Bungeni: Mbowe aweka msimamo wa posho

Bungeni: Mbowe aweka msimamo wa posho

Edson Zephania

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2011
Posts
517
Reaction score
112
Msimamo wa kutopokea posho upo palepale, tufanye maamuz kwa maslah ya wananch na si wabunge, walimu, polisi, manesi nk wanapata wapi posho?. Kama suala ni sheria bunge ndo hutunga sheria hvyo pia kunauwezekano wa kubadilisha.

Ni kwamba Mbowe amejaribu kuelezea unafiki wa viongozi na wabunge katika nyanja hizi.
1. Je kuna kiongozi mpaka leo hii ambaye hajui ukimwi unaambukizwaje? Sasa hizo semina ni za nini?
2. Wafadhili wanasafiri na economy class watanzania wafanyakazi business class
3. Je ni wangapi wakistaafu wanaweza nunua shangingi? Sasa ni kwanini yasiuzwe na wafanyakazi wakopeswhe magari yao?
4. Semina zimezidi kila waheshimiwa wakienda wanaishia kupewa mabegi, huo ni wizi mkubwa sana.

Kwa kifupi viongozi wanatumia muda mwingi kwenye vikao vya kulipana posho na kama hamna posho hamna anayehudhuria
 
Msimamo wa kutopokea posho upo palepale, tufanye maamuz kwa maslah ya wananch na si wabunge, walimu, polisi, manesi nk wanapata wapi posho?. Kama suala ni sheria bunge ndo hutunga sheria hvyo pia kunauwezekano wa kubadilisha.

endeela kutuhabarisha mkuu
 
Nimemsikiliza Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe. Kwa kweli alichokiongea naweza Kusema Amefunga Bunge la kumi (10), bila shaka kuna watu machozi yamewatoka. Ni Misumari ya Moto mwenye Macho haambiwi Tazama
 
lete habar mkuu mbona kimya hiyo nitaingalia saa sita usiku jamaa ni mtambo sasa na kuhusu habari ya magazeti kwenye gazeti la mwanchi?na upotoshaji wa taarifa unafiki sana
 
Wabunge wanasafiri First Class kwenda Washngton kwa Kwa Shillingi millioni 12 wakati Donors wanasafiri Economy class
 
Jamani hakuna umeme - tv zimika. leteni habari
 
Yahaaaaa ni kweli nimemsikiliza ameongea point mwanzo mwisho,alafu kulikuwa na utulivu wa hali ya juu pindi anaongea.
 
Viongozi wiki nzima wanakimbizana kwenye Seminar lengo lao ni kufukuzana na Posho. Kuna Viongozi mpaka leo hawajui jinsi ya Kujikinga na ukimwi?
 
Kila kikao wanapewa mabegi, tangia awe mbunge analather bag 24 zinaishia kugaiwa kwa ndugu 2.
 
aisee ccm wanalo je kuna kitu wanaweza zungumza tena wandugu hao ccm si ni bora bunge lifungwe alafu watekeleze hayo
 
Duh!safi sana mawazo mbadala ni muhimu sana katika kuongozi nchi hii!!
 
Ameuliza ni watumishi wangapi wa Uma leo wakiingia kwenye Sekta Binafsi wataendelea kutumia Mashangingi? Ni watanzania wangapi walio kwenye sekta ya Una leo hii wakiwa kwenye sekta binafsi watasafiri Bussoness Class ( Hata kupanda ndege tu). Hiki ni Kibano ambacho nadhani mpaka sasa Wabunge wanaendele kukijadilia mioyoni mwao
 
wakishastafu ubunge hakuna anaethubutu kupanda first class, wala bussinec class na wengine hata hzo ndege hawapandi kabisa.... Kanifurahisha sana.
 
Back
Top Bottom