Boti yazama Zanzibar

WATU 10 WAMENUSURIKA NA WENGINE WAWILI HAWAJULIKANI WALIPO, ILIKUWA INATOKA ZANZIBAR KWENDA PANGANI.

Source: ITV

NOTE:
Nilianzisha thread kwamba nimeota meli imezama Zanzibar baada ya sikukuu, na nikatoa maelezo ya kutosha lakini mods wakaitupa kapuni thread yangu.

Kwa kuwa ndoto ile imekuja kuwa ni kweli, mods fanyeni mpango muirudishe.
kwa nini usiote umekufa mwenyewe kuliko kuota wengine wamekufa maji? wewe ni replica wa sheikh yahaya nn??
 
Kuna haja ya kuanzisha intelijensia za kuchunguza vyombo vya majini badala ya hizi zilizopo zinazochunguza mikutano ya vyama vya siasa pekee :car:

vyombo vya majini vinachunguzwa na watu ambao maboss wao ndio wamiliki wa vyombo husika unategemea nn?
 
Ni kweli hiyo ndoto niliiona wewe unatisha ........Mod arudishe na akuombe radhi
 
WATU 10 WAMENUSURIKA NA WENGINE WAWILI HAWAJULIKANI WALIPO, ILIKUWA INATOKA ZANZIBAR KWENDA PANGANI.

Source: ITV

NOTE:
Nilianzisha thread kwamba nimeota meli imezama Zanzibar baada ya sikukuu, na nikatoa maelezo ya kutosha lakini mods wakaitupa kapuni thread yangu.

Kwa kuwa ndoto ile imekuja kuwa ni kweli, mods fanyeni mpango muirudishe.

Mkuu. Ukilitazama vizuri jina lako then ukaondoa baadhi ya herufi kamaDON na K Utabaki na ILLUMINAT Ambao ni memba wa freemasns. Na katikati ya jina kuna neno KILL.
Naomba nikuulize kidogo. Je majina haya na ndoto uliyo ota yana uhusiano wowote na ajali hii?
Haya ni mawazo yangu tu and do not quote me wrong. Tuondoe hasira na chuki ili tuelimishane.
 
Watu 10 wameokolewa wakiwemo raia wa kigeni 3. Watu 2 hawajulikani walipo. Source: Radio 1 Stereo.
 
Boti zile za mbao tokea zbar kwenda Pangani ndio imezama na wameokolewa watu 10 kati ya 12....hizo zinabeba shehena kubwa ,mbao,mkaa,fenicha,ng'ombe,mbatata etc....wafanya bishara wa mazao wanapita humo kila siku!!
Kama namuona mtu fulani bingwa wa kupokea pesa za maafa akiwa mlango wazi anasubiri......."serious joke"
 
mtabiri tutabirie na lini itakuwa mwisho wa ccm? ili nisimuuze jogoo wangu nimle wakati wa sherehe!
 
Kuna haja ya kuweka mkesha wa dini zote kwa ajili ya kuomba ajali zitoweke. This time is too much.
 
Hivi kila mtu akidai ndoto zake ziwe habari humu,si tutakuwa na jukwaa la ajabu sana hatimaye?
Poleni sana manusura wa ajali hiyo.
 
Modi ,umeondoa kitu hapa ,ila nimeona ufahamu wako kwa wale walio na akili finyu ,na hujiona wao ndio watu wa peponi.
 
Kwakweli kuja kufikia 2015 wa-Tanzania wengi tutakuwa na hali mbaya kama si kiuchumi basi kisaikolojia, majanga yametuzidi. ni juzijuzi tu MV-Stagik imeua watu kibao sasa na hii leo inazama!! si balaha hii.

MV spice islander ilizama baada ya idi el fitri, MV skagit ilizama siku mbili kabla ya ramadhani, hii nayo imezama baada ya idi el fitri, hii coincidence inahitaji kutazamwa, isijekuwa ni hujuma.
 
Aisee baba yangu embu acha uvivu 2ambie hiyo boti ilikuwa inatoka wapi kwenda wapi na imezama maeneo gani saa ngapi

naenda kunjwa mbege nitarudi,,nikute majibu

Huna haja ya kwenda kunywa manake hapo ushalewa tayari Mtoa mada kaweka vizuri ilipokuwa inatoka na ilipokuwa inaelekea
 
Back
Top Bottom