Wa kusoma
JF-Expert Member
- Jul 30, 2011
- 3,454
- 2,975
Mwenyeketi wa kamati ya nishati na madini january anamalizia kuongea na baada ya hapo spika atamwita mwenyekiti wa kamati ndogo ya bunge iliyoundwa kuchunguza sakata la Jairo. Tuendelee kujuzana.
UPDATED:
Jairo, Luhanjo na Ngeleja wabanikwa Bungeni!
Spika Makinda
Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza sakata la malipo ya mamilioni ya shilingi kwa watendaji wa Wizara ya Nishati ili kusaidia bajeti ya wizara hiyo ipite katikati ya mwaka huu imewasilishwa Bungeni na kuonesha kuwa malipo hayo hayakuwa halali na ulaghai mkubwa umefanyika na hivyo kutaka wahusika wawajibishwe.
Taarifa hiyo imesema kuwa baada ya kupitia ushahidi wote na kuwahoji watu mbalimbali imehitimisha kuwa "utaratibu wa uchangishaji wa fedha uliofanyika katika Wizara ya Nishati na Madini haukuwa na uhalali wowote kwa mujibu wa Katiba, Sheria na Kanuni za Fedha za Umma." Ripoti hiyo pia ilimtuhumu Katibu Mkuu Bw. Luhanjo kutosema ukweli kuhusu utaratibu huo. "Kamati Teule imeridhika pia kwamba huo siyo utaratibu wa kawaida kama ilivyoelezwa na Katibu Mkuu Kiongozi katika Taarifa yake kwa Umma kupitia Vyombo vya Habari kuhusu Uchunguzi wa Awali" imesema ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imeeleza pia kuwa fedha zilizotumika kutekeleza agizo la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. David Jairo hazikutoka kwenye bajeti yoyote iliyowekwa kwa ajili hiyo bali zilichotwa kutoka katika akaunti mbalimbali zilizokuwa zimetengewa fedha. "Nyaraka za matumizi halisi zinaonyesha kuwa fedha zilizokusanywa zimetumika kwa ajili ya malipo ya posho ya kujikimu kwa watumishi 69 wa Wizara, posho ya vikao kwa watumishi 243 waliokuwa Dodoma, manunuzi ya chakula, manunuzi ya vifaa vya kuandikia, malipo ya Takrima kwa Waziri na Naibu Waziri na manunuzi ya mafuta kwa ajili ya magari, matumizi ambayo yangeweza kugharimiwa na kasma husika za Wizara bila kuhitaji kuchangisha" imebainisha ripoti hiyo.
SOMA HABARI HII KWA KIREFU ZAIDI
Attachment chini ni Report ya Kamati ya kuchunguza sakata lenyewe:
UPDATED:
Jairo, Luhanjo na Ngeleja wabanikwa Bungeni!
Spika Makinda
Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza sakata la malipo ya mamilioni ya shilingi kwa watendaji wa Wizara ya Nishati ili kusaidia bajeti ya wizara hiyo ipite katikati ya mwaka huu imewasilishwa Bungeni na kuonesha kuwa malipo hayo hayakuwa halali na ulaghai mkubwa umefanyika na hivyo kutaka wahusika wawajibishwe.
Taarifa hiyo imesema kuwa baada ya kupitia ushahidi wote na kuwahoji watu mbalimbali imehitimisha kuwa "utaratibu wa uchangishaji wa fedha uliofanyika katika Wizara ya Nishati na Madini haukuwa na uhalali wowote kwa mujibu wa Katiba, Sheria na Kanuni za Fedha za Umma." Ripoti hiyo pia ilimtuhumu Katibu Mkuu Bw. Luhanjo kutosema ukweli kuhusu utaratibu huo. "Kamati Teule imeridhika pia kwamba huo siyo utaratibu wa kawaida kama ilivyoelezwa na Katibu Mkuu Kiongozi katika Taarifa yake kwa Umma kupitia Vyombo vya Habari kuhusu Uchunguzi wa Awali" imesema ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imeeleza pia kuwa fedha zilizotumika kutekeleza agizo la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. David Jairo hazikutoka kwenye bajeti yoyote iliyowekwa kwa ajili hiyo bali zilichotwa kutoka katika akaunti mbalimbali zilizokuwa zimetengewa fedha. "Nyaraka za matumizi halisi zinaonyesha kuwa fedha zilizokusanywa zimetumika kwa ajili ya malipo ya posho ya kujikimu kwa watumishi 69 wa Wizara, posho ya vikao kwa watumishi 243 waliokuwa Dodoma, manunuzi ya chakula, manunuzi ya vifaa vya kuandikia, malipo ya Takrima kwa Waziri na Naibu Waziri na manunuzi ya mafuta kwa ajili ya magari, matumizi ambayo yangeweza kugharimiwa na kasma husika za Wizara bila kuhitaji kuchangisha" imebainisha ripoti hiyo.
SOMA HABARI HII KWA KIREFU ZAIDI
Attachment chini ni Report ya Kamati ya kuchunguza sakata lenyewe: