Bus zuri Dar to Arusha

Wasikutishe mkuu, hotel kwa elf 50 zipo tena nzuri tu. Fikia hata Atlanta hotel, kuna rooms had 50
 
Hilo Tahmeed zilikuwa vifuso mpaka juzi tu.?
Nayachukia kupita maelezo hata nauli ingenkuwa dala na ndani unapata pilao sipandi.
Lenyewe likiwa ccm mi ntakuwa ukawa, likiwa ukawa mi ntakuwa ccm tusikutane sehemu moja.
Hizo chuki zote zimetokana na nini mkuu?
 
Sio chuki ila ni hasira mtu anapipotosha kitu unachokijua vizuri na kuona watu wanaelekea kumwamini.
 
Kidia
Happy Nation
Dar express
Kakore
Tahmeed,
Kilimanjaro Express

Chukua Tahmeed au ukichelewa chukua Kilimanjaro ila Tahmeed mimi nimesafiri nao kutoka Arusha to Dar wako vizuri ndani kuna mpaka choo cha dharura.
 
Kwa Hotel
Usijidanganye na hiyo pesa labda ukalale Lexus pale Njiro ila kwa hotel waweza enda Joshmal ndo ni 50,per day
Nimeambiwa kuna Victoria, Miami, Briston, naweza kupata kwa bei hiyo hadi 45,000 tena double. Unaifahamu Briston Hotel?
 
Motel 2000 ipo sakina ,35,000 tu. Unaweza Google uuone mandhari . Nimewahi lala hapo pazuri kwa Bei hiyo
 
Nilisafiri kwenda Arusha juzi kati pale nikapanda libasi fulani hivi tingatinga(jina silitaji nisije onekana nina majungu) wale jamaa wapiga debe wakalipamba lile tingatinga nikawapa nauli 25,000! mbaya zaidi ndio ilikua mara ya kwanza kwenda huko!

Niliichukia ile safari aisee! masiti yenyewe ni 2*3 huku vitoto vinalia!! gari ni kuukuu! nilikaa dirishani siti ya watu 3 kero tupu mara huyu anataka nimuitie wa korosho! mara huyu hivi! Next time siji kurudia ule ujinga. Mabasi ya kupanda nimeshayajua sasa watanikoma.
 
Asanteni sana wakuu kwa taarifa mbalimbali mlizonipatia. Nilisafiri na Bus la Kilimanjaro, ni semi-luxury halina hata AC kumbe ila mwendo wao ni mzuri na uendeshaji wao ni mzuri.
Na hoteli nilipata inaitwa Briston iko karibu na mnara wa Azimio la Arusha ni mpya na bei ni 40,000. Pazuri sana.
 
Back
Top Bottom