Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,919
- 31,161
VYAMA vya The Tanzania Democratic Alliance (Tadea) na United Peoples Democratic (UPDP), vimeeleza kushangazwa kwa kutochukuliwa hatua kwa viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, akiwamo Mkurugenzi Mtendaji wake, Joseph Butiku, kwa madai wametenda kosa la jinai na uhaini kwa kumtusi Rais Jakaya Kikwete.
Wakitoa tamko lao mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa Tadea, John Chipaka na Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa, walisema kuwa viongozi hao wa taasisi hiyo wakiwemo mawaziri wakuu wastaafu na mawaziri wengine waliohudhuria kongamano la kujadili mustakabali wa nchi katika kumbukumbu ya miaka 10 baada ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere ,waliligeuza kongamano hilo kuwa la kutukana watu, uchochezi na kujitangaza kugombea na kungangania madaraka.
iweje leo viongozi hao wakutane na kuchochea chuki ya waziwazi hadharani ili wananchi waichukie na kuikasirikia serikali pamoja na kiongozi wa nchi, eti hawezi kuongoza kwa vile dhaifu isipokuwa wao tu wanaweza, ni aibu, huu ulikuwa uhaini kamili.
Viongozi na wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere isipokuwa Butiku, wote ni mawaziri wakuu wastaafu na mawaziri, wamekosea kuonyesha misimamo yao katika warsha hiyo na kumchafua kwa matusi Rais Kikwete, jambo ambalo si sahihi, tunashangaa kwa nini hawakukamatwa na kushitakiwa kwa makosa ya jinai na uhaini, kesi ambazo huvuta adhabu kali na kubwa, walisema bila kutaja majina ya viongozi hao.
Wakimchambua Butiku, walidai kiongozi huyo hana uwezo kikazi na alishindwa kutekeleza kazi alizopewa wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.
Alipokuwa Katibu Myeka wa Mwalimu Nyerere alitingisha Ikulu na alikuwa na mamlaka ya kutoa vibali kwenda vijijini na mitaani akiamuru anachotaka.
Butiku anadaiwa baada ya Mwalimu Nyerere kungatuka kwenye madaraka, yeye hakuwa tayari kuondoka Ikulu na tamko hilo kuongeza,
sina hakika kama aliachia nyumba ya serikali na aliendelea kuishi bila kulipa pango na hata alisahau kustaafu kwenye Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Maoni ya Butiku ni ya mashaka kwani haamini kama kuna wananchi wengine wanaweza kuwa na uwezo kuliko yeye ndiyo maana analilia madaraka.
Viongozi hao walisema kuwa Rais Kikwete ni kiongozi bora na muwazi ambaye kwa hulka na tabia yake, hawezi kuharibu sifa yake kwa kuwafuata viongozi hao wanaotaka awarithi tabia zao za ukandamizaji. Rais Kikwete ametajwa kutekeleza ilani ya CCM na kuimarisha uhuru na ujenzi wa demokrasia endelevu.
Walisema wakati wa utawala wa Rais Kikwete wananchi wamepewa uhuru wa kutoa maoni yao na kujinafasi huku mwenyewe akifuatilia maendeleo kwa makini na hakuna vitisho kama ilivyo siku za nyuma.
Bila kutaja majina, walisema kutokana na viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuutangazia umma kuwa CCM imepoteza dira ni vema wakaondoka kwenye chama hicho na kujiunga kwenye vyama vingine au kuunda chama chao ambapo wasisitiza :
Inaonekana viongozi na wadhamini wa taasisi hiyo hawana maono na hawataki kukubali kila zama ina kitabu chake na nchi haiwezi kunganganizwa zama za ujamaa wakati nchi nyingine zinaendeshwa kwa uchumi huria.
Walisema nia ya kuwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere haikuwa kuunda taasisi ya kugombea na kungangania madaraka au taasisi korokoroni wa siasa za CCM kama chama cha siasa mbadala, bali iliundwa kufanya utafiti wa mambo mbalimbali kama ya siasa na kuwa kiongozi wa maadili mema ya kisiasa.
Wakati wa kongamano hilo baadhi ya viongozi wastaafu, wakiwemo mawaziri na wakuu wa mikoa na wanasiasa walimnyooshea vidole Rais Kikwete kuwa uongozi wake dhaifu na aachie madaraka.
Hata hivyo Rais Kikwete ambaye wakati tuhuma dhidi yake zinatolewa hakuwepo nchini, aliporejea alisema hashangai kukosolewa na viongozi hao wastaafu, bali angeshangaa kusifiwa nao.
Kauli za viongozi hao dhidi ya Rais Kikwete pia zilipingwa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, aliyesema viongozi hao wakati wa uchaguzi walikuwa katika kundi la mgombea aliyekuwa akichuana na Rais Kikwete na hawajafurahishwa mgombea wao kushindwa hivyo kuendeleza chuki.
Alisema Rais Kikwete anapendwa zaidi na wananchi kuliko hata CCM yenyewe hivyo atasimamishwa tena kugombea urais mwakani.
Butiku alipotafutwa kujibu madai ya viongozi hao wa UPDP na Tadea alijibu kwa njia ya simu, nikukatishe kauli mwandishi, mimi sitaki kuzungumza kitu maneno yangu yaliisha kwenye kongamano, mengine sitaki, alisema na kukata simu.
Chanzo: HabariLeo
Duh mpaka uchaguzi mkuu utakapofika mwaka 2010 tutaona mengi,nashindwa kuelewa hawa jamaa nani kawatuma.
Ikifika mahali kujadili mapungufu ya serekali iliyoko madarakani unaitwa mhaini basi inabidi tusifie hata udhaifu uliowazi.
Wakitoa tamko lao mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa Tadea, John Chipaka na Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa, walisema kuwa viongozi hao wa taasisi hiyo wakiwemo mawaziri wakuu wastaafu na mawaziri wengine waliohudhuria kongamano la kujadili mustakabali wa nchi katika kumbukumbu ya miaka 10 baada ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere ,waliligeuza kongamano hilo kuwa la kutukana watu, uchochezi na kujitangaza kugombea na kungangania madaraka.
iweje leo viongozi hao wakutane na kuchochea chuki ya waziwazi hadharani ili wananchi waichukie na kuikasirikia serikali pamoja na kiongozi wa nchi, eti hawezi kuongoza kwa vile dhaifu isipokuwa wao tu wanaweza, ni aibu, huu ulikuwa uhaini kamili.
Viongozi na wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere isipokuwa Butiku, wote ni mawaziri wakuu wastaafu na mawaziri, wamekosea kuonyesha misimamo yao katika warsha hiyo na kumchafua kwa matusi Rais Kikwete, jambo ambalo si sahihi, tunashangaa kwa nini hawakukamatwa na kushitakiwa kwa makosa ya jinai na uhaini, kesi ambazo huvuta adhabu kali na kubwa, walisema bila kutaja majina ya viongozi hao.
Wakimchambua Butiku, walidai kiongozi huyo hana uwezo kikazi na alishindwa kutekeleza kazi alizopewa wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.
Alipokuwa Katibu Myeka wa Mwalimu Nyerere alitingisha Ikulu na alikuwa na mamlaka ya kutoa vibali kwenda vijijini na mitaani akiamuru anachotaka.
Butiku anadaiwa baada ya Mwalimu Nyerere kungatuka kwenye madaraka, yeye hakuwa tayari kuondoka Ikulu na tamko hilo kuongeza,
sina hakika kama aliachia nyumba ya serikali na aliendelea kuishi bila kulipa pango na hata alisahau kustaafu kwenye Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Maoni ya Butiku ni ya mashaka kwani haamini kama kuna wananchi wengine wanaweza kuwa na uwezo kuliko yeye ndiyo maana analilia madaraka.
Viongozi hao walisema kuwa Rais Kikwete ni kiongozi bora na muwazi ambaye kwa hulka na tabia yake, hawezi kuharibu sifa yake kwa kuwafuata viongozi hao wanaotaka awarithi tabia zao za ukandamizaji. Rais Kikwete ametajwa kutekeleza ilani ya CCM na kuimarisha uhuru na ujenzi wa demokrasia endelevu.
Walisema wakati wa utawala wa Rais Kikwete wananchi wamepewa uhuru wa kutoa maoni yao na kujinafasi huku mwenyewe akifuatilia maendeleo kwa makini na hakuna vitisho kama ilivyo siku za nyuma.
Bila kutaja majina, walisema kutokana na viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuutangazia umma kuwa CCM imepoteza dira ni vema wakaondoka kwenye chama hicho na kujiunga kwenye vyama vingine au kuunda chama chao ambapo wasisitiza :
Inaonekana viongozi na wadhamini wa taasisi hiyo hawana maono na hawataki kukubali kila zama ina kitabu chake na nchi haiwezi kunganganizwa zama za ujamaa wakati nchi nyingine zinaendeshwa kwa uchumi huria.
Walisema nia ya kuwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere haikuwa kuunda taasisi ya kugombea na kungangania madaraka au taasisi korokoroni wa siasa za CCM kama chama cha siasa mbadala, bali iliundwa kufanya utafiti wa mambo mbalimbali kama ya siasa na kuwa kiongozi wa maadili mema ya kisiasa.
Wakati wa kongamano hilo baadhi ya viongozi wastaafu, wakiwemo mawaziri na wakuu wa mikoa na wanasiasa walimnyooshea vidole Rais Kikwete kuwa uongozi wake dhaifu na aachie madaraka.
Hata hivyo Rais Kikwete ambaye wakati tuhuma dhidi yake zinatolewa hakuwepo nchini, aliporejea alisema hashangai kukosolewa na viongozi hao wastaafu, bali angeshangaa kusifiwa nao.
Kauli za viongozi hao dhidi ya Rais Kikwete pia zilipingwa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, aliyesema viongozi hao wakati wa uchaguzi walikuwa katika kundi la mgombea aliyekuwa akichuana na Rais Kikwete na hawajafurahishwa mgombea wao kushindwa hivyo kuendeleza chuki.
Alisema Rais Kikwete anapendwa zaidi na wananchi kuliko hata CCM yenyewe hivyo atasimamishwa tena kugombea urais mwakani.
Butiku alipotafutwa kujibu madai ya viongozi hao wa UPDP na Tadea alijibu kwa njia ya simu, nikukatishe kauli mwandishi, mimi sitaki kuzungumza kitu maneno yangu yaliisha kwenye kongamano, mengine sitaki, alisema na kukata simu.
Chanzo: HabariLeo
Duh mpaka uchaguzi mkuu utakapofika mwaka 2010 tutaona mengi,nashindwa kuelewa hawa jamaa nani kawatuma.
Ikifika mahali kujadili mapungufu ya serekali iliyoko madarakani unaitwa mhaini basi inabidi tusifie hata udhaifu uliowazi.