Brand New I Phone 5!, Bei Poa, ya Kutupa! Ni...Laki Tatu Tuu!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,503
113,616
Wanabodi,

Juzi usiku nikiwa bar fulani maarufu karibu na Mlimani City, jamaa aliniafuata mezani na kuniambia kuna mzigo wa I Phone 5 pieces 2, na I Phone 4s pieces 3 umeibwa Mlimani City!, na bado uko ndani ya box zake na hazijafunguliwa!. Unauzwa kwa bei poa!.

Uko wapi?, nikatolewa nje na kupelekwa kwenye gari fulani hapo nje, nikakuta hizo I phone 5 simu mbili na I Phone 4S simu tatu!, ndipo nikaonyeshwa hiyo I Phone 5!. Kwa masikini mimi siijui hata hiyo I Phone 5 ya ukweli, nikamuomba aifungue niione!. Jamaa kwanza akagoma kuwa kwa vile ni brand new, iko sealed kwenye box yake, akasema ili aifungue, lazima nionyeshe I'm serious buyer, asije kuifungua halafu nisinunue, mara akaifungua nikaishangalia!.

Bei ya kuanzia ni 1.5!, akanielekeza dukani pale kwa Mama Dubai ni 1.8, na maduka mengine ni mpaka 2.2!. Kiukweli kwa mwandishi wa habari wa bongo, 1.5 ni mshahara wa robo mwaka!. Nikamwambia asifungue maana huko sifiki hata nusu!. Akanishauri basi ninunue zile 4S na moja ilikuwa imefunguliwa!.

Akaniwashia nikaitest kwa bluetooth nikathibitisha its genuine!. Hiyo 4s akasema dukani inauzwa laki 8, yeye anataka laki 6 tuu!. Huko nako ni mbali sifiki, nikamshukuru nikarudi ndani kwenye kinywaji changu!. Jamaa akanirudia, na kuniuliza nina ngapi, maana jamaa ndio kwanza ametoka kukwapua, hivyo hana kitu na atakubali kwa bei yoyote!.

Tukakubaliana I phone 5 kwa laki 5!, sijui jamaa anatumia dawa!, mara nikaanza kujisachi nilichonacho, tena nina bahati, siku hiyo nimetoka kupiga deal heavy na TPDC mtambo wa gesi Kinyerezi, "libahasha lake linene" nimesha tumia tumia hapa na pale, na kuwarushia rushia kwa m-pesa akina ninii wote, sasa nilikuwa nimejikalia bar kujipongeza hivyo nilikuwa "loaded"!.

Nikajikung'uta kung'uta nilicho nacho haikufika laki 5!, nikamwambia twende kwenye ATM ya karibu nijazie!, jamaa akaonyesha ana haraka,akaniuliza kwani zimepatikana ngangapi, nikamwambia 380,000 jamaa akasema lete tuu hata hizo hizo, kwasabu yeye hakuingia gharama yoyote!, nikamlipa nikakabidhiwa I phone 5 yangu Brand New, "Original!" ndani ya box yake kwa 380,000 tuu!. Akaniambia kama nina pesa mahali, ile I phone 5 ya pili anaweza kuniuzia kwa laki 3 tuu na zile I phone 4s atanifanyia kwa laki mbili mbili!.

Duu!, nikaona hii ni big deal!.Kimoyo moyo nikaanza kufurahi na kujifariji kuwa inaweza mimi nikawa ndie mwandishi wa habari wa wa kwanza hapa bongo kumiliki I phone 5! (niliwahi kuwa mwandishi wa habari wa kwanza bongo kumiliki pikipiki!),

Kufika home, nikamweleza wife na kumwambia kesho namnunulia na yeye!, na watoto wetu watatu wakubwa (tunao 6), kesho tunawanunua zile 4s!. Kama tumeweza kuwanunulia I pod na games za PSP!, kwa nini tushindwe kuwanunulia simu nzuri za I phone?!.

Niicharge I phone yangu, nika iwasha ili kui sinc na MacBook yangu, duu!, nikashangaa hazionani!, kujaribu camera, nikakuta ni utumbo mtupu, kwenda kwenye I tunes, haiendi!, nikawasha tena bluetooth ku browse computer yangu, ikagoma ku pair!, ndipo sasa nikafunguka macho!...yaani hata mimi?!. Kumbe nimeingizwa mjini hivi hivi huku najiona!. Hivi sikustuka jamaa kaanzia 1.5 na kushuka mpaka laki 3, na mimi nimeendewlea kupelekwa tuu kama ling'ombe!. Inawezekana hawa jamaa wanatumia dawa?!. Ila kiukweli huyu Mchina sasa ni mwisho!, kama huijui the "original" thing!, you can't tell a difference!.

Swali kwa mnaoijua I phone ya ukweli, ina nini cha ziada mbona hii ya mchina ina karibu kila kitu?!.
Nimechaki bei ya I phone 5 ya ukweli kwenye net ni $ 199 (16gb), $299 (32gb) na $399 (64gb), nini kinachoifanya hii I phone 5 iuzwe kwa milioni 1.8 hadi 2.4 maduka ya hapa kwetu!?.
Pasco.
 
Pole kuingizwa mjini Pasco. Unategemea bila watu kama wewe matapeli watapata wapi maisha bora kwa kila mtanzania?
 
Hahahahahahahahahha mkuu nacheka nmekumbuka jambo lingine tofauti na mada.. Nmekumbuka kile kipindi chako hivi kilikuwa kila j5 cz siku nyingi.. Nways pole.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Pole kuingizwa mjini Pasco. Unategemea bila watu kama wewe matapeli watapata wapi maisha bora kwa kila mtanzania?
Jamaa wana dawa ya kumjua mtu mwenye cash mfukoni!, siku hiyo ndio nimetoka kupiga deal kubwa la TPDC kule Kinyerezi, yaani fungu hata halikufika home, japo akina nanii wao walishapata ka mgao chao kwa kuwatumia kwa m-pesa, fungu la home ndilo lililokuwa kubwa na halikufika!.
 
Hahahahahahahahahha mkuu nacheka nmekumbuka jambo lingine tofauti na mada.. Nmekumbuka kile kipindi chako hivi kilikuwa kila j5 cz siku nyingi.. Nways pole.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Thanks. Kipindi kilikuwa J.5 ila nategemea kurudi hewani Jan, 2013!. Nitarudi kivingine kidogo na kiutu uzima zaidi kuelekea 2015 ndio nastaafu rasmi!.
 
Duh!, ila kweli juzi nilimkimbiza jamaa alitaka kuniuzia samsung galaxy s3 kumbe mchina mana kwa kuitazama hivi huwezi kataa kama si s3.....
 
Mkuu Pasco Pole!

Kwanza una bahati umepata ya Kichina! ... wengine baada ya kufungua hukuta mche wa Sabuni.

To stay safe always be alert, keep aware, and think twice before accepting any deal too good to be true. The best scams are the ones that don't feel like scams, so always double check yourself.
 
Thanks. Kipindi kilikuwa J.5 ila nategemea kurudi hewani Jan, 2013!. Nitarudi kivingine kidogo na kiutu uzima zaidi kuelekea 2015 ndio nastaafu rasmi!.

Nakisubiri kwa hamu. Hpe kitakuwa pale pale mtaa wa zaramo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mjini shule vizuri vinagharama...mkome kabisa!

MYTAKE
Hizo simu ziko za aina mbili line phone na card phone..Kwa Tanzania hatuna mfumo huu tunatumia zaidi card phone.

Line phone inauzwa kwa bei cheee au sehemu nyingine ni bure unachukua ila kuna kuwa na contract mara nyingi huwa ni 2 yrs contract unachukua simu kutoka company husika ila unatakiwa ulipie bill kila mwezi kulingana na kiasi walichokiweka kwa mf.dollar 100 kila mwisho wa mwezi utumie au usitumie lazima ulipie..na ikitokea ukatumia ikidizi lazima ulipe zaidi ya hiyo bei mbayo biill wamekuletea ndiyo maana ukitafuta kwenye mitandao ndiyo utaona hiyo simu ni bei chini na sehemu nyingine wamekwambia free phone..but reality its super expensive..mfumo huu haujafika Tanzania huko kwenye nchi zilizokwisha endelea

Card phone kwa kwetu ndiyo tunaita GSM.hizi simu unanunua kwa lapsum..hakuna bill ndiyo maana unaona bei zake ziko juu..(prepaid phone) na hakuna haja ya vitambulisho.

 
Duh!, ila kweli juzi nilimkimbiza jamaa alitaka kuniuzia samsung galaxy s3 kumbe mchina mana kwa kuitazama hivi huwezi kataa kama si s3.....
Mimi niliitest mpaka blue tooth yake ika read I phone 5!. Japo nilipoona inaingiza sim card ya kawaida wakati Apple lazima sim card ikatwe!, jamaa akaniambia kwa I phone 5, apple wametoa simu zinazoingiza smn kard ya kawaida bila kukata!, nilitakiwa nishtuke..lani wapi?.
 
Nakisubiri kwa hamu. Hpe kitakuwa pale pale mtaa wa zaramo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Nataka nianze na TBC ndio the cheapest, then kitakuja ITV na Star TV, kita run stations 3 kwa kuanzia, sponsors wakiongezeka, kitaenda na Zaramo, Mawingu na hata kukivusha bahari!.
 
Mimi niliitest mpaka blue tooth yake ika read I phone 5!. Japo nilipoona inaingiza sim card ya kawaida wakati Apple lazima sim card ikatwe!, jamaa akaniambia kwa I phone 5, apple wametoa simu zinazoingiza smn kard ya kawaida bila kukata!, nilitakiwa nishtuke..lani wapi?.
Mkuu sio Apple zote lazima ukate line, hata Iphone 3Gs hukati line. Jambo jingine hizo bei za Iphone 5 ulizoquote mitandaoni sidhani kama ni sahihi.
 
Pole Pasco.
Lakini kikubwa zaidi ni kwamba umewaokoa wanajamvi wengi sana ambao wangeingia kwenye mtego huo.
Shukrani.

Binafsi kwa mimi sina uzoefu wowote na utambuzi wa simu orijino na feki, ila kwa ishara ya bei hiyo mkuu ulitakiwa kustuka.

Kama haka kasimu kangu tu ka Samsung GT-S6802 kanauzwa kwa kilo nne ingekuwa Iphone 5 iuzwe bei hiyo, hata kama ni ya wizi?
Huu ni mkasa unaoweza kumpata mtu yeyote, na kila siku watu wanalia.
Lakini maisha ni lazima yaendelee.
 
Bei za iphone 5 ni hizo alizokutajia ambazo retails, Hizo ulizoona za dola 199 ni kwa wale wanaonunua under plan za makampuni ya simu na inakuwa locked kwa line ya kampuni moja tu

Never buy a cellphone mtaani!
I phone ya ukweli utaijua kwa display yake crystal clear, Ingia apple store haraka uone kama ina kupeleka apple store, check about the phone uone model number na operating sytem zake

Bei ikiwa rahisi sana dont buy it!!!
 
Mjini shule vizuri vinagharama...mkome kabisa!
Ni kweli na nakubaliana na wewe, kwenye maisha kuna "needs" na "wants" na vyote ni mahitaji!. usafiri ni "need" na choice ya usafiri, miguu, boda boda, bajaji, daladala au personal car ni "want", kuna wengi ambao wanautumia usafiri wa dala sio kwa sababu wanapenda, bali kwa sababu ya shida, wangekuwa na uwezo, wote pia wangependa kutumia usafiri wa magaria yao wenyewe!.

Vivyo hivyo kwenye simu na vizuri vingine, nako kuna "needs" ya hand set na "wants" ya iphone, samsung au nokia ya tochi. Sio wote wanaotumia Nakio ya tochi, wanaitumia kwa sababu wanaipenda, bali wakijikuna hapo ndipo wanapofikia!. Na mimi nimekuwa nikitumia kasimu changu fulani kwa sababu ndipo nilipofikia!. Sasa baada ya kutoka I phone 5, inaelezewa kuwa ndio simu bora kuliko zote, na kwa kawaida huwezi kuifikia, ikitokea ikauzwa kwa bei poa unayofikia, si unajikuta una kwangua hata kaa akiba chako chote ili na wewe angalau umiliki kitu bora?!.

Sijutii juhudi zangu kutaka kumiliki I phone 5 bali naisikitikia akiba yangu yote niliowekeza kwenye I phone 5 nikidhania nimepata kumbe ..!.
 
Back
Top Bottom