Ronal Reagan
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,299
- 3,055
Ni sawa wabunge hao kutaka iwe hivyo, na wana haki ya kuogopa, sana tu.
Wamekuwa wanafanya mambo ya ajabu na ya OVYO sana. Uwakilishi wa wananchi wa majimbo yao ambao ndio msingi wa kuwepo kwao bungeni hawaufanyi badala yake wamekuwa sehemu ya genge la mafisadi ambao pia ndio wamiliki wa serikali ya JK. Kwa hiyo dhamira zao zimewasuta na wamejiona wako uchi, cha kusikitisha badala watubu na kubadilika wanataka kujificha kwa kubaki gizani.
Huo uthubutu wa kutoa hoja mbovu kama hiyo unaonesha kiwango cha ulevi wa madaraka na umaututi wa uongozi wa ccm.
Wamekuwa wanafanya mambo ya ajabu na ya OVYO sana. Uwakilishi wa wananchi wa majimbo yao ambao ndio msingi wa kuwepo kwao bungeni hawaufanyi badala yake wamekuwa sehemu ya genge la mafisadi ambao pia ndio wamiliki wa serikali ya JK. Kwa hiyo dhamira zao zimewasuta na wamejiona wako uchi, cha kusikitisha badala watubu na kubadilika wanataka kujificha kwa kubaki gizani.
Huo uthubutu wa kutoa hoja mbovu kama hiyo unaonesha kiwango cha ulevi wa madaraka na umaututi wa uongozi wa ccm.