Bunge lingefanya kazi za kibunge kwa kamati, jifunzeni kwa Bunge la Marekani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,264
Huo mfumo tunaotumia sasa wa bunge zima na wabunge wote kujadili kila masuala hautupi tija na pia unaligharimu taifa bila umuhimu wote. Kama huu ndio mfumo wa mabunge ya jumuiya ya madola basi hauna tija kwetu inabidi tuachane nao tu.

Ilipaswa kuwe na kamati za kisekta za bunge kujadili na kusimamia masuala ya nchi na wabunge wagawanye huko kulingana na utaalamu na uzoefu wao. Sasa hivi unaweza kukuta mbunge anachangia ripoti ya CAG wakati hajui hata balance sheet ikoje au sheria ya manunuzi ya nchi inasemaje. Mtu anachangia sekta ya gesi akitokwa na povu na hajui chochote kuhusu biashara ya gesi, mwingine unakuta anotoka Kinondoni au Ilala na anachangia kwenye kilimo.

Bunge lingegawa kazi zake kwenye kamati, midahalo na usimamizi wote wa serikali ufanyike huko. Hata hiyo ripoti ya CAG ingejadiliwa na uamuzi kumalizika kwenye kamati ya wabunge wachache husika, sio kuita wabunge wote kuijadili wakati wengine wanataka waonekane live tu. Sasa hivi unaweza kukuta mambo CAG na ushoga yanajadiliwa katika kikao kimoja! Hii inakuwa shaghalabaghala tu.

Bunge zima likutane tu wakati wa kupitisha miswaada iliyotoka kwenye kamati na bajeti kuu, hii italeta tija ya mijadala na itasaidia sana na kubana matumizi.
 
Tatizo ni kuwa wabunge hawakuchaguliwa kulingana na taaluma zao bali ukada wa chama hivyo kuna mada au hoja nyingi zitashindwa kujadiliwa kwa sababu ya ukosefu wa wataalam husika!
 
ULIPOTAJA TU MAREQAN UZI UMENIBOA KUUSOMA
Tanzania bila ushoga inawezekana
 
Hao ambao hawana taaluma au uzoefu wowote wasubirie kikao cha pamoja cha bunge kupiga kura tu. Itasaidia kuokoa hata pesa za posho.
Tatizo ni kuwa wabunge hawakuchaguliwa kulingana na taaluma zao bali ukada wa chama hivyo kuna mada au hoja nyingi zitashindwa kujadiliwa kwa sababu ya ukosefu wa wataalam husika!
 
Ningetolea mfano Iran, Saudi Arabia, China au Urusi kama ningekuwa najua jinsi mabunge yao yanafanya kazi.
ULIPOTAJA TU MAREQAN UZI UMENIBOA KUUSOMA
Tanzania bila ushoga inawezekana
 
Badala ya uwepo wa wabunge wa viti maalum, ungewekwa utaratibu wa kupata wawakilishi wa kisekta kutokana ubobevu wao wa kitaalamu katika maeneo husika.

Mathalani Chama cha Walimu kupitia Mkutano Mkuu wa Mwaka, wangepuga kura kuchagua mwakilishi wao, hali kadhalika Tanganyika Legal Society, Chama cha Watu Wenye Mahitaji Maalum, n.k.

Wawakilishi wa makundi maalum ni watu sahihi kabisa katika kuzichambua na kuzielezea hoja za kisekta vizuri na umahiri mkubwa kuliko hili kundi la wanasiasa ambao wapo wapo tu kwa ajili ya maslahi ya vyama wanavyoviwakiliaha.

Hapo sikazumgumzia uwakilishi wa wabunge wasiokuwa na chama chochote kile kama lile kundi la COVID-19, ambao katika mabunge ya Jumuiya ya Madola huwezi kuwakuta nchi yoyote ile zaidi ya Tanzania. Hapo ndani ya Bunge yupo Mwanasheria Mkuu wa serikali, na Waziri wa Katiba na Sheria, wote hao wala hawangaishwi na ukiukaji huu wa katiba ndani ya Bunge zaidi ya kusikilizia mtazamo binafsi wa Spika wa Bunge, ama maelekezo ya "party caucus" hata kama ni kinyume cha katiba na sheria..
 
Hao ambao hawana taaluma au uzoefu wowote wasubirie kikao cha pamoja cha bunge kupiga kura tu. Itasaidia kuokoa hata pesa za posho.
Kwa kuwa hao ambao hawana taaluma ni wengi na maamuzi yote nchini huamuliwa kwa kupiga kura hoja yako haiwezi kukubalika na ndiyo utakuwa mwanzo wa nchi kutotawalika!
 
ULIPOTAJA TU MAREQAN UZI UMENIBOA KUUSOMA
Tanzania bila ushoga inawezekana
Kwamba Marekani ndo anakuja kukushikisha ukute ufir.we?
We ni shoga na wala hujabakwa na mzungu ushoga umesababishiwa na baba yako
 
You have a point..
Ingawa umechemka kuhusu kilimo Kinondoni na ilala...
Kilimo ni pamoja na ufugaji...huko kinondoni kuna wafugaji kuku na mbuzi kuliko hata WA mikoani
 
Back
Top Bottom