Bongo hiphop mistari ninayoikubali

Naona msafara wanafiki ni wengi nauli ninayo Mimi so hawafiki hata stendi by songa
 
Tenda wema nenda zako,atayekulipa Mungu
Sio unawekeza ulipwe usipolipwa majungu
Unanichekea usoni unananipondea kisogoni
Kuwa mkweli na mwazi keep it real wit your homies
Sio yule atayekuficha kama demu wako hajatulia
Kisa siku zilizopita yeye pia alimpitia
 
Watoto wanaona No kusema hata shikamoo wanakubali mi nimkubwa ila tatizo ni zao roho. Mr T touch
 
Uzembe kazini, huwa siruhusu/
Kama mpo makini,why mpate nusunusu/
 
Skiza, namba moja kushika sio kwa kasi ya Kobe/
Maji yakimwagika usizoe utazoa tope/
Mwenzako akisali, sali kabla ujaswaliwa/
Pandisha morale, morani aliyetahiriwa/
Mistari si haba vina vinajaza kibaba/
Medani za shaba nnapo simama kama langa/
Mc's wachanga wanajivika usupasta/
Kimbilia suti na nepi bado ujavaa/
Mali imepata daftari, hupotea bila khabari/
Nimechoka kuunguza utambi naunguza hadi kibatari/
Kwa mgongo wa chupa mafuta usinipake/
Mdomo usiwe mtumwa uliyeponzwa na ulimi wake/
Hivi ndivyo nnanyofanya/
Mama unayemlea Mwana kumkemea sio kumkanya/
Raaf, ninayezikosha namba/
Kwenye Giza siwezi kupotosha mwanga./


Hahahaha the best vibe all the time ..l like rap/hiphop aise!!!
 
Msanii™™ stamina ft fid q
Ngoma mwambie mwenzio

Wakuja rudi bush mji unahitaji waliosoma
Kicheche usikae uchi ukiwa umevaa sketi ya ngoma
Safisha kope mungu sio deusi
We hushangai mzungu mweupe ila kivuli cheusi
Binti usitoe mimba ukihisi utakosa soko
Zaa mtunze kinda mbinguni usichomwe moto
 
Wana wana DUNGAING ,
vitu vidogo bwana wacha kumaaind,
mind your business hauna hata HUNDAI,
Unavimba bar wakati benki inakudai,

........
 
Kwa Mungu hakuna majungu, mi na Mungu tu.
Navaa shati la jana ila gari nimebadili.

Subira haivuti bagi haigongi nyangi inavuta heri tu.
 
Yoo, nin mnataka mazee?/
Ma fans hawakujibu zamani walijibu rymes, leo imebaki aibu/
Rise na ku Flop na categories ma flow/
Maisha yanachange, Duke ana achia production/
M'bishi nina Range redioni sex corruption/

Haha #nyakati Nikk M'bishi ft Grace Matata.
 
Wanasema ugeuka mnyama sana anapotaka pesa cha ajabu anavuta bangi ila awazimii magangstar hampaki rangi donkey ili ageuke kuwa zebra ndo maana kabla hajaikoki JCB alisalenda.. Fid Q
 
Back
Top Bottom