BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.
BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.
Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.
Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.
Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi.
Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.
Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wananchi juu ya hatua hiyo.
Watu wa namna ya huyu Katibu wa Bunge,Thomas Kashilila, wana sifa zifuatazo:-
1. Udokta wao ni ule wa kudesa au kupewa kama Mkuu wa Kaya.
2. Teknolojia ya habari na mawasiliano wameionea ukubwani au madarakani.
3. Hubeba madaraka ya nyumbani kwake na kuleta Kazini.
4. Kwenye familia zao watoto hawana haki ya kuwasha TV mpaka baba arudi toka kazini.
5. Wanategemewa sana na ukoo mzima mpaka kujiona wana mamlaka ya kufanya chochote au kusema lolote kama Mungu Watu.
6. Hawana exposure ya kutosha kwenye masuala ya Uongozi na utendaji yaani wamezoea mfumo wa aina moja.
7. Wamekulia katika familia zenye mfumo wa ukandamizwaji, unyanyaswaji, unyamazishwaji na ukoloni.
8. Wana mtandao wa Ufisadi wenye hofu ya kugundulika maovu yao.
9. Waoga na wenye hofu ya mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
10. Wababaishaji na vibaraka wanaojipendekeza kwa watawala kwa maslahi binafsi.