Bunju-Posta Metro Line

Bunju-Posta Metro Line

Wazo zuri sana, tatizo itakuwa pesa na wahusika kutusikiliza...
 
Cost wise kati ya Metro line na hii Rapid transit ipi ipo chini!?..
Tuchukulie mfano tu wa treni ya Posta-Pugu/Posta-ubungo zinavyojaza watu pamoja na behewa zote zile then pigia picha itabidi vijengwe vituo vingapi kuziaccomodate hizo metro line trains!.
Lets be serious kwa sasa Mwendokasi ni suluhu ya tatizo letu tukiangalia toka ujenzi wake, uendeshaji wake, utunzaji wake na uwezo kuhimili unforeseen events!.
Kilichohitajika ni kuongeza mabasi tu sio kuanza kujenga hayo matreni ya juu ambayo kwanza ni gharama pili hatutaweza yaendesha kwa kipindi kirefu halafu matengenezo yake ni makubwa zaidi!..
Tunaweza piga kelele zijengwe hata Maglev trains lakini nauli ya Posta-Tegeta ikiwa elfu 15 tusianze kelele, hakuna mradi unaojengwa bila angalia gharama za kuuendesha na payback period yake!..
Jiji la Dar es salaam lliifanyiwa utafiti wa kina na wataalamu kutoka south america walilipwa na world bank kama sijakosea. Report yao iliongelea options zote mpaka hii ya mleta mada, BRT ili onekana itafaa zaidi. Kama mtu anaweza weka ile report itakua safi,
ilichambua vizuri sana hizo options.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kwa nini sisi tunakuwa tunajificha kwenye Kichaka cha kutokuwa na Uwezo!???
Hivu Kuwa/Kutokuwa na Uwezo maana yake ni ninu?
Kuna mambo mengi sana madogo zaidi ya hilo yanatushinda
 
Badala ya mwendokasi kwanini tusiweke Metro line kutoka Bunju Hadi Posta? Hii inawezekana kupita juu Kwa juu katikati ya barabara bila kuathiri magari ya kawaida. Train za umeme full automated bila dereva zitatumika. Station zinakuwa juu huko huko abiria wanapanda na kushuka kwa kidaraja juu ya barabara. Treni moja ni Sawa na mabasi ya mwendokasi manne au matano hivyo zinaweza kubeba watu 500-600 Kwa mara moja. Mfano wake ni hapo chini. Picha ya tatu ni stationView attachment 984917View attachment 984918View attachment 984919

Dubai Metro,one of the best transport systems in th world.Safi,Timely and well maintained.imesaidia sana movements za watu na kuepuka mafoleni ya kijinga.Unapanda na suit yako safi kabisa na unafika uko fresh.
Ikipatikana Dar hii hata tukianza kwa phases tu itasaidia sana sana
 
Stigler's itakuwa tayari iwapo mradi huu utatekelezwa.
Mhmm nchi hii umeme usisikie hadithi za stigler's gorge. Walisema hivyo hivyo kuhusu gas, kwamba umeme ungekuwa historia naona gas ndiyo ikawa historia. Na shida iko pale pale.
Labda itawezekana nisiseme mengi.
 
Tanzania Ni Tajiri Tutajenga Hiyo Haraka Sana
Tunapenda Mawazo Ya Kusaidia Nchi Hii
 
Bunju-kariKoo utashuka Moroko utapanda mwendokasi,utafanya hivyo hivyo kwenda kwingine. Huko kwingine kuna mwendokasi aka BRT.
Samahani nikisema hiyo njia itakuwa ngumu maana imejaaa, gharama za fidia tu zitafanya mradi hata usianze au usiwepo kabisa
 
Mhmm nchi hii umeme usisikie hadithi za stigler's gorge. Walisema hivyo hivyo kuhusu gas, kwamba umeme ungekuwa historia naona gas ndiyo ikawa historia. Na shida iko pale pale.
Labda itawezekana nisiseme mengi.
Sasa hivi tatizo la umeme limepungua sana. Stigler's Wamisri wapo site kama ni hadithi haya.
 
serikali iwaite matajiri wetu wa ndani wawape Tenda ya kujenga barabara za juu
Gharama watakazo zitoa ni mara 5 ya ghalama alisia ndiyo shida ya sekta binafsi za kiafrica
 
SGR na Stiegler's bado havijakamilika, subiri. Ni option nzuri ila ni expensive bila shaka.
 
Sasa hivi tatizo la umeme limepungua sana. Stigler's Wamisri wapo site kama ni hadithi haya.
Limepungua?! Huku bunju hatupati umeme mchana.
Kwani stigler's imeshaanza kuzalisha?! Nini kimepumguza tatizo?! Limepungua wapi?!
 
Hamu ipo, ghalama ndio kichefuchefu. Gasi ingekuwa yetu hata kwa 30% uwezo ungekuwepo tu. Labda tuongeze kodi ni kutopandishwa mishahara kwa miaka mingi tu(tufunge mikanda kifuani)
 
Limepungua?! Huku bunju hatupati umeme mchana.
Kwani stigler's imeshaanza kuzalisha?! Nini kimepumguza tatizo?! Limepungua wapi?!
Siwezi ligi. Umeshinda.
 
Badala ya mwendokasi kwanini tusiweke Metro line kutoka Bunju Hadi Posta? Hii inawezekana kupita juu Kwa juu katikati ya barabara bila kuathiri magari ya kawaida. Train za umeme full automated bila dereva zitatumika. Station zinakuwa juu huko huko abiria wanapanda na kushuka kwa kidaraja juu ya barabara. Treni moja ni Sawa na mabasi ya mwendokasi manne au matano hivyo zinaweza kubeba watu 500-600 Kwa mara moja. Mfano wake ni hapo chini. Picha ya tatu ni stationView attachment 984917View attachment 984918View attachment 984919
We usituletee matatizo hapa! Hayo Ma SGR, Flyover na Bombadier yamesababisha mwaka wa tatu watu hawajaongezewa mishahara....kujenga hio metro si ndio tutaambiwa mishahara tulipwe siku za sikukuu tu!!!
 
Kuanzisha kitu kama hiyo inawezekana,issue ni je ukiambiwa nauli 5000.00 Bunju-Posta utaweza ? au mtataka zile nauli zetu za 800.00 ili ziendeshe mradi mkubwa kama huo..!
 
Kuanzisha kitu kama hiyo inawezekana,issue ni je ukiambiwa nauli 5000.00 Bunju-Posta utaweza ? au mtataka zile nauli zetu za 800.00 ili ziendeshe mradi mkubwa kama huo..!
Eicher zitakuwepo kwa wasiomudu gharama.
 
Back
Top Bottom