Bomoa Bomoa ya TANROADS Morogoro Road Dar Es Salaam

Bomoa Bomoa ya TANROADS Morogoro Road Dar Es Salaam

Mkuu hapa ndo tunakosea. Sheria ipo ifuatwe.

Serikali haina wajibu wa kukukataza wewe kujenga au kutojenga. Ni jukumu lako kujiridhisha kama sheria husika imefuatwa. Huwezi ukajenga ..halafu kesho unauliza eti serikali ilikuwa wapi kipindi najenga. It is your fault. Na nimeona wengi wakiumia kwa approach hii.

Kawa wasemavyo wanasheria. Ignorance of the law is no defence.
What if wamepewa hati na kabla ya kujenga ramani imepitishwa na halmashauri na kila awamu ya ujenzi imekuwa approved
 
Ila tu niseme kwamba kuna roho za uharibifu zimetajwa mpaka kwenye misahafu, hili ni pepo baya sana ....daima halitengenezi bali linaharibu na likitengeneza kitu hakitakosa kuwa na walakini mkubwa.... Hiyo ndio roho ya uharibifu ilivyo
Tunahitaji kuwa na barabara pana eneo husika Lakini hekima na utu vitawale watu walipwe fidia waondoke kwa amani ubabe hautatufikisha popote
Tanzania Kupata Fidia Iliyo Kamilika Ni swala Gumu Sana

Kama rambi rambi Wamegawana Izo Pesa fidia wakupe Tuu kirahis
 
Juzi jamaa yangu nyumba zake zilibomolewa hapo hapo Kibamba. Alikuwa amepata NSSF yake akaamua awe mjasiriamali kwa kuanzisha biashara. Zote zilifyekwa.

WaTanzania tuna asili ya ku-ignore sheria especially pale ambapo hazitekelezwi (nakumbuka jamaa yangu nilimwambia kabisa..Mkuu hebu angalia sheria inasemaje kuweka hela yako ya maana sehemu kama hii-it might be road reserve. Alichonijibu ni kwamba..mipango ya serikali ni ya mda mrefu kwa hiyo barabara watajenga ila siyo leo wala kesho). The rest is history.

Mfano DSM watu wenye hela zao na influence..wamejenga almost baharini kabisa. na vibali (vingi vya figisu) wanavyo. Lakini sheria za kimataifa na za Tanzania ziko wazi. Ufukwe wa Bahari mpaka sehemu ya ujenzi/maendeleo ni mita 60! Sasa kama wengi tunavyojua wanaoishi baharini ni wenye nazo. Lakini kesho Magufuli au mwingine akiamka akasema wote walio ndani ya mita 60 wabomoe nyumba zao..utaona vilio na kudai fidia. Lakini hiyo sheria iko kwenye vitabu miaka na miaka. Ni mambo mengi ambayo tunafanya bila kuzingatia sheria. Refer: Mama Lwakatare kujenga baharini Mbezi beach , Matias Manga wa Arusha kujenga Hotel ya Kimataifa barabarani nk sehemu ambazo haziruhusiwi. Lakini kwa vile tunaweza kuwahonga wanaotoa vibali we do it knowing kwamba hatutasumbuliwa.

Serikali ina mapungufu yake na sometimes inatumia ubabe. Lakini lazima tujue DSM ya leo siyo dsm ya miaka 50 au 100 ijayo. Lazima tupange mipango tukifikiria vizazi na vizazi vijavyo. Imagine mtu aliye-plan mita 60 miaka hiyo DSM haina hata wakazi laki tano! But they did that with an eye on the future. waliopanga leo hawapo. na wala hata huo uwezo wa kujenga barabara hawakuwa nao kipindi hicho.

In all: Katika nchi yoyote ukitaka kuishi vizuri na salama, jifunze kuheshimu na kufuata sheria. Utafanikiwa. WaTanzania wengi hatuheshimu sheria ndo maana mambo yetu yanakwenda hovyo hovyo. Kila kitu tunaweka siasa au kutaka huruma za hiyo hiyo sheria!
Naamini watakuwa wamekuelewa sana.
 
Sheria ya kikoloni1920 ilikuwa meta 120 kutokea katikati ya barabara,je kwanini ilibadirishwa kuwa 60 na pengine 30 meters?
Aliebadirisha sheria yaani serikali inawajibika kulipa fidia.
 
ikiwa ni hali sawa, lakini kwa maelezo hayo juu hapo, nafikiri nizaidi ya ushetani wa mioyo yetu inavyotutuma kufanya na kukoma jamii fulani.....
 
What if wamepewa hati na kabla ya kujenga ramani imepitishwa na halmashauri na kila awamu ya ujenzi imekuwa approved
Kama wapo wa aina hiyo ni wachache sana, jinsi tunavyofanya mambo yetu ni hovyo hovyo tu. Nyumba zinajengwa kama uyoga na ukifuatilia kwa undani hakuna hata mwenye kibali cha ujenzi. Ukiuziwa eneo, kesho unaanza msingi hata kujisumbua kidogo kuona mamlaka za eneo husika hatufanyi!! Tuna tatizo kubwa sana, na tutazidi kulalamika kila siku
 
Ujenzi wa barabara ya Dsm hadi mlandizi unatekelezwa kwa maslahi mapana ya wananchi walio wengi, hivyo kamwe huwezi kukwamisha maslahi ya wengi kwa kuwalinda wachache!!!
lazima barabara zijengwe kwa maendeleo ya wengi!!
 
Juzi jamaa yangu nyumba zake zilibomolewa hapo hapo Kibamba. Alikuwa amepata NSSF yake akaamua awe mjasiriamali kwa kuanzisha biashara. Zote zilifyekwa.

WaTanzania tuna asili ya ku-ignore sheria especially pale ambapo hazitekelezwi (nakumbuka jamaa yangu nilimwambia kabisa..Mkuu hebu angalia sheria inasemaje kuweka hela yako ya maana sehemu kama hii-it might be road reserve. Alichonijibu ni kwamba..mipango ya serikali ni ya mda mrefu kwa hiyo barabara watajenga ila siyo leo wala kesho). The rest is history.

Mfano DSM watu wenye hela zao na influence..wamejenga almost baharini kabisa. na vibali (vingi vya figisu) wanavyo. Lakini sheria za kimataifa na za Tanzania ziko wazi. Ufukwe wa Bahari mpaka sehemu ya ujenzi/maendeleo ni mita 60! Sasa kama wengi tunavyojua wanaoishi baharini ni wenye nazo. Lakini kesho Magufuli au mwingine akiamka akasema wote walio ndani ya mita 60 wabomoe nyumba zao..utaona vilio na kudai fidia. Lakini hiyo sheria iko kwenye vitabu miaka na miaka. Ni mambo mengi ambayo tunafanya bila kuzingatia sheria. Refer: Mama Lwakatare kujenga baharini Mbezi beach , Matias Manga wa Arusha kujenga Hotel ya Kimataifa barabarani nk sehemu ambazo haziruhusiwi. Lakini kwa vile tunaweza kuwahonga wanaotoa vibali we do it knowing kwamba hatutasumbuliwa.

Serikali ina mapungufu yake na sometimes inatumia ubabe. Lakini lazima tujue DSM ya leo siyo dsm ya miaka 50 au 100 ijayo. Lazima tupange mipango tukifikiria vizazi na vizazi vijavyo. Imagine mtu aliye-plan mita 60 miaka hiyo DSM haina hata wakazi laki tano! But they did that with an eye on the future. waliopanga leo hawapo. na wala hata huo uwezo wa kujenga barabara hawakuwa nao kipindi hicho.

In all: Katika nchi yoyote ukitaka kuishi vizuri na salama, jifunze kuheshimu na kufuata sheria. Utafanikiwa. WaTanzania wengi hatuheshimu sheria ndo maana mambo yetu yanakwenda hovyo hovyo. Kila kitu tunaweka siasa au kutaka huruma za hiyo hiyo sheria!
Mkuu ukipita Morogoro road kuanzia ubungo to kibamba utaona mapango makubwa yaliyopo pale kimara yanayoonyesha eneo la barabara.Pili wenye akili zao hawajajenga barabarani ndo maana huoni nyumba nzuri sana barabarani
 
What if wamepewa hati na kabla ya kujenga ramani imepitishwa na halmashauri na kila awamu ya ujenzi imekuwa approved

The underlined is clear. Ingawa na wewe hujui. Lakini kama ndo hivyo sheria ziko wazi. ukiwa na hati ya serikali utapewa haki yako. As simple as that.
 
Mkuu nakubaliana na wewe ila umekuwa mkali sana.....hahahaha
Masanja matatizo yote haya yanakuja sababu ya upole wa serikali zilizo pita.nyumba za enzi hizo zingevinjwa leo watu wangeogoa kujenga ndani ya hifadhi ya barabara.
Dawa ya jipu ni kulitumbua tu.
Si unaona watu wanauliza serikali ilikuwa wapi maana yake mbona haikuchukua hatua.
 
Lakini nakumbuka wote waliojenga barabara ya Morogoro road walilipwa miaka mingi iliyopita fidia yao.

Hao wanaodai sasa wamejenga baada ya malipo kufanyika na ramani ipo mamlaka husika kwa ushahidi.

Uwezekano wa kulipwa fidia unaweza kuwa mdogo sana kwa wenye nyumba unless otherwise
Ni kweli wengi walipewa viwanja eneo la mbweni kunaitwa ubungo maji
 
Tanroad waje kujibu na kuweka mambo sawa. Ningependa kusikia upande wao pia wanasemaje.
 
Siku barabara ya kupitia baharini coco beach ikipingwa ndio itakuwa mkombozi wa uaribifu wa kodi za wananchi. Badala ya mwendo kasi ijengwe reli kutoka mnazi mmoja mpaka bagamoyo dar es tutasahau foleni gharama za daraja hili ni ghali.
 
Mtazamo wangu:

Hii nguvu kubwa ya kubomoa hizi nyumba inatokana na matajiri wanaotaka kujenga na kuendesha hii barabara kwa njia ya ushirikiano na serikali lakini kwa kutoza ushuru watumiaji wa hii barabara...

Ukiangalia gharama za ujenzi wa hii barabara kwa vyovyote vile wawekezaji hawatarudisha fedha zao kwa muda mfupi pia kwa kuzingatia sera nyingine za serikali kama ujenzi wa reli mpya na kituo cha magari makubwa nje ya jiji na pia serikali kuhamia dodoma...

Hii ardhi inayotafutwa bila fidia ndiyo mahali watakapopiga fedha...serikali ikisitisha ujenzi wa hii barabara kwa ubia utaona kabisa suala la kubomolea watu mita 121.5 kila upande litaisha
 
Back
Top Bottom