana halisi ya neno mtandao. MN anajiuliza hivi huyu mzee mwaka 2005 wakati anazunguka nchi nzima kumwombea kura Dk. Salim Ahmed Salim alikuwa anafanya nini?

Tena wapo wanaosema alizunguka kwa kutumia kasma ya Taasisi ya Mwalimu Nyeree. Hakuna asiyejua juhudi kubwa alizofanya kumwingiza madarakani Dk. Salim. Tena MN alikuwa akipita mahala akakuta Butiku akijadiliana na wakubwa wenzie nani anafaa kuwa Rais

Butiku alikuwa akizungumzia uzoefu, si ujuzi wala weledi, bali akisema anayefaa kuwa Rais wa nchi hii ni Dk. Salim, Hapa tunapoelekea ni uchaguzi wa mwakani. Butiku yeye alikuwa na matandao wake mwaka 2005, sasa hajatueleza kama aliuvunja au ulikufa wenyewe baada ya mtu wake kushindwa akaweweseka au vipi?

MIMI NI MSTAAFU NA NAIELEWA HISTORIA YA TAASISI YA MWALIMU NYERERE. NAELEWA HAYA YALIYOSEMWA HAPA NI UZUSHI WA WAZI KABISA.

TANGU MWALIMU NYERERE AKIWA BADO YU HAI, TAASISI YA MWALIMU NYERERE ILIKUWA NA ZOEZI LA KUTAFUTA MICHANGO KWA AJILI YA KUPATA FEDHA ZA KUENDESHA TAASISI. HAKUNA ASIYEELEWA KWAMBA MWALIMU ALIPOKUWA MADARAKANI HAKUTUMIA NAFASI YAKE YA UONGOZI KUJINUFAISHA WALA KUJILIMBIKIZIA MALI. KWA HIYO NI WAZI ALIPOTOKA MADARAKANI ALIKUWA HANA FEDHA ZOZOTE ZA KUWEZA KUANZISHA NA KUENDESHEA TAASISI. LAKINI, ALIAMINI KWA DHATI KABISA KWAMBA WANANCHI NA WATU WENGINE WENYE NIA NJEMA WANGELIWEZA KUICHANGIA TAASISI.

BAADA YA MWALIMU KUFARIKI DUNIA BADO TAASISI ILIKUWA BADO HAINA FEDHA ZA KUTOSHA KUWEZA KUJIENDESHA YENYEWE, KWA HIYO KAZI YA KUTAFUTA MICHANGO ILIENDELEA HADI MWAKA HUO WA 2005 BUTIKU ALIKUWA ANAENDELEA NA ZOEZI LA KUTAFUTA MICHANGO KUTOKA KWA WANANCHI. KADI ZA MAOMBI YA MICHANGO KWA AJILI YA TAASISI ZILIPELEKWA HADI KWENYE KATA KWA AJILI HIYO.

HATA HIVYO ZOEZI HILO LILISITISHWA NAAMINI KWA NIA NJEMA BAADA YA KUONEKANA LINAWEZA KUINGILIA MCHAKATO WA KUTAFUTA MGOMBEA URAIS.

INAVYOELEKEA WAZUSHI TAYARI WALIKUWA WAMEISHACHUKULIA ZOEZI HILO KAMA NI KAZI YA TAASISI KUMPIGIA DEBE ‘MGOMBEA' WAKE!

NINAWEZA KUSEMA KWA UHAKIKA KABISA NA BILA KUUMA MANENO KWAMBA KAMPENI ZA SALIM ZA KUTAFUTA KUCHAGULIWA KUWA MGOMBEA WA URAIS HAZIKUHUSIANA HATA KIDOGO AMA KWA NJIA YOYOTE ILE NA TAASISI YA MWALIMU NYERERE AMA UONGOZI WA TAASISI HIYO.

PENGINE KUTOKANA NA KUPOROMOKA KWA MAADILI WATU WANASHINDWA KABISA KUPAMBANUA NA KUELEWA UADILIFU WALIONAO BAADHI YA VIONGOZI WA SASA NA WALE WALIOKUWA VIONGOZI WA NCHI HII HUKO NYUMA. DK. SALIM KWA UADILIFU WAKE ASINGELIWEZA AKACHEZA MCHEZO MCHAFU WA KUITUMIA TAASISI KATIKA KAMPENI ZAKE. NA NAAMINI HATA NDUGU BUTIKU MWENYEWE ASINGELIKUBALI TAASISI ITUMIKE KWA AJILI HIYO.

KUTOKANA NA NILIYOYAELEZA HAPO JUU SI KWELI KWAMBA BUTIKU ALIKUWA NA MTANDAO KWA AJILI YA DK. SALIM. KWA HIYO SUALA LA YEYE KUUVUNJA MTANDAO HUO HALIPO! NI UZUSHI USIO NA MAANA YOYOTE.


Ila kubwa lililomsukuma MN kumgusa mzee huyu, ni tabia yake iliyoibuka. Tabia hii inakuwa na isipokemewa ataipeleka nchi pabaya. Mzee huyu ameamua kufumba macho ingawa hana upofu. Haelekei kusifia hata neno alilolitenda Rais Jakaya Kikwete.

KWA MIAKA YANGU NA KUPENDA KUSOMA HABARI NIMEKUWA MSOMAJI MZURI WA GAZETI LA MTANZANIA ENZI ZA JENERALI ULIMWENGU NA AKINA BWIRE WAKIWA PALE HABARI CORPORATION. KIBONZO CHA MPITA NJIA KILIKUWA KINAHABARISHA KINAELIMISHA NA KINAKOSOA KWA LUGHA YA KISTAARABU SANA NA KUWAHESHIMU WASOMAJI. INASIKITISHA SANA KUONA JINSI AMBAVYO MPITA NJIA HUYU WA SASA ANAVYOWEZA KUTUMIA LUGHA ISIYOHESHIMU WASOMAJI WAKE!

Anataka kuwaaminisha wananchi kuwa uongozi wa Rais Kikwete umeshindwa kazi. Kila kukicha anakaririwa akilalamika tu. Hawezi kumsifia Rais hata kwa hatua alizochukua kupanua wigo wa demokrasia nchini. Hata malalamiko anayotoa akaendelea kuishi uraiani bila kubughudhiwa anapaswa kufahamu kuwa ni kazi ya Rais Kikwete.

KUSEMA KWAMBA KILA KUKICHA BUTIKU ANALALAMIKA NA KUTAKA KUWAAMINISHA WANANCHI KUWA UONGOZI WA RAIS KIKWETE UMESHINDWA KAZI, NI UCHOCHEZI NA UCHONGANISHI USIO NA TIJA. HIVI HUYU BUTIKU YEYE HANA KAZI, KILA KUKICHA KAZI YAKE NI KULALAMIKIA UONGOZI WA RAIS KIKWETE? HAPA ANAYESTAHILI KUCHUKULIWA HATUA NA KUBUGHUDHIWA NI MWANDISHI WA MPITA NJIA KWA KUJARIBU KULETA UCHONGANISHI KATI YA WANANCHI NA RAIS/WANANCHI WENGINE.

Sasa Mzee huyu MN anampa ushauri wa bure. MN anamwambia kuwa haiwezekani hata siku moja wapiga kura wakaamka na kwenda kwenye vituo vya kura bila kushawihiwa wampigie nani kura. Si hilo tu, hata chama alichomo yeye kitendo cha yeye kukata kadi ya uanachama tayari ni mtandao.

HAYA PIA NI MANENO YA KEJELI NA DHARAU KWA WANANCHI KWAMBA WAO NI MAMBUMBUMBU HAWAJUI TOFAUTI KATI YA MTANDAO UNAOZUNGUMZIWA NA MTANDAO WA KICHAMA!

Ifahamike kuwa kama taifa hatuwezi kurejea kwenye enzi za ujima. Enzi ambazo si baba, mama wala au mtoto aliyejua ndugu kala nini, kalala wapi, hakukuwapo uchaguzi wala kugombea uongozi. Enzi hizo zilifutika. Ndiyo maana tuna vyama vya siasa. Vyama hivi ni mitandao.

HEY! UMEZALIWA LINI ‘MPITA NJIA' WA SIKU HIZI?! ENZI ZA UJIMA BABA, MAMA, MTOTO, MJOMBA, SHANGAZI, NDUGU WA KARIBU NA WA MBALI NA HATA JIRANI WALIJUANA VYEMA NA KILA MMOJA ALIJUA MWENZIWE KALA NINI NA KALALA WAPI. WENZETU WA KABILA LA WANYATURU NA WAGOGO TANGU ENZI ZA UJIMA WANA SALAMU YAO YA KILA ASUBUHI YA KUULIZANA 'UMEKULA NINI?! TOFAUTI NA ILIVYO SASA AMBAPO ‘MWENYE SHIBE HAMJUI MWENYE NJAA'!

MN anatakiwa kumwelimisha mzee huyu kuwa maana ya vyama ni kikundi cha watu waliokubaliana kiamwazo, kiitikadi na wana ajend ainayofanana kwa nia ya kuliletea taifa lake maendeleo. Kinachotokea sasa, wapo wenye kujiona kama si wana-mtandao, na hivyo u-CCM wao haukamiliki vizuri, hivyo lazima wasisemee hili. Si kweli!

HIVI KWELI MPITA NJIA YUKO SERIOUS ANAONA ANAO UBAVU WA KUMWELIMISHA MZEE BUTIKU MAANA YA VYAMA NI NINI? MATUNDA YA UTANUZI WA WIGO WA DEMOKRASIA NI MATAMU KWELI.

WATANZANIA TUMSHUKURU RAIS KIKWETE KWA KUPANUA WIGO WA DEMOKRASIA LAKINI ASLANI TUSIUTUMIE VIBAYA NA KUHATARISHA KILE TUNACHOKIFAIDI. TUPINGANE KWA HOJA LAKINI TUENDELEE KUISHI KWA UPENDO KAMA WATANZANIA, TUHESHIMIANE NA KUJENGA/KUENDELEZA MAADILI MEMA YA TAIFA LETU ILI TUWEZE KUENDELEA KUISHI KWA AMANI NA UTULIVU KWA MANUFAA YETU SASA NA MANUFAA YA VIZAZI VIJAVYO.

Bibi Ntilie/Mama Ntilie Mstaafu!
 
Bibie Ntilie,
Sishangai Mpita Njia anaandikia gazeti la Rostum. Kuganga njaa kubaya sana mama yangu!
 
Heshima kwako FMEsm

Nimependa andiko lako kwa kweli Muungwana kashikwa pabaya mbaya zaidi bado anafikiria Watanzanda ni mabwege.Kwa mara ya kwanza nadhani Muungwana anamuhitaji Ngoyai amsaidie kuweka mambo sawa,Ngoyai angekuwepo asingekubali hizi cheap propaganda kuwatumia kina Chipaka na maandamano ya waislam jumamosi ni makosa ya kuwa na timu ya watu wa hovyo

- Hizi mkuu ni dalili za kutudharau sisi wananchi wa taifa hili, kwamba this is all we deserve ili yeye kujisafisha, inasikitisha sana hata kusikia watu wa maana kama Mpita Njia nao wamo kwenye pay roll ya mtandao ni aibu sana!

Respect.


FMEs!
 
Chipaka ni mhaini aliyejaa mawazo ya kihaini na anafikiri kila mtu ni mhaini kama yeye! kwani uhaini wake ulifutika lini? baada ya kutoka gerezani?
 

Heshima kwako Mzee Punch,

Ni kweli hata mimi nimesikia kuna mpango kabambe wa kumsafisha Muungwana kabla ya uchaguzi mkuu mwakani tutasikia vimbwanga na vibweka kibao yetu macho.

Ukichunguza sana utagundua kitu kimoja watu au taasisi zinazojichomoza kumtetea Muungwana mara nyingi hawapendi kujibu hoja bali wanakimbilia kujadili watu na masula binafsi.Hoja zote zilizojadiliwa katika kongamano la Mwl Nyerere ni za kweli kuzijibu ni vigumu ndio maana Muungwana mpaka leo hajasema kitu anajaribu kuwatumia wanasiasa na taasisi za hovyo kuwaondoa watanzania katika masuala ya msingi.
Clever post!
 
Kuna haja na sisi wa upande mwingine kuanzisha maandamano ya kutoridhishwa na utendaji wa JK. Wanapaswa waanze kuona joto la jiwe hawa. Tatizo ni nani wa kutuongoza, wenzetu Zimbabwe wanae Morgan Tsvangirai, Kenya Odinga, SA walikuwa nao akina Steve Biko, Mzee Mbeki na Mandela. Sisi masikini hatuna mtu.

Nafikiri hapo ndio vyama vikubwa vya upinzani kama CHADEMA, CUF na NCCR wanatakiwa kuonyesha creativity and responsibility yao kwa wananchi, waorganize pia maandamano ya kuunga mkono yaliyosemwa na kupendekezwa kwenye hilo kongamano la Nyerere....kumbuka wana mass kubwa tu behind them.
 
Watakaoandamana wote siku hiyo wasife kabla ya kuonja maumivu ya ufisadi wa nchi hii!

This's just a wish, we need to do something, we need to act now! Hao unaowataka waonje maumivu walishaonja tayari for sure, it's time to make changes, and changes is all down to our own decision! If you read my signature you'll understand what I mean.
 
Mkuu kuichambua si kosa ila kuweka matusi ni tatizo hapo.kwa uchambuzi wa Tadea na wengine binafsi nauukubali,kwani kufanya hivyo ni kuatarisha amani ya nchi.kwa viongozi wakuu wastaafu kuikosoa serikali kwa njia kama ile ni hatari sana.wao naamini wananjia nzuri tu ya kupeleka mawazo kwa serikali iliyopo madarakani.

wamekiuka miiko na viapo walivyokula wakati wanahika nyadhifa zao.

Bravo TADEA NA WENZIO
Mmmh! Sound like a puppet!
 
TADEA na UPDP wamechanganyikiwa. Kukosoa Serikali kwa mapungufu yake, hasa yaliyo dhahiri ni kupenda nchi yako, sio uhaini. Ni uzalendo. Hata Rais Kikwete mwenyewe amekubali kuwa hakutegemea hawa viongozi wamsifu.

Labda Chipaka wa TADEA na mwenzake Dovutwa wa UPDP wanadhani Kikwete anaweza kufikiria vyama vyao na kuvisaidia vikue, badala ya kudumaa. Hivi ni vyama vya Dar es Salaam tu, na havionekani mikoani. Waende mikoani, badala ya kukaa Dar kuita mikutano na waandishi wa habari na kushiriki ktk maandamano yasiyokuwa na tija.

Ni dhahiri kwamba CCM kama Mwalimu Julius Nyerere alivyoiasisi mwaka wa 1977 ni tofauti sana na hii inayoongozwa na Kikwete na Makamba. Kukumbatia mafisadi au kutowachukulia hatua za haraka za kisheria hakuwezi kufumbiwa macho na wazalendo kama Butiku na Mawaziri wastaafu kama wale waliohudhuria Kongamano la MNF.

Kinachotakiwa kufanywa na hawa viongozi wazalendo na jasiri ni kujitoa katika chama kinachoonyesha kinakumbatia mafisadi, na kuungana na chama chenye mwelekeo wa kushughulikia janga hili linalolikumba taifa letu la Tanzania sasa. Hata Mwalimu Nyerere mwenyewe alitamka kwamba CCM sio mama yake, na kwamba angeweza kuiacha kama haitekelezi matakwa ya Watanzania kama alivyoyajua.

Sasa kuna vyama vingi vya siasa na ni vizuri viimarishwe na vitoe changamoto kwa CCM ili ijirekebishe, la sivyo iondolewe madarakani kwa kunyimwa kura wakati wa Uchaguzi Mkuu mwakani. Huo ndio ujumbe kutoka Kongamano la MNF.
 
Back
Top Bottom