Box Office battle: Avatar Vs Avengers

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,681
106,794
1615916376140.png

Wapenzi wa movie😅😅😅
Tulishachotwa akili kweli na hawa watengenezaji wa muvi. Hivi lini bongo movie tutafika huku..walishawahi kupata hata Tsh 10Mil???.
Issue Ipo hivi....
Muvi ya Avatar ilitoka 2009 ikashika rekodi ya kua muvi iliyoingiza pesa nyingi zaidi duniani baada ya kuvunja rekodi za Titanic na Lion King (1992)

Mwaka 2019 ndio ikatoka Avanger Endgame ikavunja rekodi ya Avatar kwa kupata Dollar 2.797Bilions, sasa bwana wiki iliyopita Director wa Avatar David Cameron akasema anahitaji $Mil 7 tu aweze kuivunja rekodi ya Endgame. Avatar ikaonyeshwa tena huko kwa Xi Jiping akapata $12.3Milions kwa siku mbili. Kafikisha kiasi cha Dollar 2.802Bilions.

Hivyo avatar imerudi kwenye rekodi yake ya muvi iliyoingiza pesa nyingi zaidi duniani..

Mashabiki wa Marvel Studio/Marvel Cinematic Universe nami nikiwemo😅😅 wanawashinikiza Director wa Avanger Endgame Joe na Anthony Russo na producer wa Marvel Studio Kevin Feige waionyeshe upya muvi warudi kwenye rekodi yao.

Kweli vita ya panzi ni furaha ya kunguru, Marvel Studio inayomiliki Avanger Endgame ni kampuni tanzu iliyonunuliwa na Disney Company...Lakini pia kampuni inayosambaza muvi ya Avatar ambayo ni 20th Century Fox nayo inamilikiwa na kampuni ya Disney Company. So technically faida yote inaenda kwa Disney wakati sisi huku tunaparuana macho😆😆
FB_IMG_16159148568343028.jpg
 
Hawa jamaa wanajua kutengneza movie,imagine nilikuwa naangalia hiyo avatar siku moja,mzee wangu mwanzo akanicheka,na kebehi juuu “yaani wewe na ukubwa wote unaangalia cartoons”,ehehe siku hizi anaangalia mpaka Tom and jerry,anasema dah “kumbe ni mtazamo tu,kumbe sisi hatukufaidi”
Full kumsumbua “alexa” siku hizi😉😉
 
Hawa jamaa wanajua kutengneza movie,imagine nilikuwa naangalia hiyo avatar siku moja,mzee wangu mwanzo akanicheka,na kebehi juuu “yaani wewe na ukubwa wote unaangalia cartoons”,ehehe siku hizi anaangalia mpaka Tom and jerry,anasema dah “kumbe ni mtazamo tu,kumbe sisi hatukufaidi”
Full kumsumbua “alexa” siku hizi😉😉
Anayezibeza cartoons namuhurumia tu.. Kuna animation nzuri sana na realistic like movie. Hawajajua kwanini animation zinapiga pesa ndefu Zaid
 
timu avengers hapa wa kufa na kuzikanana yaan mpak DC wakitoa kitu kikali moyo unaniuma wakitinyanga nafurahi kinoma
Binafsi nahisi nikioewa mtihani wa MCU naweza score B kama sio A. Hua nasoma maComics kabisa.
DC kwa muvi hawawezi kutufikia kwa muvi hata wafanyaje wanatudhinda kwenye series, animation nk. Ila kuanzis mwaka huu tutawashinda vyote...
Ili nishabikie mpira labda MCU ife😅
 
Character ya Captain America inanfanana na Jon Snow..wote wanajali na kupenda haki na utu. Ndio character naopenda kuishi kama wao

Binafsi nawapenda
Doctor Strange
Thor
Captain Marvel
Black Panther
daa umenikumbusha watu wangu wa nguvu
Lannister family wajanja wajanja na wana strategy za maana kuna little finger anakuchoma muda wowote king Joffrey moto mkali afu mutu mubad Ramsay Bolton hahaha ngoja nikaipakue nianze season 1 kabisa

#what is dead may never die
 
Binafsi nahisi nikioewa mtihani wa MCU naweza score B kama sio A. Hua nasoma maComics kabisa.
DC kwa muvi hawawezi kutufikia kwa muvi hata wafanyaje wanatudhinda kwenye series, animation nk. Ila kuanzis mwaka huu tutawashinda vyote...
Ili nishabikie mpira labda MCU ife😅
Kwanini vision alibadikika na kuwa kama binadamu wa kawaida
 
Kwanini vision alibadikika na kuwa kama binadamu wa kawaida
Baada yaBruce na Tony kupata ile Stone aliyokua anatumia Loki kubadiriaha watu Tony aliichunguza akaona ipo kama alogalithm Tony akamuomba Bruce amsaidie kutengeneza Artificial Intelligence nyingine iitwayo Ultron kwa kutumia stone ya loki.

Baadae AI ya Ultron ilienda kinyume/Rogue ikachanganya Jarvis na Ultron kua kitu kimoja. Kumbuka mwanzo wa Avanger Age of Ultron Balton alipigwa risasi (?) ubavuni akaitwa doct Heren kutoka Korea ambae alikua anaweza kuotesha Tissue through cellular regeneration kwa muda mfupi Barton akawa amepona.

Ulton nae alimfuata doctor heren atengeneze mwili Artificial kwa kuotesha Tissue kweye mitambo ili Ultron apakie mind/AI kwenye huo mwili awe kama binaadamu. Baadae Cap na Wenzie waliziwia hilo Jarvis ndio akawa Uploaded kwenye mwili huo.
Sasa ule mwili uliotengenezwa ulikua unaEvolve taratibu kila siku hadi kua binaadamu kamili lakini ndani yake ni Artificial Intelligence.
 
Back
Top Bottom