Buriani Mhe. Komba wa 'Joka la kufugwa'

Buriani Mhe. Komba wa 'Joka la kufugwa'

Ushabiki wa kisiasa usikupeleke kwenye kukufuru.Kila nafsi iliyozaliwa itaonja umauti hakuna atakaepaa.Capt John Komba alikuwa mwanasiasa wa kawaida ndani ya CCM akiwatumikia vyema wananchi wa jimbo la Mbinga Magharibi katika siasa za kawaida za kidemokrasia sasa kinachofanya wewe na majuha wenzako mushangilie nini?

Sababu ni kwamba amekufa Komba, Warioba yuko hai.
 
Nitaendelea kumuenzi daima kwa kauli yake ya kutaka mlango wa bunge ufungwe ili apigane, nafikiri lengo lake kuu lilikuwa ni kuuwa wenzie cha ajabu kaanza yeye. Nitamkumbuka kwa kipaji chake kizuri cha kutabiri kifo chake kwa kusema ataingia msituni, naamini kama angeingia msituni tusingemuona tena pengine angeshambuliwa na wanyama wakali na kupoteza maisha hivyo isingekuwa tofauti na huu msitu alioingia sasa hivi "MSITU WA MILELE". Nitamuenzi sana kwani kila nikimkumbuka napata pia nafasi ya kumkumbuka msanii mwenzie marehemu Kanumba bila kumsahau Lulu.
 
Ushabiki wa kisiasa usikupeleke kwenye kukufuru.Kila nafsi iliyozaliwa itaonja umauti hakuna atakaepaa.Capt John Komba alikuwa mwanasiasa wa kawaida ndani ya CCM akiwatumikia vyema wananchi wa jimbo la Mbinga Magharibi katika siasa za kawaida za kidemokrasia sasa kinachofanya wewe na majuha wenzako mushangilie nini?

Nakuambia hivi huyo muhuni mmoja alimzohaki Mzee Warioba kesha potea..

Sasa kama na wewe ulishiriki kumtukana Warioba andaa mahali pa kuzikwa..
 
Hawa ndio zao la uongozi wa Mbowe na Dr Slaa.Sina shaka kama viongozi wao wana fikra zinazofanana.

tulia we hao sis tunataka ukomboz na moja kat ya vikwazo vinaondoka kwa kasi acha tufurah nawe pia utafurah na sie pindi fikra za utumwa zikikutoka
 
Heading ingekuwa: Captain Komba JOKA la kufugwa!
1. Ukifuga Joka UTALIFUNDISHA namna na mambo ya kufanya. Mtu huimba anachoambiwa kuimba. Tofauti ipo katika wanaomwambia aimbe nini. Komba wa wakati wa Nyerere aliimba vitu vya maana kuliko Komba wa wakati wa Kikwete. Zamani aliimba na kusifia Uzalendo wa Dhati ulioakisiwa kwenye siasa ya Nchi. Wa zama hizi ameimba na kupiga soga (Bungeni) akiakisi alichoambiwa na CCM.
2. Komba wa mwaka 1979 hakuwa na KITAMBI, wa sasa ametwaliwa akiwa na KITAMBI (ishara ya UBWANYENYE na UBEPARI) aliouchukia na kuuimba vibaya enzi za Mwalimu Nyerere.
3. Twasikitika. Komba wa kwanza ALISHAKUFA zamani na kwa kweli KILA KONA ya NCHI ilisikitika. Komba aliyekufa sasa anasikitikiwa na kule ALIKOACHA pengo!
Tangulia John... Tangulia.....Madelu anakulilia. Nepi inakulilia.....CCM inakulilia...
 
Upumzike kwa Amani Captain Komba... Uwasamehe wote wanaotumia kifo chako kukuhukumu kwa kejeli bila kujali maumivu familia yako inayopata... ulikua mwanasiasa ambae kama mwanasiasa mwingine yoyote ulitetea upande wako...Tanzania itakukumbuka daima
 
Komba ametutoka lakini mazuri au mabaya aliotenda yatadumu milele.Lakini kama Komba alikuwa shujaa huko nyuma kitu gani kilimbadirisha kuwa hivi?Labda maradhi ndio tatizo kuwa alitenda bila kujua?
 
biblia inasema chumvi ikisha chacha itiwe nini hata iweze kukolea????? pia ikaongeza kuwa mema yako elfu moja yatafutwa kwa baya lako moja haikuishia hapo ikasema kuwa chachu kidogo huchachua donge zima
 
Nakuambia hivi huyo muhuni mmoja alimzohaki Mzee Warioba kesha potea..

Sasa kama na wewe ulishiriki kumtukana Warioba andaa mahali pa kuzikwa..


Hii ndio Think tank ya Chadema.. Mnaojua kutukana tu.
 
Tuna imani roho yake haijafa... ndo mana kuna mambo ya laana za marehemu etc... all in all ni vibaya sana kumkejeli na kumdharau mtu aliyekufa

Hiyo laana ya marehemu ni imani yako,Hakunaga hiyo kitu!!!
 
Back
Top Bottom