Nimekuuliza hili swali sababu kwenye comment yako umeitaja kazi yake na mwisho unasema ati anataka huruma ya wananchi kwa kushambulia watu. Unless unajua nini kazi ya mwandishi wa habari za uchunguzi huwezi kuandika ulichokiandika. Kwa taaluma nyingine sijui ungeuliza kwanini mpasuaji hakubaki kuwa GP tu agawe vidonge na kuchoma watu sindano badala ya ku specialise. Comment yangu hakumaanisha kukushusha hadhi bali kukuasa kuthamini taaluma za wstu. Martin Luther King II kulikua na watu kama ninyi walikua wanamdhihaki lakini leo hii wote mnaunua umujimu wake
Mkuu yule si mwandishi wa habari za kiuchunguzi.
Yule ni mchambuzi wa mambo ya kisiasa.
Anyway lets get back to the point. Tufanye yeye ni muandishi wa habari za kiuchunguzi. Hivyo anajuwa anachokifanya ni kama kutembea kwenye eneo ambalo watu wanapigana vita huku risasi zikirushwa ovyo. He may find himself caught in cross fire.
Kama hiyo ni taaluma yake aliyo somea anapaswa kujua ni kazi ya hatari sana sababu unachezea ulaji/maslahi ya watu.
Katika kulielewa hilo watu waliosomea taaluma hiyo ya habari za kiuchunguzi kuna protocol (sijui niite protokali au itifaki) flani zimewekwa ili kujilinda usidhuriwe kirahisi kama inavyotokea kwake.
Umeona jinsi mwandishi fulani wa 'Ze-ikonomi' alivyo chukuliwa kwa shida nyumbani kwake kiasi kwamba ilibidi walio mchukuwa waseme wamechukua na hakudhuriwa?
Uliwaona wale waandishi wa kimataifa watetezi wa waandishi wa habari sijui toka SA na nchi jirani walivyo chukuliwa kwa shida na kurudishwa kwa namna ile?
Sababu kubwa hao walikuwa wanajua protocol na walizifuata.
Sio kama huyu Bollen Ngeti mara kadhaa anatekwa(au anasingizia kutekwa) kirahisi sana na kurudishwa kirahisi mno, huyu anatumiwa na wajanja ambao nao ni makanjanja wanamuuza kwa kutompa ulinzi.
What I was doing in that comment is just stating the obvious, kwamba kazi anayofanya anajuwa ni ya hatari na nini kitamtokea hivyo hasipo chukuwa hatua au tahadhari yakimkuta yanayo mkuta hatakiwi kuja kulia lia kwa wananchi. Ipo siku anaweza kudhuriwa pakubwa na hata wananchi wakija kumlilia haitabadili kitu atakuwa kashamezwa na chatu hawezi au watu hawawezi kubadili kitu.
Alafu hapa lazima tuweke ukweli mmoja wazi, kuna mstari mdogo sana kati ya kuandika kwa malengo ya kulikomboa taifa na kuandika sababu ya kufanya propaganda za kumsaidia mtu flani ashike dola nawewe upate shibe yako na familia yako.
Waandishi njaa na vijarida au vigazeti uchwara vipo vingi sana, hasa baada ya kuzaliwa wanamtandao. Na vyama vingi vya vya siasa kupata pesa toka kwa mabeberu ya kuanzisha vijarida vya propaganda.
Siasa ni vita, ukijiingiza ktk siasa kwa namna yeyote ile ujue unajiingiza ktk vita.
Kuna mwana nadharia wa kivita wa kijerumani aitwae
Carl von Clausewitz alipendekeza tafsiri ya vita iwe ni
"Vita ni muendelezo wa siasa kwa njia nyingine"
Kwa namna hiyo kimantiki utaona kumbe siasa ni vita ktk njia nyingine au ktk sura nyingine.
Kama tukitafsiri siasa ni vita basi inabidi ukubaliane na nadharia nyingine ambayo ni ukweli tupu kwamba na hapa namnukuu tena
Carlo von Clausewitz
"watu wenye moyo mwema wanafikiri bila shaka kuna njia ya busara ya kumpokonya sila na kumshinda adui yako bila kumwaga damu nyingi, na huweza kudhania kwamba haya ndio hasa malengo halisi ya vita, Dhana hii hata ipendeze vipi masikioni mwa watu lakini sio dhana sahihi na uongo unaopaswa kuwekwa bayana. Vita ni biashara hatari sana kwamba makosa yatokanayo na fadhili(roho njema kwenye vita yoyote) ndio mabaya zaidi"
Maana yake nini hapa? Usitegemee fadhila toka kwa adui yako, pigana kwa mbinu au njia zozote umshinde adui wako, ushinde vita. Inashangaza kuona watu wengi hapa wanataka upande mmoja wa wanaopigana vita vya kupigania dola/madaraka uwe unawapa fadhila washindani(adui) wake. Atumie mbinu au njia safi huku yeye akiwekewa hadi sumu na kuombewa afe.
Au awape adui zake fadhila huku hao adui wanatafuta wafadhili (mabeberu) waje wammalize anae takiwa kutoa fadhila kama alivyomalizwa Ghadaf au Saddam Hussein.
Vita haijui mipaka (War knows no boundaries) hivyo huwezi kumpangia adui yako mipaka au mbinu za kushinda vita dhidi yako, hakuna huruma ktk vita. Ukiingia vitani hakuna huruma wala busara zaidi ya kuhakikisha unashinda vita. Iwe kwa kutumia bunduki, maneno ya mdomoni au kalamu kwenye maandishi ya vitabuni, mitandaoni au magazetini.
Mfadhili wa Bollen Ngeti kama angepata nafasi ya kumuondoa adui wake ofisi kuu hata kwa kumuondoa duniani kwa sumu au risasi angeitumia nafasi hiyo haraka sana, vivyo hivyo huyo mtu/watu wa ofisi kuu akipata/wakipata nafasi ya kumshinda Bollen Ngeti na/au mfadhili wake basi ataitumia/wataitumia hiyo nafasi by any means necessary.