Bunge Linapotumia Nguvu Kubwa Kuficha Udhaifu Wake...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya mambo ya kwanza kabisa tunayojifunza kama wazazi ni kubembeleza watoto. Mtoto anapozaliwa anakuwa ni mtegemezi mkubwa wa mzazi kwa kila kitu na pole pole anavyozidi kukua ndivyo anavyozidi kupunguza utegemezi huo. Lakini kama kuna kitu ambacho mzazi anaendelea kuwa nacho kwa mtoto ni nguvu yake ya kuweza kumuumiza mtoto kwa maneno au kumbembeleza. Ni nguvu kubwa sana kwa mzazi kuweza kumuita mtoto wake (hata kama ameshakua mtu mzima) na kumtuliza anapokuwa katika matatizo. Hili ni jukumu la kama mzazi na tunalipitisha jukumu hili kwa watoto wetu ili na wao wawe wazazi bora kwa watoto wao.

Hivyo, mzazi mara nyingi haumizwi sana na mtoto wake na anajifunza kumvumulia mtoto wake sana. Uvumilivu wa mzazi kwa mtoto wake nao ni mkubwa sana. Kama mzazi amemkuza mtoto toka anavyojimwagia kinyesi hadi makamasi basi mzazi anaweza kuvumilia mengi tena hata kwa mtoto mkubwa. Mtoto ambaye amekua na maisha yakamharibikia bado anaweza kupata uvumulivu kwa mzazi wake. Inapofika mahali mtoto anamuumiza mzazi hadi mzazi anaona ameshindwa kabisa kuvumilia jambo lile ndio hugeuka kile kinachoitwa "laana".

Ndugu zangu serikali na watumishi wa serikali si wazazi wa Watanzania. Uvumulivu au upendo wao kwa wananchi haulingani na wazazi na hawapaswi kututendea kama watoto wao au sisi kuwachukulia kama wazazi wa taifa. Wanasiasa na viongozi wa kuchaguliwa wote ni watumishi tu wa wananchi. Hawapaswi kuumizwa sana na maneno ya watu au matendo ya watu kiasi cha kukwazika sana.

Mojawapo ya mambo yananikera - na hili nimeshawahi kulisema mara kadhaa huko nyuma - ni kuwa viongozi wetu wasijione kama wao ni wazazi na hivyo wanataka watu wawabembeleze kwa maneno matamu. Sipendi kuona viongozi wako huru kusema lolote kwa yeyote lakini wao wakisemewa yale yale wanayoyasema wao wanajisikia kuumia. Hili la Spika na CAG ni mfano mdogo tu wa jinsi gani chombo kikubwa kama Bunge kinaumizwa na maneno! Hii ni fedheha! Yaani, kuna watu wameumia sana hadi kufanya kikao na kupitisha azimio kabisa kuwa wameumizwa! Huu ni udhaifu wa namna gani?

Wadudu kama nzi ni wasumbufu sana na wana madhara wakati mwingine; lakini hakuna mtu ambaye ana akili timamu ambaye anaamua kutumia gobole kuua nzi! Kuna mtu aliwahi kuishia kuchoma nyumba yake kwa sababu alitaka kujaribu kuua mende kwa kuwachoma na mshumaa! Kauli ya CAG hata kama angekuwa amemaanisha kabisa kuwa Bunge ni dhaifu (kwa utendaji na kwa namna ilivyo) bado haikuwa sababu ya msingi ya kumuita kujieleza wala kutumia muda wa Bunge kujadili! Huku ni kutumia nguvu kubwa kushughulikia jambo dogo; kujaribu kuonesha nguvu katika udhaifu!

Ni lazima tujifunze kuvumulia maoni hata kama yanaudhi sana. Viongozi au kiongozi ambaye hawezi kuvumulia maoni ni muhimu sana asitafute uongozi! Kutofautiana maoni au mawazo ni sehemu ya uhuru wa maoni na mawazo. Mwaka 2008 niliandika hapa kuwa haki ya maoni na uhuru wa mawazo vilivyomo katika Katiba haulindi maoni na mawazo mazuri! Haki hizi ziko kwenye Katiba kulinda maoni mabovu, ya kuudhi, ya kijinga na wakati mwingine ya kukera kweli kweli. Haya ndio maoni yanayolindwa kwa sababu maoni mazuri, ya kufurahisha na ya kutuliza mioyo hayahitaji kulindwa!

Nafahamu pia kuwa kuna watu kwa asili yao hawana uvumulivu; wanaumizwa sana moyoni wakipingwa, wanakwazika sana kuwajibiwa, na wanajisikia kutukanwa wakipingwa. Hili ni kweli hasa kama watu wana madaraka makubwa. Mwalimu akijibishiwa na mwanafunzi anajisikia amedharauliwa hata kama mwanafunzi yuko sahihi; polisi akikataliwa na raia kwenye jambo fulani anaona basi ngoja ampige kirungu! Ndio maana mojawapo ya misemo ya awali niliyoiasisi ni kuwa "hoja ijibiwe kwa hoja na si kwa vihoja". Mtu anapojibu hoja kwa vihoja anake ameshindwa hoja!

Hili la Spika na wabunge wenzake kutumia nguvu kubwa hata - naamini wakiwa timamu - kuamua ati kutoshirikiana na CAG ni ushahidi kabisa kuwa Bunge ni dhaifu, linajifedhehesha na limelewa ule ugimbi uleweshao wa madaraka! Wanaamini kabisa kwa kuwa wao ni wabunge na wako wengi basi wanaweza kufanya lolote, popote na kwa lolote kwa kusema kwa kauli moja tu "ndiyo".

Nani atawaambia ukweli huu bila kuonekana naye anawaumiza? Inawezekana basi kama taifa tuendelee kuwabeba kwenye mbeleko na kuwabembeleza wasiumie sana moyoni wakikosolewa, wasinung'unike wakikataliwa, na wasijisikie unyonge wakinyimwa! Tutakuwa na taifa la viongozi wa namna gani.

Sitaki hata kufikiria.
 
Ni vema ijulikane aliyagiza CAG kufanyiwa hayo aliyofanyiwa Ni JIWE mwenyewe.

Bifu lao ni la muda mrefu tangu akiwa ujenzi ambapo Profesa alishikia bango matumizi ya Bilioni 240 ambayo yalionekana kwenda kujenga barabara lakini kiuhalisia fedha hizo hazikuwa huko.

Ni vile Katiba imempa KINGA CAG vinginevyo baada ya JIWE kuwa Mkuu angeanza kumtumbua.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya mambo ya kwanza kabisa tunayojifunza kama wazazi ni kubembeleza watoto. Mtoto anapozaliwa anakuwa ni mtegemezi mkubwa wa mzazi kwa kila kitu na pole pole anavyozidi kukua ndivyo anavyozidi kupunguza utegemezi huo. Lakini kama kuna kitu ambacho mzazi anaendelea kuwa nacho kwa mtoto ni nguvu yake ya kuweza kumuumiza mtoto kwa maneno au kumbembeleza. Ni nguvu kubwa sana kwa mzazi kuweza kumuita mtoto wake (hata kama ameshakua mtu mzima) na kumtuliza anapokuwa katika matatizo. Hili ni jukumu la kama mzazi na tunalipitisha jukumu hili kwa watoto wetu ili na wao wawe wazazi bora kwa watoto wao.

Hivyo, mzazi mara nyingi haumizwi sana na mtoto wake na anajifunza kumvumulia mtoto wake sana. Uvumilivu wa mzazi kwa mtoto wake nao ni mkubwa sana. Kama mzazi amemkuza mtoto toka anavyojimwagia kinyesi hadi makamasi basi mzazi anaweza kuvumilia mengi tena hata kwa mtoto mkubwa. Mtoto ambaye amekua na maisha yakamharibikia bado anaweza kupata uvumulivu kwa mzazi wake. Inapofika mahali mtoto anamuumiza mzazi hadi mzazi anaona ameshindwa kabisa kuvumilia jambo lile ndio hugeuka kile kinachoitwa "laana".

Ndugu zangu serikali na watumishi wa serikali si wazazi wa Watanzania. Uvumulivu au upendo wao kwa wananchi haulingani na wazazi na hawapaswi kututendea kama watoto wao au sisi kuwachukulia kama wazazi wa taifa. Wanasiasa na viongozi wa kuchaguliwa wote ni watumishi tu wa wananchi. Hawapaswi kuumizwa sana na maneno ya watu au matendo ya watu kiasi cha kukwazika sana.

Mojawapo ya mambo yananikera - na hili nimeshawahi kulisema mara kadhaa huko nyuma - ni kuwa viongozi wetu wasijione kama wao ni wazazi na hivyo wanataka watu wawabembeleze kwa maneno matamu. Sipendi kuona viongozi wako huru kusema lolote kwa yeyote lakini wao wakisemewa yale yale wanayoyasema wao wanajisikia kuumia. Hili la Spika na CAG ni mfano mdogo tu wa jinsi gani chombo kikubwa kama Bunge kinaumizwa na maneno! Hii ni fedheha! Yaani, kuna watu wameumia sana hadi kufanya kikao na kupitisha azimio kabisa kuwa wameumizwa! Huu ni udhaifu wa namna gani?

Wadudu kama nzi ni wasumbufu sana na wana madhara wakati mwingine; lakini hakuna mtu ambaye ana akili timamu ambaye anaamua kutumia gobole kuua nzi! Kuna mtu aliwahi kuishia kuchoma nyumba yake kwa sababu alitaka kujaribu kuua mende kwa kuwachoma na mshumaa! Kauli ya CAG hata kama angekuwa amemaanisha kabisa kuwa Bunge ni dhaifu (kwa utendaji na kwa namna ilivyo) bado haikuwa sababu ya msingi ya kumuita kujieleza wala kutumia muda wa Bunge kujadili! Huku ni kutumia nguvu kubwa kushughulikia jambo dogo; kujaribu kuonesha nguvu katika udhaifu!

Ni lazima tujifunze kuvumulia maoni hata kama yanaudhi sana. Viongozi au kiongozi ambaye hawezi kuvumulia maoni ni muhimu sana asitafute uongozi! Kutofautiana maoni au mawazo ni sehemu ya uhuru wa maoni na mawazo. Mwaka 2008 niliandika hapa kuwa haki ya maoni na uhuru wa mawazo vilivyomo katika Katiba haulindi maoni na mawazo mazuri! Haki hizi ziko kwenye Katiba kulinda maoni mabovu, ya kuudhi, ya kijinga na wakati mwingine ya kukera kweli kweli. Haya ndio maoni yanayolindwa kwa sababu maoni mazuri, ya kufurahisha na ya kutuliza mioyo hayahitaji kulindwa!

Nafahamu pia kuwa kuna watu kwa asili yao hawana uvumulivu; wanaumizwa sana moyoni wakipingwa, wanakwazika sana kuwajibiwa, na wanajisikia kutukanwa wakipingwa. Hili ni kweli hasa kama watu wana madaraka makubwa. Mwalimu akijibishiwa na mwanafunzi anajisikia amedharauliwa hata kama mwanafunzi yuko sahihi; polisi akikataliwa na raia kwenye jambo fulani anaona basi ngoja ampige kirungu! Ndio maana mojawapo ya misemo ya awali niliyoiasisi ni kuwa "hoja ijibiwe kwa hoja na si kwa vihoja". Mtu anapojibu hoja kwa vihoja anake ameshindwa hoja!

Hili la Spika na wabunge wenzake kutumia nguvu kubwa hata - naamini wakiwa timamu - kuamua ati kutoshirikiana na CAG ni ushahidi kabisa kuwa Bunge ni dhaifu, linajifedhehesha na limelewa ule ugimbi uleweshao wa madaraka! Wanaamini kabisa kwa kuwa wao ni wabunge na wako wengi basi wanaweza kufanya lolote, popote na kwa lolote kwa kusema kwa kauli moja tu "ndiyo".

Nani atawaambia ukweli huu bila kuonekana naye anawaumiza? Inawezekana basi kama taifa tuendelee kuwabeba kwenye mbeleko na kuwabembeleza wasiumie sana moyoni wakikosolewa, wasinung'unike wakikataliwa, na wasijisikie unyonge wakinyimwa! Tutakuwa na taifa la viongozi wa namna gani.

Sitaki hata kufikiria.


Mzee mwenzangu, mimi naona in the past two years ume-adopt approach ya "the end will justify the means". I wish I could share this perspective. However, changamoto kubwa ni kama haya uliyoyaeleza hapo juu. Viongozi wanalewa madaraka. JPM ni populist leader, wasaidizi wake wameamua wasibaki nyuma..... Wanatwambia yale tunayopenda kuyasikia (TZ ni tajiri, inaweza kuwa donor country, tunaweza kujenga viwanda lukuki nk). Lakini Ukweli ni kwamba hawatwambii tutafikaje huko! kwa hii approach yake, it is difficult kuiona hiyo neema tunayohubiriwa kila siku. precisely kila kitu kinafanywa kwa mileage ya siasa. Rejea swala ka Korosho. Ni kitu ambacho watawala hawakuangalia mbele madhara yake. Hata kama wakulima umewalipa kwa hela ya ndani..mwisho wa siku tunahitaji Hard currency! Tumelifanikisha hilo? tukaonyeshwa ANDO akisaini mkataba wa dola 180M..what happened? wote tunajua... Rejea swala la CAG.....eti ameliita bunge dhaifu!

Adui namba moja wa taifa letu, ni kwa viongozi wetu kuona sheria kama vikwazo badala ya kuwa 'enablers". Hata siku moja hatuwezi kujenga taifa huru kwa kusigina sheria. wasichojua wengi, sheria ndo inamfanya mnyonge na tajiri wote waitwe waTanzania. waonekane wana utu. Short of that, wote tunajua madhara. Law is the last protector and guarantor of our humanity and unity as peoples. Sasa hivi kasumba imezuka ya kuona mtu akivunja sheria kama kitu cha kawaida hata kama ni Kiongozi (au ni mwenzetu). Lakini madhara yake ni makubwa...leo, kesho au kesho kutwa no one knows!

Again, wengi tumekuwa disillusioned na watawala kwa miaka mingi. Lakini sioni hii awamu kama itatupeleka kwenye neema. Simple reason being, huwezi kuongoza kwa kuamini kwamba mawazo yako ndo bora na muhimu. Kiongozi thabiti ni yule anayetumia ushawishi kuhakikisha mawazo yake/hoja zake zinakubalika. Siyo yule anayeamini kwenye nguvu ya polisi na dola...Utakwama tuu...

Ni muhimu waTanzania kwa ujumla wetu kutambua kwamba ...hawa viongozi wetu wanaolewa madaraka...ni kwa sababu wanaamini kabisa mifumo iliyopo/na sisi wenyewe hatuwezi kuwawajibisha..after all wengi wenye uwezo huo au kutambua umuhimu wa kuwajibishana ni sehemu ya huo utawala kwa namna moja au nyingine. But for how long can status quo continue? Sijui!

Tufike mahala waTanzania, kwa ujumla wetu, tuwe mstali wa mbele kutetea na kuunga mkono uongozi na viongozi wanaoheshimu sheria zilizowekwa kwa manufaa ya waTanzania na waTanzania wenyewe..... Vinginevyo tunachimba shimo letu wenyewe.

Na ipo siku tutalaumiana. Maendeleo hatuyaoni Ingawa umoja na mshikamano wetu tumeuweka rehani.
 
It's just that Africans are stupid creatures, otherwise wasingekuwa wanahangaika kudhoofisha mamlaka ya CAG! Msomi yeyote wa kawaida anajua BUNGE LA TZ NI DHAIFU MNO, ujinga ujinga tu. Sasa usipoisimamia serikali vizuri nani atafanya hivyo? While the parliament is constitutionally mandated to supervise the government? Eti bunge halitafanya kazi na CAG! Hizi akili za matope utaziona kwa mtu mweusi tu. For sure we r such an abnormal, misplaced creatures, messed up everywhere. Kama wanataka kutengeneza tyranny waseme.
 
Acha unafiki!

 
Bunge hatimaye limemuonyesha CAG kama lenyewe sio dhaifu pale liliposusa kumpa ushirikiano, inachekesha sana..

Bunge letu lingekuwa imara kwenye kushauri, kuonya na kuiwajibisha Serikali basi leo hii tungekuwa mbali sana..
 
Mzee mwanakiji hii anajifanya halijui
Ni vema ijulikane aliyagiza CAG kufanyiwa hayo aliyofanyiwa Ni JIWE mwenyewe. Bifu lao ni la muda mrefu tangu akiwa ujenzi ambapo Profesa alishikia bango matumizi ya bilioni 240 ambayo yalionekana kwenda kujena barabara lakini kiuhalisia fedha hizo hazikuwa huko. Ni vile Katiba imempa KINGA CAG vinginevyo baada ya JIWE kuwa Mkuu angeanza kumtumbua. Suala lingine ni UDINI, nina ushahidi kila mara jiwe akiwa anamuhusisha PROFESA na DINI yake na wala wasaidizi wake hawajawahi kumzuia kufanya hivyo.

USOGA WI KUA KATI MWINA NSONGOO
 
Na Kumbuka wakati wabunge wanapiga kelele budget ya CAG kupunguzwa Mzee mwanakiji alijetokeza kuteteana huo upungwazaji, akaenda mbali zaidi hadi kudiliki kusema kama CAG hawezi fanya kazi na hiyo budget aliyotengewa a ondoke.

Chuki za jiwe kwa CAG hazihitaji PhD kuzigundua
Akili zako zimeanza kurudi kikaragosi cha dikteta na dhalimu. Wewe ndiye ulikuwa wa kwanza kutaka CAG Assad afukuzwe kazi au ajiuzulu..

USOGA WI KUA KATI MWINA NSONGOO
 
Pole mzee wetu "Mwanakijiji" usiombe JF ikukatae. Ungechagua kusimamia ukweli basi ukweli leo ungekutetea..

Yule mheshimiwa, mtukufu, mfalme nashangaa anaogopa ukaguzi. Yeye si mwenyeheri hana dhambi anaogopa vipi ukaguzi..!!! Halafu anaomba awe kiongozi mkuu wa malaika.. Maajabu hayawezi kwisha
 
Ninaliona tatizo kubwa la ufahamu wa lugha ya kiswahili katika sakata hili.Ninachelea kufahamu kama kweli kamati walikuja na uamuzi huu kwa kigezo cha tasfiri ya kamusi au uelewa wa lugha yetu mama.Prof Assad hajatamtaka kwamba " BUNGE DHAIFU" alisema "NI MADHAIFU YA BUNGE".... kama neno MADHAIFU linaleta tafsiri ya goigoi,hafifu basi kuna sababu ya sisi waswahili kuanza kujifunza kiswahili cha kigogo,kinyakyusa na kisukuma ili tueleweke.Au la tukiri kwamba siku zote tumekuwa tukikitumia kiswahili ndivyo sivyo.Kwa uelewa wangu mimi kama mswahili ni kwamba neno MADHAIFU ni MAPUNGUFU.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya mambo ya kwanza kabisa tunayojifunza kama wazazi ni kubembeleza watoto. Mtoto anapozaliwa anakuwa ni mtegemezi mkubwa wa mzazi kwa kila kitu na pole pole anavyozidi kukua ndivyo anavyozidi kupunguza utegemezi huo. Lakini kama kuna kitu ambacho mzazi anaendelea kuwa nacho kwa mtoto ni nguvu yake ya kuweza kumuumiza mtoto kwa maneno au kumbembeleza. Ni nguvu kubwa sana kwa mzazi kuweza kumuita mtoto wake (hata kama ameshakua mtu mzima) na kumtuliza anapokuwa katika matatizo. Hili ni jukumu la kama mzazi na tunalipitisha jukumu hili kwa watoto wetu ili na wao wawe wazazi bora kwa watoto wao.

Hivyo, mzazi mara nyingi haumizwi sana na mtoto wake na anajifunza kumvumulia mtoto wake sana. Uvumilivu wa mzazi kwa mtoto wake nao ni mkubwa sana. Kama mzazi amemkuza mtoto toka anavyojimwagia kinyesi hadi makamasi basi mzazi anaweza kuvumilia mengi tena hata kwa mtoto mkubwa. Mtoto ambaye amekua na maisha yakamharibikia bado anaweza kupata uvumulivu kwa mzazi wake. Inapofika mahali mtoto anamuumiza mzazi hadi mzazi anaona ameshindwa kabisa kuvumilia jambo lile ndio hugeuka kile kinachoitwa "laana".

Ndugu zangu serikali na watumishi wa serikali si wazazi wa Watanzania. Uvumulivu au upendo wao kwa wananchi haulingani na wazazi na hawapaswi kututendea kama watoto wao au sisi kuwachukulia kama wazazi wa taifa. Wanasiasa na viongozi wa kuchaguliwa wote ni watumishi tu wa wananchi. Hawapaswi kuumizwa sana na maneno ya watu au matendo ya watu kiasi cha kukwazika sana.

Mojawapo ya mambo yananikera - na hili nimeshawahi kulisema mara kadhaa huko nyuma - ni kuwa viongozi wetu wasijione kama wao ni wazazi na hivyo wanataka watu wawabembeleze kwa maneno matamu. Sipendi kuona viongozi wako huru kusema lolote kwa yeyote lakini wao wakisemewa yale yale wanayoyasema wao wanajisikia kuumia. Hili la Spika na CAG ni mfano mdogo tu wa jinsi gani chombo kikubwa kama Bunge kinaumizwa na maneno! Hii ni fedheha! Yaani, kuna watu wameumia sana hadi kufanya kikao na kupitisha azimio kabisa kuwa wameumizwa! Huu ni udhaifu wa namna gani?

Wadudu kama nzi ni wasumbufu sana na wana madhara wakati mwingine; lakini hakuna mtu ambaye ana akili timamu ambaye anaamua kutumia gobole kuua nzi! Kuna mtu aliwahi kuishia kuchoma nyumba yake kwa sababu alitaka kujaribu kuua mende kwa kuwachoma na mshumaa! Kauli ya CAG hata kama angekuwa amemaanisha kabisa kuwa Bunge ni dhaifu (kwa utendaji na kwa namna ilivyo) bado haikuwa sababu ya msingi ya kumuita kujieleza wala kutumia muda wa Bunge kujadili! Huku ni kutumia nguvu kubwa kushughulikia jambo dogo; kujaribu kuonesha nguvu katika udhaifu!

Ni lazima tujifunze kuvumulia maoni hata kama yanaudhi sana. Viongozi au kiongozi ambaye hawezi kuvumulia maoni ni muhimu sana asitafute uongozi! Kutofautiana maoni au mawazo ni sehemu ya uhuru wa maoni na mawazo. Mwaka 2008 niliandika hapa kuwa haki ya maoni na uhuru wa mawazo vilivyomo katika Katiba haulindi maoni na mawazo mazuri! Haki hizi ziko kwenye Katiba kulinda maoni mabovu, ya kuudhi, ya kijinga na wakati mwingine ya kukera kweli kweli. Haya ndio maoni yanayolindwa kwa sababu maoni mazuri, ya kufurahisha na ya kutuliza mioyo hayahitaji kulindwa!

Nafahamu pia kuwa kuna watu kwa asili yao hawana uvumulivu; wanaumizwa sana moyoni wakipingwa, wanakwazika sana kuwajibiwa, na wanajisikia kutukanwa wakipingwa. Hili ni kweli hasa kama watu wana madaraka makubwa. Mwalimu akijibishiwa na mwanafunzi anajisikia amedharauliwa hata kama mwanafunzi yuko sahihi; polisi akikataliwa na raia kwenye jambo fulani anaona basi ngoja ampige kirungu! Ndio maana mojawapo ya misemo ya awali niliyoiasisi ni kuwa "hoja ijibiwe kwa hoja na si kwa vihoja". Mtu anapojibu hoja kwa vihoja anake ameshindwa hoja!

Hili la Spika na wabunge wenzake kutumia nguvu kubwa hata - naamini wakiwa timamu - kuamua ati kutoshirikiana na CAG ni ushahidi kabisa kuwa Bunge ni dhaifu, linajifedhehesha na limelewa ule ugimbi uleweshao wa madaraka! Wanaamini kabisa kwa kuwa wao ni wabunge na wako wengi basi wanaweza kufanya lolote, popote na kwa lolote kwa kusema kwa kauli moja tu "ndiyo".

Nani atawaambia ukweli huu bila kuonekana naye anawaumiza? Inawezekana basi kama taifa tuendelee kuwabeba kwenye mbeleko na kuwabembeleza wasiumie sana moyoni wakikosolewa, wasinung'unike wakikataliwa, na wasijisikie unyonge wakinyimwa! Tutakuwa na taifa la viongozi wa namna gani.

Sitaki hata kufikiria.
Ingawa hutaki hata kufikiri, lakini hebu fikiri kama iwapo bunge lingeamua kukaa kimya na kuuthitishia umma kwamba wao sio dhaifu kwa kutengeneza vigezo na vitendo vitakavyolifanya Bunge lisionekane dhaifu kwa watanzania.
Inasikitisha sana hawana na hawataki kuuthibitishia umma kwamba Bunge sio Dhaifu! Ubabe hauwezi kufuta Udhaifu au kujimwambafai hakutasaidia kitu. Ni wakati sasa wa Wabunge kujitafakari na kufanya tahajudi ya kuwathibitishia kwamba wao sio DHAIFU.
 
Back
Top Bottom