Bomoa Bomoa ya TANROADS Morogoro Road Dar Es Salaam

Bomoa Bomoa ya TANROADS Morogoro Road Dar Es Salaam

Nilijua hii argument itakuja na ndio hapo utakapoona makengeza kwenye maamuzi
Upana wa barabara hii hubadirika kuanzia mwanzo wake hadi mwisho wake. Haupo constant. Hiyo ni kwa mujibu wa sheria zilizopo.

Kwangu mie nafahamu fidia ilishatolewa tangu enzi za mwinyi na mkapa kuanzia jangwani hadi kibamba kwa UPANA WA MAXIMUM MITA 60. Hilo la mita 120 ni geni masikioni.

Maeneo ya Jangwani hadi ubungo walilipwa kwa miya 30.
 
Je ni lini malipo haya yalifanywa? ni watu wangapi walilipwa? je walipaswa kuhamia wapi? je kuna orodha ya waliolipwa na uthibitisho wa malipo hayo?

Je walifanyiwa fidia walikuwa wamejenga upande gani wa barabara ya Morogoro? kabla ya kufika ubungo au baada ya kupita ubungo?

Mchakato, mkakati na mpango wa kujenga/kupanua barabara ya Morogoro ulianza lini na unapangwa umalizike lini?
Waliolipwa wengi walihama WAKAWAUZIA WAKUJA
 
Ukitazama sana, nia nzuri na ya manufaa makubwa ya mbeleni inaingia madoa na kuzaa chuki kutokana na namna inavyotekelezwa.

Kuna watu wamekaa maeneo hayo miaka 40 sasa, leo unakuja wahamisha kibabe bila kuwapa sehemu mpya au kuwapa haki stahiki ya kufidia wahamie mahali kupya.

Basi wafanyiwe thamani ya mali zao na Serikali iwape nyumba za NHC zilizokamilika kama fidia ya kuhamishwa na kubomolewa nyumba!
Mkuu Rev upo very correct hawa watu wapewe fidia inayostahili.

Nimeongea na jamaa zangu wanaoishi Kimara Stop Over asubuhi leo walikuwa wanaelekea Mahakamani kwani wakazi wote ambao wapo kwenye hati hati ya kuvunjiwa wameambiwa wawepo Mahakamani asub.

Yani hili pepo la uharibifu mpaka litakapo maliza awamu yake sijui wangapi watakuwa wamesalimika.
 
Ngosha,

Naafiki kuna waliomo na wasiokuwemo. Hapa lazima Serikali itumie haki,busara na utu kufanya uamuzi wake ili kila mtu apate haki yake anayostahili.

Wale ambao walilipwa fidia wakazinywa na wakabakia watambuliwe na iwe ni shauri yao kupata fidia. Wapewe muda muafaka wenye utu kuhama.

Wale ambao hawakulipwa fidia, lakini mali zao zisizohamishika ziko kwenye maeneo yaliyopimwa na wizara ya ardhi katika ramani zake za mipango miji, wapewe haki yao ya fidia pamoja na kupewa maeneo mapya ya kuhama,nao wapewe muda muafaka wa kuhama.

Wale ambao walivamia maeneo,hawana hati walaaina yeyote ya utambulisho kuwa walipewa ardhi na ikasajiliwa na kijiji, wizara, nao wapewe muda muafaka kuhakikisha wanahama.

Muda muafaka kwa makundi yote haya matatu uwe walau miezi 18-24, ili watu waweze kupata mahali papya pa kuweka makazi mapya.
Mkuu unatania. Muda wa miezi 24?

Maendeleo yasimame kwa miaka 2 kusubiri wavunja sheria wahame?

Hao wavamizi walishaambiwa wahame ZAIDI YA MIAKA 20 SASA tangu enzi za mzee RUKSA. Kwa sasa wataisoma namba.

Watanzania tuliomba kuwa na Rais mwenye MAAMUZI sasa tumempata TUNALALAMIKA.

HATUJUI NINI TUNATAKA.
 
Waliolipwa wengi walihama WAKAWAUZIA WAKUJA
Na hili ndilo tatizo lililopo.Nawajua watu wengi walilipwa pembezoni na wao wakawauzia wengine kinyemela.
Ila kuna tatizo la Utata wa upana wa barabara,haijulikani ni mita 30,60 au 90.
 
Na hili ndilo tatizo lililopo.Nawajua watu wengi walilipwa pembezoni na wao wakawauzia wengine kinyemela.
Ila kuna tatizo la Utata wa upana wa barabara,haijulikani ni mita 30,60 au 90.
Upana wa barabara upo kisheria na ni mita 30 hadi 60 kulingana na eneo husika.
 
13. Inasemekana mpango wa kupanua barabara hii kutoka Ubungo uko hati hati kutokanana kukosekana kwa fedha na kipaumbele kupelekwa maeneo mengine ya nchi yananayohitaji upanuzi wa barabara, fedha na kipaumbele kuwekwa barabara ya kutoka daraja la kigamboni, fly over za Tazara na Ubungo, Daraja jipya kutoka Aga Khan mpaka Coco Beach, Bandari ya Bagamoyo, Reli mpya na miradi mingine ya miundo mbinu nchini. Mradi unasemekana umesimama kwa kati ya miaka mitano hadi saba na hivyo kuweza kutoa fursa njema kwa mipango inayoeleweka kufanyika ikiwa na kuwapa wakazi watakaoathirika maeneo mapya ya kuhamia na fidia.

Kwa kutazamo hayo mambo 13 niliyataja hapo juu, ni wazi kuna ulazima wa jambo hili kufanywa kwa umakini, haki na kuthamini utu na si kufanyiwa upambe na ushabiki wa kisiasa.

Mkuu Kishoka, Palipopigiwa mstari soma hotuba ya waziri hapa chini ukurasa wa 161.

On the other end wakuu tuwe makini kwani vishoka wengi wamewaingiza watu wengi mikengeni kwa kujua ama kutokujua. Vishoka wako kila kona, TANESCO, Ardhi, Uhamiaji kwenye Paspoti, kutafuta kazi ktk taasisi za serikali n.k

Sehemu ya hotuba naiweka hapa chini:

======================================================
Upanuzi wa Barabara ya JNIA – Pugu (km 8) kuwa njia sita umetengewa jumla ya Shilingi milioni 122.00 katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tatu (BRT Phase III) kwa kuwa barabara hii ni sehemu ya mradi huo. Upanuzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (km 25.7) ikijumuisha Upanuzi wa Madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji umetengewa jumla ya Shilingi milioni 122.00 kwa ajili ya maandalizi ya upanuzi wa barabara na madaraja hayo. Mradi huu utatekelezwa kwenye awamu ya pili ya mradi wa Dar es Salaam Maritime Gateway chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.

=====================================================
 
Kupitia jibu hili zuri naomba wakili aiombe mahakama (kesi ikishafunguliwa) ihamie eneo la tukio wapime hizo meters wanazozitaka za hifadhi ya barabara kutokea mwanzo wa barabara.
Hapo Mpaka Lumumba na UVCCM hazitosalimika.
 
Mkuu Kishoka, Palipopigiwa mstari soma hotuba ya waziri hapa chini ukurasa wa 161.

On the other end wakuu tuwe makini kwani vishoka wengi wamewaingiza watu wengi mikengeni kwa kujua ama kutokujua. Vishoka wako kila kona, TANESCO, Ardhi, Uhamiaji kwenye Paspoti, kutafuta kazi ktk taasisi za serikali n.k

Sehemu ya hotuba naiweka hapa chini:

======================================================
Upanuzi wa Barabara ya JNIA – Pugu (km 8) kuwa njia sita umetengewa jumla ya Shilingi milioni 122.00 katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Tatu (BRT Phase III) kwa kuwa barabara hii ni sehemu ya mradi huo. Upanuzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (km 25.7) ikijumuisha Upanuzi wa Madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji umetengewa jumla ya Shilingi milioni 122.00 kwa ajili ya maandalizi ya upanuzi wa barabara na madaraja hayo. Mradi huu utatekelezwa kwenye awamu ya pili ya mradi wa Dar es Salaam Maritime Gateway chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia.

=====================================================
Milion 122? Sijaelewa! Haya maandalizi tafsiri yake nini? Kusogeza magreda site au?
 
Lakini nakumbuka wote waliojenga barabara ya Morogoro road walilipwa miaka mingi iliyopita fidia yao.

Hao wanaodai sasa wamejenga baada ya malipo kufanyika na ramani ipo mamlaka husika kwa ushahidi.

Uwezekano wa kulipwa fidia unaweza kuwa mdogo sana kwa wenye nyumba unless otherwise


Mkuu:
Fidia unayo zungumzia ni hadi mita 30 tu kutoka katikati ya Barabara kuu zaidi ya hapo hakuna fidia yeyote iliyo lipwa.
 
Ndugu Rev. Kishoka, Point # 13 ndo umeharibu,
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

13. Inasemekana mpango wa kupanua barabara hii kutoka Ubungo uko hati hati kutokanana kukosekana kwa fedha na kipaumbele kupelekwa maeneo mengine ya nchi yananayohitaji upanuzi wa barabara, fedha na kipaumbele kuwekwa barabara ya kutoka daraja la kigamboni, fly over za Tazara na Ubungo, Daraja jipya kutoka Aga Khan mpaka Coco Beach, Bandari ya Bagamoyo, Reli mpya na miradi mingine ya miundo mbinu nchini.
xxxxxxxx
unaishi kwa hisia "inasemekana"
 
sheria ipo wazi na hata kwenye hiyo kesi serikari ilishinda ,hata rufaa iliyo katwa ,serikali ilishinda.Ila kuna watu wamewauzia wajinga barabarani.na waowakanunua.

Msidanganywealama za roadi reserve ziko morogoro road tangu enzi za mkoloni,alama zikp,ilikuwa miti na becon ziko morogororad yote .Ila watu wamezizarau na kujenga ndani yake.
Nasisitiza alama ziko mimi nimeziona miti na becon watu wamevamia makusudi.
Ni kesi ipi hiyo serikali ilishinda ,maana ukweli serikali ilishindwa tena ikatakiwa kulipa fidia.
 
Ndugu Rev. Kishoka, Point # 13 ndo umeharibu,
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

13. Inasemekana mpango wa kupanua barabara hii kutoka Ubungo uko hati hati kutokanana kukosekana kwa fedha na kipaumbele kupelekwa maeneo mengine ya nchi yananayohitaji upanuzi wa barabara, fedha na kipaumbele kuwekwa barabara ya kutoka daraja la kigamboni, fly over za Tazara na Ubungo, Daraja jipya kutoka Aga Khan mpaka Coco Beach, Bandari ya Bagamoyo, Reli mpya na miradi mingine ya miundo mbinu nchini.
xxxxxxxx
unaishi kwa hisia "inasemekana"
Wewe ndo umeingia chaka kabisa inaonekana hujasoma matupio yote hili ameshaliweka bayana baada ya kuulizwa.Soma uzi wote tangia mwanzo na wachangiaji wengine uone sababu ya kulitumia hilo neno.
 
Kwa mienendo hii, ni bora tukahama hii sayari dunia tuwaachie miji yao na ardhi uchwara maana, sheria zao zinabadilika kama anga.

Inakera Sana, viongozi wanapokosa utu na hekima juu ya maamuzi yao kwa wale wanaowaongoza.

Japo, miundombinu ni muhimu, lakini utekelezwaji usiwe wa kuwakomoa wananchi .
 
Kwani huyoo nabii.. Anataka kujenga mto mpaka.. Atake kuchukua eneo kubwa kiasi hicho? Watu wanaishi hapo generation kwa generation yeye hata hajulikani ktk hii Tanzania.. Yuko kwao chato huko.. Alafu unazuka..tu na roho yako ya uharibifu usio na tija kabisa kabisa yaan mmmhh..
 
Lakini nakumbuka wote waliojenga barabara ya Morogoro road walilipwa miaka mingi iliyopita fidia yao.

Hao wanaodai sasa wamejenga baada ya malipo kufanyika na ramani ipo mamlaka husika kwa ushahidi.

Uwezekano wa kulipwa fidia unaweza kuwa mdogo sana kwa wenye nyumba unless otherwise

Ni vizuri ukajua kwamba ni kweli kila wakati mahitaji yanapokuwa ni lazima, basi Serikali hutwaa ardhi kukidhi matakwa hayo, na kwa ajili hii hulipa fidia. Sehemu inayozungumziwa imebadilishwa na Sheria ya 2007 na hasa kanuni chini ya sheria hio za 2009 na eneo la kama kilomita 20 tu ndio linahusu upana wa 120m. Kwa uhakika wananchi wale wanastahili fidia kwani barabara imewafuata.- Nukuu za Road Regulations za 2009 hizi hapa

upload_2017-5-15_13-57-15.png
 
Back
Top Bottom