Bomoabomoa imenikuta

Bomoabomoa imenikuta

Chukulia kila kibanda basi milioni 2 hivi nzima nyumba ngapi zitalipwa
Ndiyo mkuu kila kijumbba 1.2 au 1.5mln (police post type)
Watu wanakosea sawa ila serikali nayo ni sehemu ya makosa hapo,serikali ipo kwa ajili ya wananchi ingefanya vyovyote kuwaweka wananchi ktk hali nzuri kimtindo
Ubomoaji iliyofanyika mkwajuni ndy kwanza umeongeza uwizi,ukabaji, umalaya, wavutaji unga, etc
Hakuna kitu muhimu kama shelter Ukiwa na sehemu ya kulala ah hayo mambo mengine yatakuja taratibu
 
Inasikitisha sana... Pole mkuu.... na hao vibaraka wanaotumwa nahsi asilimia kubwa ni wapangaji hapa mjini... hawajui uchungu wa nyumba... polisi nao kwasababu wanaishi kota ndo kabisa hawaelewi uchungu wa nyumba...

Tupeane moyo... shida zina mwisho pia...
Polisi nao wanajua msiwaonee hapa jirani yangu kuna nyumba mbili za polisi tofauti na wanajeshi watatu nao nyumba zao zinavunjwa
 
Yaani mtu amejitahidi amejenga kakibanda chake na hela ilivyo ngumu mnambomolea. Wakati anajenga hadi anamaliza mlikuwa wapi? So sad!
 
Alafu nivipeleke wapi?
Utajua mwenyewe, heri nusu Shari kuliko Shari kamili. Chungu lakini ndo dawa. Tufike mahali tufate sheria na taratibu, ukishangilia flani katumbuliwa ndo hivyo hivyo nawe upokee machungu. Tulikuwa tumelala sana ngoja atunyooshe tukae vizuri
 
Wadau,

Kama kichwa cha habari kinavyojielezea bomoa bomoa imenikuta nyumba zetu mbili za familia zote kuvunjwa ni huzuni na vilio, kweli tunaisoma namba.

Pole sana ndugu, hayo yangeni kuta hata mimi leo kama ningemsikiliza bwana mmoja aliyetaka kuniuzia kiwancha hapo magomeni bondeni. Lakini nilifikiri sana na nikafuatilia shria hapo ikabidi hiyo deal niruke. watu walikua wakisema hakuna kitakachotokea, hii ni Tanzania kila kitu kinawezekana ni hela yako lakini sikusikiliza. Pole sana
 
Utawala wa sheria ni mgumu sana, hasa kama serikali zilizopita hazikuzingatia sheria. Wanaoumia ni wananchi...
 
wewe bomoa tu chanika yapo mapori kibao kiwanjwa laki mbili
master plan mpya inasemaje kuhusu haya mapori

nachoona mbeleni tena kuna waathirika

serikali imeshindwa kujipanga aftermath ya hawa wanaovunjiwa wanaenda kuanzisha squatters mpya
 
Nashangaa mtu anajenga nyumba ya milioni 50 kigogo sambusa!
 
Hivi walipokuwa wakijenga Serikali ilikuwa wapi? Tanzania ni sehemu hatari sana Duniani...!
 
Back
Top Bottom