Salaam wana jamii,
Nachukua nafasi hii kumpongeza katibu wa BMT kwa utendaji wake katika kuongoza taasisi hii nyeti kwa jinsi alivyoweza kuandaa mikakati ya kuthibiti undanganyifu uliozoeleka katika mitihani ya taifa kuanzia mitihani ya kidato cha pili hadi ya kidato cha sita.Wote ni mashahidi wa hali mbaya ya udanganyifu wa mitihani ulivyokuwa umekithiri kiasi cha kuziona paper za mithiani zikizagaa mtaani.
Sasa huyu mama ameidhibiti hali hiyo,jamani tumuunge mkono na wala kamwe tisimkatishe tamaa. Matokeo haya ya mitihani ya kidato cha pili na ile ya kidato cha nne yanaakisi hali halisi ya udhibiti wa mitihani inayofanywa na bosi huyu mwanamama na timu yake.
Tisimlaumu kwa kushindwa kwa wanafunzi kwani yeye siye msimmamizi wa sera za elimu nchini yeye kazzi yake ni kuandaa upimaji.
Huu ndio mtizamo wangu
lengo la mtihani wowote ule ukiwemo hata huu wa NECTA ni kupima kama mwanafunzi amepata maarifa, ujuzi, stadi na maelekeo yaliyokusudiwa katika malengo makuu na malengo mahsusi ya elimu, yatakomwezesha mhitimu kuwa na badiliko chanya la kudumu linalopelekea aweze kuyamudu maisha na mazingira yake.
Kama wanafunzi wakifeli, basi ujue moja kwa moja kuwa malengo makuu na mahsusi ya elimu hayakufikiwa, yaani kwa lugha rahisi ni kwamba, wanafunzi hawakupata maarifa, ujuzi, stadi na mielekeo(tabia) ya iliyokusudiwa.
Kwa hiyo kumpongeza Joyce Ndalichako si sahihi hata kidogo.
Ili mwanafunzi afaulu mtihani basi awapo ndani ya chumba cha mtihani anahitaji awe na:-
(Knowledge, skills, attitude) + Speed +Accuracy.
Cha kujiuliza ni je, wakati wanafunzi wanafanya mtihani kichwani walikuwa na package kamili? Na je waliandaliwa kikamilifu kimaarifa,Ujuzi, stadi na kitabia/mwelekeo wa kumudu kufaulu mtihani na baadae maisha halisi?