Nyakarungu
JF-Expert Member
- May 1, 2011
- 472
- 377
BURIANI MH. KOMBA WA JOKA LA KUFUGWA .
Mwaka mmoja kabla ya mimi kuzaliwa 1979, kuna tukio kubwa sana lilitokea katika nchi yetu chini ya uongozi wa Rais wa awamu ya kwanza ‘Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere,
Wakati huo aliyekuwa Rais wa nchi ya Uganda General Idd Amin Dadaa aliichokoza nchi yetu, pamoja na uchokozi huo aliokuwa ameuanza muda mrefu sana lakini Rais wetu alivumilia sana mpaka ilipolazimu Rais wetu kutangaza vita iliyopelekea mapambano kati ya majeshi ya nchi ya Uganda na Tanzania, hata hivyo ni jambo la kumshukuru Mungu kwani katika vita ile Idd Amin alipigwa na nchi yetu kuchukua ushindi.
Vijana wetu wa Tanzania walipigana kiume na kwa ari ya kuhakikisha wanatimiza adhima ya kuilinda nchi yetu dhidi ya uvamizi wa Idd Amin,
Nyuma ya ari na moto waliokuwa nao vijana wetu wanajeshi, kulikuwa na uadilifu na uzalendo mkubwa sana uliopikika ndani ya mioyo yao, hali hii ilichagizwa pia na hamasa walizopewa jeshini wakati wa maandalizi ya kwenda vitani (katika nchi zote au katika makundi yote wanapojiandaa na vita, huwepo hali ya kutumia sanaa na namna ya sanaa yoyote ile kuwapa ari na moto wanajeshi kabla ya kwenda vitani)
Nakumbuka nikiwa na umri wa miaka 11 nikiwa nyumbani kwetu nikilelewa na wazazi wangu, wakati Baba akiwa kiongozi wa kata akitumikia umma kama katibu wa kata, alikuwa akisafiri kwenda umbali wa km 5 katika ofsi yake kwa kutumia baiskeli aina ya phonex, mara zote alichelewa kurudi nyumbani na alifika mida ya saa 2-3 usiku akiwa amechoka na safari hiyo,
Lakini tukiwa familia yenye watoto kadhaa, tulimngoja baba mpaka afike nyumbani usiku ule hivyo mara zote tulikusanyika kwenye nyumba iliyokuwa ikitumika kama jiko tukingojea chakula kipikwe huku tukingojea kusikia sauti ya mbwa wakibweka tukotke nje kumpokea baba kwani tuliamini yeye anapofika mbwa watabweka lakini watatoa sauti za kuashiria furaha ya mtu mtu wanaemfahamu.
Wakati wote huo tukiwa ndani ya jiko mama akipika au akichochea moto jikoni, dada yangu mkubwa Grace na kaka yangu mkubwa Zachayo walikuwa wataalamu wa kunogesha hadithi za shuleni kwao au habari za hapa na pale.
Nakumbuka siku moja nikiwa nimesimama ndani ya jiko nikitazama kwa makini ukali wa moto uliokuwa ukipika mahindi na viazi vitamu huku nikiwa nimeshikiria nguzo iliyokuwa imeshikiria ile nyumba yetu ya nyasi (ambero) kuna wimbo ulisikika ukiimbwa na Marehemu komba radioni wakati huo tulikuwa na radio aina ya mkulima na tulizoea kusikiliza mchezo wa radio ulioitwa chibuku "jangara" ule wimbo uliposikika dada akamuuliza mama, je huyu anaeimba ndiye alikuwa akiimba kipindi kile mjomba Ramadhani a.k.a anko mandevu a.k.a Osama alikuwa anaenda vitani? Mama alijibu ndio, huyu ni mwimbaji wa hizo nyimbo za vita anaitwa komba mtu wa jeshini ni mwanajeshi kabisa na alienda vitani,
Mjomba wetu alipigana ile vita akiwa mstari wa mbele, wakati wa maandalizi ya vita familia ilitega sikio kila mara radioni kwa sababu ya kutaka kujua kinachoendelea ikizingatiwa ndugu yetu alikuwa miongoni mwa wanavita wale,
Hivyo nyimbo zilizotumika kuhamasisha watanzania wajiamini na kulipa jeshi mori na ari zilikuwa zikipigwa kila wakati hivyo baadhi ya watu waliweza kuzikariri,
Siku hiyo Kaka, Dada na Mama waliozisikia nyimbo zilizotungwa na kuimbwa na marehemu komba walianza kuimba kipande huku wakieleza walivyokuwa na wasiwasi juu ya mjomba wetu ambae hata hivyo alirejea akiwa mzima.
Chorus ile ilinivutia ukizingatia nilikuwa na kipaji cha kuimba na kukariri kwa haraka na ndio siku nilipojua jina la mwanajeshi aliyeimba wimbo uliotumika kuwatia moyo wananchi na kuwapa ujasiri na mori wanajeshi.
WALIIMBA….
Tanzania kumezuka…..
Na joka kubwa la kufugwa ni lazima tuliponde life…
Idd Amin Dadaa ni joka kubwa la kufugwa ni lazima tuliponde life….
KOMBA WA JOKA LA KUFUGWA AMETANGULIA, MWIMBAJI NA MTUNZI MAHIRI
Kwa bahati moja au nyingine Baba alirejea na tukatoka kumpokea na hiyo ikiwa mwisho wa stori ile mpaka nilipokuwa mkubwa kiitikio hiki kimekuwa kikiimba kichwani.
Lakini jana baada ya kupata habari za kifo chake nilimpigia mama simu na kumpa taarifa hiyo iliyomsikitisha na kwa bahati nzuri wimbo huo ameniambia anaukmbuka wote, naahidi kuupata.
Je tuna nini cha kujivunia kwa shujaa komba kama sio kukumbuka kazi kubwa aloifanya kwa taifa wakati muhimu kama ule wa vita?
Nawaombea wanafamilia wote Mungu awape nguvu tunawaombea.
Mwaka mmoja kabla ya mimi kuzaliwa 1979, kuna tukio kubwa sana lilitokea katika nchi yetu chini ya uongozi wa Rais wa awamu ya kwanza ‘Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere,
Wakati huo aliyekuwa Rais wa nchi ya Uganda General Idd Amin Dadaa aliichokoza nchi yetu, pamoja na uchokozi huo aliokuwa ameuanza muda mrefu sana lakini Rais wetu alivumilia sana mpaka ilipolazimu Rais wetu kutangaza vita iliyopelekea mapambano kati ya majeshi ya nchi ya Uganda na Tanzania, hata hivyo ni jambo la kumshukuru Mungu kwani katika vita ile Idd Amin alipigwa na nchi yetu kuchukua ushindi.
Vijana wetu wa Tanzania walipigana kiume na kwa ari ya kuhakikisha wanatimiza adhima ya kuilinda nchi yetu dhidi ya uvamizi wa Idd Amin,
Nyuma ya ari na moto waliokuwa nao vijana wetu wanajeshi, kulikuwa na uadilifu na uzalendo mkubwa sana uliopikika ndani ya mioyo yao, hali hii ilichagizwa pia na hamasa walizopewa jeshini wakati wa maandalizi ya kwenda vitani (katika nchi zote au katika makundi yote wanapojiandaa na vita, huwepo hali ya kutumia sanaa na namna ya sanaa yoyote ile kuwapa ari na moto wanajeshi kabla ya kwenda vitani)
Nakumbuka nikiwa na umri wa miaka 11 nikiwa nyumbani kwetu nikilelewa na wazazi wangu, wakati Baba akiwa kiongozi wa kata akitumikia umma kama katibu wa kata, alikuwa akisafiri kwenda umbali wa km 5 katika ofsi yake kwa kutumia baiskeli aina ya phonex, mara zote alichelewa kurudi nyumbani na alifika mida ya saa 2-3 usiku akiwa amechoka na safari hiyo,
Lakini tukiwa familia yenye watoto kadhaa, tulimngoja baba mpaka afike nyumbani usiku ule hivyo mara zote tulikusanyika kwenye nyumba iliyokuwa ikitumika kama jiko tukingojea chakula kipikwe huku tukingojea kusikia sauti ya mbwa wakibweka tukotke nje kumpokea baba kwani tuliamini yeye anapofika mbwa watabweka lakini watatoa sauti za kuashiria furaha ya mtu mtu wanaemfahamu.
Wakati wote huo tukiwa ndani ya jiko mama akipika au akichochea moto jikoni, dada yangu mkubwa Grace na kaka yangu mkubwa Zachayo walikuwa wataalamu wa kunogesha hadithi za shuleni kwao au habari za hapa na pale.
Nakumbuka siku moja nikiwa nimesimama ndani ya jiko nikitazama kwa makini ukali wa moto uliokuwa ukipika mahindi na viazi vitamu huku nikiwa nimeshikiria nguzo iliyokuwa imeshikiria ile nyumba yetu ya nyasi (ambero) kuna wimbo ulisikika ukiimbwa na Marehemu komba radioni wakati huo tulikuwa na radio aina ya mkulima na tulizoea kusikiliza mchezo wa radio ulioitwa chibuku "jangara" ule wimbo uliposikika dada akamuuliza mama, je huyu anaeimba ndiye alikuwa akiimba kipindi kile mjomba Ramadhani a.k.a anko mandevu a.k.a Osama alikuwa anaenda vitani? Mama alijibu ndio, huyu ni mwimbaji wa hizo nyimbo za vita anaitwa komba mtu wa jeshini ni mwanajeshi kabisa na alienda vitani,
Mjomba wetu alipigana ile vita akiwa mstari wa mbele, wakati wa maandalizi ya vita familia ilitega sikio kila mara radioni kwa sababu ya kutaka kujua kinachoendelea ikizingatiwa ndugu yetu alikuwa miongoni mwa wanavita wale,
Hivyo nyimbo zilizotumika kuhamasisha watanzania wajiamini na kulipa jeshi mori na ari zilikuwa zikipigwa kila wakati hivyo baadhi ya watu waliweza kuzikariri,
Siku hiyo Kaka, Dada na Mama waliozisikia nyimbo zilizotungwa na kuimbwa na marehemu komba walianza kuimba kipande huku wakieleza walivyokuwa na wasiwasi juu ya mjomba wetu ambae hata hivyo alirejea akiwa mzima.
Chorus ile ilinivutia ukizingatia nilikuwa na kipaji cha kuimba na kukariri kwa haraka na ndio siku nilipojua jina la mwanajeshi aliyeimba wimbo uliotumika kuwatia moyo wananchi na kuwapa ujasiri na mori wanajeshi.
WALIIMBA….
Tanzania kumezuka…..
Na joka kubwa la kufugwa ni lazima tuliponde life…
Idd Amin Dadaa ni joka kubwa la kufugwa ni lazima tuliponde life….
KOMBA WA JOKA LA KUFUGWA AMETANGULIA, MWIMBAJI NA MTUNZI MAHIRI
Kwa bahati moja au nyingine Baba alirejea na tukatoka kumpokea na hiyo ikiwa mwisho wa stori ile mpaka nilipokuwa mkubwa kiitikio hiki kimekuwa kikiimba kichwani.
Lakini jana baada ya kupata habari za kifo chake nilimpigia mama simu na kumpa taarifa hiyo iliyomsikitisha na kwa bahati nzuri wimbo huo ameniambia anaukmbuka wote, naahidi kuupata.
Je tuna nini cha kujivunia kwa shujaa komba kama sio kukumbuka kazi kubwa aloifanya kwa taifa wakati muhimu kama ule wa vita?
Nawaombea wanafamilia wote Mungu awape nguvu tunawaombea.