Bungeni: Shibuda aongelea hatma yake ndani ya CHADEMA!

Bungeni: Shibuda aongelea hatma yake ndani ya CHADEMA!

Nimemsikiliza sana Shibuda tena kwa makini sana. Hili ni jambo linaloweza kuletwa kwenye vikao ambavyo mimi ni mjumbe. No comment for the time being.
Umekuja kufanya nini sasa hapa, si ueleze mtazamo wako vinginevyo nenda huko kwenye vikao vyenu
 
Tutamtoa na kanisani tutamtenga, tena Pengo alikuwa anaangalia bunge wala hawezi kusubiri ripoti ya padri Slaa kuchukua maamuzi.
Maneno yako na avatar yako vinaendana sana mkuu. Misukule tu ndo inaweza kusema haya.
 
Shibuta tatizo lake ni mtu mwenye 'over comfidence' na anajiona yuko sahihi wakati wote,
mtu akiwa hivyo always anakuwa ni tatizo mahali popote hivyo CDM wanalo hilo. kumfukuza sasa hivi si muafaka kabisa.
 
It takes extra ordinary people to do extraordinary things. Sifa ya kiongozi thabiti ni kutokutabirika
si kwa namna ya huyu mzee - nimeamini kwa nini CCM walimwita MAKAPI aka left overs.
 
Mkuu unaweka habari nusu nusu.... ameponda viongozi wa kisiasa hasa wa Chadema kwa udhalimu, na maslahi binafsi.Amesema yeye hatishwi na Kamati Kuu na amewaonya waandishi wa habari wanaobeba maslahi binafsi ndani ya Chama. Wakati anaongea wabunge wa CDM walionekana wanyonge sana

Nahisi huyu jamaa anaelewa kila kitu sasa na ndio maana ana jeuri ya kuwa mkweli kunakopelekea wabunge wa cdm kuwa wanyonge.
 
shibuda hatufai watanzania kwa sababu hana msimamo kwa lolote ccm alishindwa na leo cdm anafaa nini?

Hakufai wewe Gwaje, hauwezi kuwa unatuwakilisha watanzania wote. Utakuwa unawakilisha tabaka dogo tu lenye mtazamo kama wako
 
Shibuda kesha jisahau,alianza kuwafanyia hivyo hivyo CCM hadi kuna wakati walimshusha kwenye treni huko Tabora,yeye anajiona ni zaidi ya Chadema,inabidi atoswe kutoka kwenye Jahazi la Chadema,aende huko huko kwa waliomtosa,amesahau kuwa Chadema ndio iliyomuweka hapo,Shibuda hana umaarufu kuizidi Chadema bana
 
Halafu Magwanda wakachukua makapi, siku nyingine mjifunze siyo kukurupuka tu
Huwezi kuilaumu chadema kwa kumchukua Shibuda, CDM ni chama kinachokua na kinakubalika na wananchi. Unapofungua milango watu waje kujiunga na wewe kwa nia njema kabisa kwa bahati mbaya unaweza kupata na MAINZI, MENDE, MIJUSI na watu wenye akili timamu. Sasa hili la SHIBUDA siwezi kuilamu CDM kwa namna yeyote ile. yaani CDM ilipata GALASA kwa bahati mbaya bila kujua.

But i take this as a challenge and challenge gives you an opportunity to learn, na kumbuka CHAMA kinapopanuka (kukua) vitu kama hivi lazima vinajitokeza tu mahali popote duniani. Na vizuri zaidi ni kwamba SHIBUDA in nothing as far as CDM popularity is concerned.

CHADEMA ina nguvu ya umma, no one is more pupular in CDM than us members and suppoters. (wananchi walalahoi ndiyo wenye CHADEMA for your info).
 
hapo dawa nikumtimua aungane na madiwani wake na kitu kingine hamjui kama hilo ni fupa waliolisusa chama cha mafisi wa ahadi kwa hiyo hili nishuzi lao cdm itabidi wafanye namna..
 
Bahati mbaya sijasikia hiyo hutuba yake lakini mimi naamini kitu kimoja tu kwamba Shibuda ni mkweli na si mtu wa kumung'unya maneno. Tatizo lilianzia kwenye posho baada ya kupingana na wenzake lakini sasa suala la Posho ndani ya CDM limeishia wapi? Mbona hawalipingi tena na wamekaa kimya? Sasa kama Shibuda hakuwa mkweli ni nini? Hakutaka kuwa mnafiki kama walivyowanafiki wengi.
 
ukweli ni kuwa shibuda anajihami kutafuta huruma na umaarufu akifukuzwa,lakini analazimisha kichokozi kuona reaction ya viongozi ili ajue upepo ulivyo!
 
shibuda kutokuwa na uhakika na hatma yake zaidi ya kupata tetesi inamtesa sana na wajanja waliokuwa wanamsapoti wamemkimbia kidizaini! Safari ndio mwisho wa shibuda kisiasa! Hauziki tena nje na ndani ya cdm!
 
Anachojivunia Shibuda ni kinga aliyonayo awapo bungeni. Kisheria huwezi kumchukulia mbunge yeyote kwa kauli aliyoizungumza akiwa bungeni. CDM wanalifahamu hilo ndiyo maana wanasita kumchukulia hatua. Sasa kama kweli Shibuda ni jasiri atoke bungeni aende kwenye jimbo lake halafu akauseme huo upuuzi, ninavyowajua CDM hatachukua round atakuwa out. Mpeni muda tu atoke Bungeni.
 
kwa kifupi ni kazi kufanya kazi na shibuda kwanza anaamini yeye anjua kuzidi yeyote na siku zote anapenda kusikilizwa hata kama anaharibu.anaonekana anapenda utukufu na vyombo vya habari anivipenda vimwandike vizuri na si vinginevyo.anapenda madaraka na naamini haoni shida kurudi sisiemu kama akihakikishiwa ulaji lakini kwa sasa ni mwisho wake.anajua kiswhili vizuri na anaweza vizuri kutumia semi na tungo nzuri zinazoweza kuwashawishi watu wasioona mbali kuwashawishi kuwa yeye yupo safi lakini japo mimi si mwana siasa sioni kama ni kiongozi mnzuri.kwa sababu anaonekana anaweza kwenda na rangi inayomvutia tuwe makini .ningewashauri cdm waangalie kwa makini jinsi ya kumfukuza kwa kuwa huyu mtu anapenda kutumia vyombo vya habari kujisafisha.ni vizuri wakajipanga wakamuondoa
 
Wataalam wa lugha.. Hivi sio kweli kwamba Makapi ndiyo yenye nutrition zaidi ya unga mweupe!. sasa kwa nini makapi yasithaminiwe zaidi au ndio ktk utamaduni wa mtu mweusi kuthaminisha rasilimali (watu na mazingira) zake bila ubora wake isipokuwa shibe kwanza.. yaani kwetu Tanzania makapi (yenye afya) ndio hutupwa mazoea ya tukaletewa (Bulga) ngano ilikobolewa kama msaaada basi ndio tukaona kukoboa ndio bomba.
Aisifiaye mvua imemnyeshea.... (uhaba wa mvua) - wakati wenzetu Ulaya wao hulaani mvua na kusifia jua zaidi..
 
Back
Top Bottom