Kuhusu Wabunge kuongezewa posho (ambayo ndio chanzo cha kupishana na CDM) hujasikia? Nadhani hujamwelewa hata kidogo kwa sababu amerudia maneno yake ya baadhi ya viongozi kuwa na maslahi binafsi (ambapo amekuwa akumaanisha Zitto) na akasema wananchi wa Maswa wasitishwe na watu wanaotishia kumfukuza ambao sio vyombo vya habari bali ni viongozi wake.
unajua unaweza kuwa na hoja makini na njema, lakini mtu mwenye busara anaangalia wapi aisemee, kwa akina nani, katika mazingira gani na kwa lengo gani. Mtu kama Shibuda ambaye hajuia hayo ni wa kuogopwa, na sidhani kama watoto na mke wake anawatendea haki. jambo la kukumbukwa na kila mtanzania ni juu ya yale aliyokuwa anayasema, alipokuwa akikishutumu chama chake cha zamani, CCM, na alipoingia upinzani alisifia nini na kuiponda CCM kwa kiasi gani. Asifikiri kuwa watanzania wa sasa ni wajinga na wsahaulifu kama yeye. Wala asiwaone wasukuma wa maswa kama vimada vyake, wana akili na busara za kutosha, iko siku atalinywa