Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Salaam wana jamii,
Nachukua nafasi hii kumpongeza katibu wa BMT kwa utendaji wake katika kuongoza taasisi hii nyeti kwa jinsi alivyoweza kuandaa mikakati ya kuthibiti undanganyifu uliozoeleka katika mitihani ya taifa kuanzia mitihani ya kidato cha pili hadi ya kidato cha sita.Wote ni mashahidi wa hali mbaya ya udanganyifu wa mitihani ulivyokuwa umekithiri kiasi cha kuziona paper za mithiani zikizagaa mtaani.
Sasa huyu mama ameidhibiti hali hiyo,jamani tumuunge mkono na wala kamwe tisimkatishe tamaa. Matokeo haya ya mitihani ya kidato cha pili na ile ya kidato cha nne yanaakisi hali halisi ya udhibiti wa mitihani inayofanywa na bosi huyu mwanamama na timu yake.
Tisimlaumu kwa kushindwa kwa wanafunzi kwani yeye siye msimmamizi wa sera za elimu nchini yeye kazzi yake ni kuandaa upimaji.
Huu ndio mtizamo wangu
Kama suala la kuvuja mitihani lipo wazi hivyo anajitia kitanzi kwa vile ndiye mwenye dhamani na taasisi hiyo, nawajibika kuthibiti hayo hiyo. Hakuna mwenye jukumu la kuthibiti hali hiyo isipokuwa taasisi yake na yeye akiwa ndiye mshika usukani.