Bukoba tumebaki analogi

Bukoba tumebaki analogi

Tena wote wa kagera...huyo byabato na makamba mama yake wa misenyi...

Bado waziri wa tamisemi anayehusika na halmashauri ni wa karagwe lakin hata kushawishi stendi ya bukoba ijengwe hawezi..
Noted
 
Poleni sana wahaya..

Kumbe mna hali mbaya namna hiyo.
Niliambiwa eti hata hapo stendi ya mkoa kinapigwa kihaya tupu, ukiwa mgeni shida sana kama hujui kihaya vipi ni ya kweli hayo??
 
Kagera inabebwa na muleba,misenyi na karagwe...lakin bukoba imeisha kabisa
Kwa hili hapana. Tuko Pamoja bila kujali mtu anatoka Muleba, Misenyi, Kyerwa, au Karagwe. Wote tunataka Bukoba Mjini pawe sehemu ya kuvutia. Stand ile ijengwe vizuri, solo libomolewe lijengwe la kisasa na hospitali pia. Ifike muda serikali kama haitaki kuendeleza Kagera kwa ujumla, itwambie au ituruhusu tujiunge na nchi jirani tutakayo chagua au tuanzishe 'Jamhuri ya Rweru'.
 
Ng'oa hizo bati...ukipakana au ukiwa jirani nao ni full kero na migogoro.
Ni jamii fulani ya hovyo sana yaani mtu umuachie sehemu na yeye ana sehemu kubwa kwa mbele but still anakuchokoza anajenga nyumba maji ya mvua anayaelekeza kwako.

Ni kwamba ananimudu sana au vipi?huwa najiuliza maswali mengi sana nakosa majibu,huyu nataka nifukishane nae kwa mjumbe.
 
Kwa hili hapana. Tuko Pamoja bila kujali mtu anatoka Muleba, Misenyi, Kyerwa, au Karagwe. Wote tunataka Bukoba Mjini pawe sehemu ya kuvutia. Stand ile ijengwe vizuri, solo libomolewe lijengwe la kisasa na hospitali pia. Ifike muda serikali kama haitaki kuendeleza Kagera kwa ujumla, itwambie au ituruhusu tujiunge na nchi jirani tutakayo chagua au tuanzishe 'Jamhuri ya Rweru'.
Duh! Umekereka kweli mkuu.Nashukuru kwa mchango wako.Wakora waitu
 
Co kweli ubinafsi mji inajengwa na wagen miii yote ambayo hawataki mgen afanye biashara haiendelei.

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
Stendi zinajengwa na wageni? Barabara zinajengwa na wageni? Masoko yanajengwa na wageni? Acheni ubinafsi mada inaongerea public seveces.
 
Kwa hiyo mkuu tuki-calculate ndani ya hii miaka 60+ ya uhuru na kunavyoonekana sasa itaibidi Kagera japo kwa uchache kuchukua tena miaka mingine siyo chini ya 80 ili iifikie au iipite Moshi au Arusha?

Viongozi wenyewe ndiyo hivyo hovyo hovyo tu siyo raisi siyo wabunge siyo wakurugenzi wote wanajali kushiba kwao na familia zao hawafanyi kile walipaswa kufanya ndani ya serikali.
Arusha na Moshi zina mazingira tofauti kabisa na Bukoba au Kagera nzima. Kaskazini kuna mzunguko mkubwa wa fedha na vyanzo vingi vya mapato. Mlima Kilimanjaro unaleta mapato mengi, pale Arusha ni soko la madini, utalii mwingi unapita mikoa hiyo. Kagera mkoa una resources ambazo hazijaguswa ni kitendo cha kutokea sera za maana zilizosimama na viongozi sahihi miaka mitano tu mkoa unakuwa level za juu.
Nimeishi Moshi nikazuru Arusha, Arusha ni jiji ila tofauti ya Moshi na Bukoba kwa maendeleo ni ndogo wala hakuna widening of gap.

Kwanza hakuna umaskini kivile, tatizo ni ukosefu wa vyanzo vya mapato. Nimezaliwa Bukoba na kusoma uko O level sijawahi kuona tractor wala combine harvester, nimekuja kuyaona mikoa mingine. Sikuwahi ona mtaalamu wa kilimo wa serikali uko, sikuwahi ona pembejeo zinatolewa na serikali, ule mkoa ni semi autonomous ndio maana wana jeuri ya kutukana Rais kwenye kampeni maana hawamtegemei kwa lolote. Serikali au viongozi wakiamka wakaweka sera nzuri ambazo hata sio gharama kubwa utashuhudia kilimo cha kahawa kinakua haraka sana, vannila, parachichi, ndizi. Hivyo vyote wala serikali haihitajiki kutoa hela.

Mkoa unaishi kwa remittance kutoka mikoa mingine, sio kama Shinyanga wanaouza madini nje wakawa na hela za nje nje ukienda kuuza hata mitumba au viatu unapata wateja. Mtwara wakiuza korosho ukienda kuwauzia simu wananunua, Kagera mwaka mzima hauna msimu wa hela. Hawafi njaa ila hawana hela. Mipaka yenyewe ndio hiyo yenye migogoro, wakati Arusha wamepakana na Kenya yenye mahitaji tofauti na Tanzania, Kagera iko na Uganda ambao bidhaa zao na za Kagera ni zilezile. Utatoka Songea upite Arusha uuze mahindi Kenya, uliwahi sikia bidhaa yoyote ya msingi tunaiuza Uganda? Bidhaa za Uganda zina bei nafuu wakati hawana bandari, nguo zinanunuliwa China zinapita Mombasa zinaingia Uganda tunaenda zinunua Mutukula ya Uganda kwa bei nafuu kuliko zinazopita bandari ya DSM. Humu JF kuna nyuzi za biashara na Uganda, katafute kama kuna mjadala wa exportation, badala yake ni importation kutoka Uganda. Majirani wengine ni Rwanda na Burundi, tuna majirani wa hasara wao muda wowote wanatuletea wakimbizi, majambazi, wagonjwa wa Ebola, Zika virus na UKIMWI. All of them they don't have purchasing power.

Kagera ina disadvantages kuendelea ila inahitaji serious efforts kidogo. Kwanza umbali wenyewe tatizo, mtu utabeba mbao, ng'ombe, maziwa, mazao kutoka kule. Gharama za usafirishaji ni kubwa unatafuta alternative eneo la karibu, kule hakuna reli. Kama demand ni ndogo na uzalishaji ni mdogo
 
Huko ni uganda kwanza wanahofu mtarudi kwenu mtakimbia nchi.
 
Alafu eti Rais Samia anakuja tarehe 8 kuzindua msikiti!!! Hii nchi haiishi vituko, yaani hamna hata mradi wowote uliotekelezwa Kagera zaidi ya msikiti na mradi wa maji kyaka.
 
Ukiangalia hali ya mikoa na wilaya vinavyobadilika unaona kabisa Bukoba tuliachwa analog kila kitu Bukoba tuko nyuma sio stendi kuu sio soko kuu sio hospital sio vyuo vikuu yaani hatuna chuo kikuu ata kimoja mkoa mzima lakini ni mkoa umaoongoza kwa kuzalisha wasomi walioolowea ughaibuni.
Wasomi wasio na faida kazi ni kutujazia makaburi. Naandika kwa hasira ivi WAHAYA nani aliyewaloga? Yaani Mbunge anakarabati soko zee kwa kuezeka na bati za SENENE? Tumezidiwa na mshenga wa Yesu Mzee wa Kaprnaum?
Sijui CCM mtajibu nini kwa Muumba, kodi mnachukua hospital hakuna madawa shule hizo usiseme barabara mitaani hoi sijui narudia sijui.
Namaliza kwa kusema ABAHAYA inywena mweshubeho Kagera yagera.View attachment 2250488View attachment 2250490View attachment 2250489View attachment 2250491View attachment 2250492
majigambo yamewazidi hahahahaha
 
Wahaya wengi hawawekezi kwao ila wanaenda kule kujaza makaburi tu kama ni mabadiliko muanze nyie wenyewe

Uzuri nimeishi kule kwa miaka 4
*Wahaya muache umimi usisi na kujiona
*Muache uvivu na ulevi
*Muache ubishi linapokuja suala la maendeleo

NB:kwa mara ya kwanza mkoa wa kagera nimeona taxi inabeba watu 13
Khaaaa hv Wahaya walivyo na sifa mjini kumbe kwao shida tupu
 
Nachojua pale Bukoba mjini ni pa hovyo kuanzia miundombinu kama barabara, stand, soko na majengo mengi pale mjini ni ya kizamani....

Ila ukienda kule vijijini watu wamejenga sana nyumba za maana kuliko vijijini vingi vya mikoa mingine.

Kuna haja ya kufanya jitihada kubwa kama wahaya kwa kushirikiana na serikali kuhusu pale Bukoba mjini
 
Alafu eti Rais Samia anakuja tarehe 8 kuzindua msikiti!!! Hii nchi haiishi vituko, yaani hamna hata mradi wowote uliotekelezwa Kagera zaidi ya msikiti na mradi wa maji kyaka.
Mimi mwenyewe nashangaa....nilitegemea aje kuzindua mradi wa ujenzi wa stendi
 
Ninae mmoja jirani yangu alisogeza mpaka nikataka kufanya ujenzi wa ukuta nikamuita tunyooshe vizuri akaniambia yeye hana aliposogeza na kwamba mpaka ulivyo ndo ulivyotakiwa kuwa nikaachana nae nikajenga hivyo hivyo.

Week mbele nimeenda kazini narudi nakutana na samansi naitwa mimi serikali za mitaa kwamba nimesogeza mpaka wa jirani,nikiwa natafakari akatuma mtoto akisisitiza nisikose kuhudhuria maana baba amedhamiria kufika mbali siku ya kesi tukaenda eneo la tukio kilichoniokoa mjumbe aliyesimamia wakati nanunua alikuwepo na niliweka kwa mkono wangu alama ya nondo nilizichimbia chini akanikumbusha siku ile uliweka alama zako ziko wapi kuangalia zipo upande wake.

Sasa amejenga nyumba maji ya bati zake yanamwagikia kwangu kuna wakati huwa najiuliza kwamba mimi mpole sana au naonekana akili sina?
Yaani Hawa ndugu zetu Ni Shida!Inatakiwa kwenda nao kiubabe ubabe alianza hizo chokochoko zake simama imara piga biti balaa,ukiwa mpolempole unaweza shangaa siku anakuita ukamfulie nguo zake....Nina jirani muhaya pia tumeshamalizana kila mtu kakaa kwa kutulia sasa
 
Miaka ya nyuma kidogo, nilikaa Bukoba wiki 3.Kuna sehemu nilikuwa nanua gazeti Kila siku!
Kuna siku nilienda nikiwa nna Sh.5000/=Yule muuzaji aliniambia Hana chenji,awali nilifikiri anatania,Kwa kuwa yulishazoeana nikaona anasisitiza! Kuwa Hana Hana 4000/= ya kunirudishia chenji!
Nilistaajabu sana!
Bahati Mbaya pale mjini kulikuwa na Vituo 2 Yu vya kuuza magazeti! Kike Cha pili nilikosa !
 
Back
Top Bottom