Bunge lamchunguza, Rais ampa zawadi

Bunge lamchunguza, Rais ampa zawadi

Buyaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
1,781
Reaction score
2,077
IK+%2822%29.jpg


Msahiki Meya wa Dar-es-Salaa, Didas Masaburi.
 
Inategemea ni zawadi ya nini. Fafanua, Ila nakushauri 'Acha vipofu waongozane', mwisho wake tutauona.
 
Yaani ina maana kwamba Bunge liache kumchunguza huyo swahiba wake katika madili waliyofanya au wanataka kufanya jijini Dar.
 
Inategemea ni zawadi ya nini. Fafanua, Ila nakushauri 'Acha vipofu waongozane', mwisho wake tutauona.

Bila kujali ni zawadi gani anayopewa huyu hakupaswa hata kukanyaga ikulu. Mbali ya tuhuma za ufisadi,juzi pia katutukana watanzania wote kupitia kwa wawakilisha wetu leo tunamwona kwenye ofisi yetu ya juu kabisa nchini akipeana mkono na mkuu wa nchi, is he being rewarded kwa kutuibia na kutuinsult?. Huu upuuzi I'm sure huwezi kuuona mahali pengine popote duniani zaidi ya Tanzania.
 
Kwa kuwa bado anachunguzwa hana hatia, mpaka pale itakapodhihirika kuwa ametenda kosa, kwa maana hiyo yuko huru kukutana na kila mtu hadi pale kosa lake litakapobainika.
 
Yaani ina maana kwamba Bunge liache kumchunguza huyo swahiba wake katika madili waliyofanya au wanataka kufanya jijini Dar.
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku
 
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku
acha mchezo na rafiki mnafiki
 
Hamkuelewa kile alichomaanisha Hosea wa takukuru mbele ya balozi wa Marekani bado?
.
 
Sasa wa kumlaumu nan masaburi au aliyempa zawadi masaburi kwa kufikiria kupitia masaburi?
 
Unatarajia nini kutoka kwa kiongozi mahiri mzururaji? Wa Tatanzania hiyo ni miaka yenu ya kuumia. mpaka mshike adabu kwa wrong choice ya uprezida
 
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku

Vipi na wewe ulipewa?
 
Kwa kuwa bado anachunguzwa hana hatia, mpaka pale itakapodhihirika kuwa ametenda kosa, kwa maana hiyo yuko huru kukutana na kila mtu hadi pale kosa lake litakapobainika.
Kama ukiwa na kashfa huna hatia mpaka itakapodhihirika, mbona Katibu Mkuu Jairo kaambiwa asikanyage wizarani?
 
Nilikuwepo kwenye hafla hii, ni siku aliyofuturisha, wanaume walipewa mifuko hii ikiwa na vikoi na supande wa wanawake mama salma aligawa zawadi ya aina hii ndani kukiwa na vitenge. Ni zawadi ya futuru.. Ila kwangu mimi sioni kama ni sadaka kwani anawaridhisha matajiri amabo hata hata hivyo vitu hawatavitumia, wanaweka makabatini tu.. Ni bora angeamua kufuturisha wale wasiojiweza , wenye shida hata ya kg 1 ya unga kwa siku
MASA BURI bado ni Meya na anawakilisha jamii. HAFLA hiyo ilikuwa jijini dar so kama meya lazima aalikwe ikulu that is protocal; angekuwa amepewa barua ya likizo ili kupisha uchunguzi kisha mr president akampa mwaliko hiyo ni kesi ingine. msimamisheni kwanza!!!!

"DONT MAKE OTHER PEOPLE LAUGH AT YOUR BACK"
 
Katibu Mkuu Jairo kaambiwa asikanyage wizarani?

Jairo wizarani ni kazini kwake na amesimamishwa kazi, vipi ukiacha kutumia Masaburi yako kufikiri unadhani Masaburi amesimamishwa kazi yake au Ikulu ni ofisini kwa Masaburi?
 
Inawezekana kabisa Mayor Masaburi akawa hana hatia,ni mtu safi, lakini kwa kipindi hiki ambacho yuko kwenye uchunguzi si busara hata kidogo kuonekana kwenye hiyo picha na Rais. Psychologically inampa Mayor Masaburi nguvu kubwa sana.

Kitu kingine ambacho kinanipa shida ni nani analipia hizi futari za kila juma? Nauliza hili kwa nia njema kabisa, na natambua hiki ni kipindi muhimu kwa waislam na nilitegemea Rais angefutarisha watu lakini (LAKINI) sikutegemea angefutarisha kwa kasi hii. Nchi masikini ambavyo inakopa kila kukicha kwa nini Rais anashindwa kutambua concept ya 'kubana matumizi'?.

Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi nusura ikwame kwa sababu ya kukosa fedha, Raisi yeye anazo mpaka za kununua zawadi kwa Watuhumiwa wa rushwa? Umpe mtu chakula na zawadi pia? Washauri wa Rais wanafanya nini? Kwanza mmeona hiyo mifuko ya zawadi? ni kiasi gani mfuko mmoja? Hawa waliofutarishwa wana njaa gani mpaka wapewe chakulana Rais?.

Kama ni lazima kufutarisha kila juma basi wafutarishwe watoto yatima na wasukuma mikokoteni. Hawa ndio wanataka chakula lakini sio wakina Mayor Masaburi.

Sijui tumefikaje hapa. Sijui!
 
Back
Top Bottom